Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumapili, 16 Novemba 2014

MAFUA YA NDEGE YATHUBITISHWA UINGEREZA


Ndege wanaofugwa wanakabiliwa na milipuko ya mafua ya ndege
Mlipuko wa mafua ya ndege umethibitishwa katika shamba moja la kuzalishia bata mashariki mwa Yorkshire, nchini Uingereza, wamesema maafisa.
Wizara ya Mazingira, Chakula na Masuala ya Vijijini (Defra) imesema hatari kwa afya ya umma ni ndogo sana. Ndege wasiohitajika wanaondolewa kutoka eneo hilo na eneo la kuwatenga limeandaliwa.
Tatizo hilo bado halijathibitishwa, lakini aina ya kirusi cha H5N1 hakijaweza kubainishwa na maafisa wa Defra.
Kirusi hicho husambaa kati ya ndege na katika matukio ya nadra, kinaweza kuwaathiri binadamu.
Picha ikimwonyesha mchuzi akiuza bata wake katika mtaa mmoja mjini Shanghai,China
Eneo la kuwatenga ndege lililopo kuzunguka shamba hilo litazuia ndege na kinyesi cha ndege ndani au nje ya eneo hilo.Ndege wote pia watatengwa.
Mlipuko wa ugonjwa hatari wa mafua ya ndege uligundulika Jumapili katika shamba moja nchini Uholanzi.
Tukio hili huko Yorkshire ni la kwanza nchini Uingereza tangu mwaka 2008, wakati ulipozuka. Mafua ya ndege daima yamekuwa yakidhibitiwa kikamilifu nchini Uingereza.
Msemaji wa wizara amesema: "tumethibitisha tukio la mafua ya ndege katika shamba la kuzalishia bata huko Yorkshire - afya za watu haziko katika hatari na hakuna hatari katika vyakula. "Tunachukua hatua za dharura katika kukabiliana na janga hili ambazo zinahusisha eneo la kilomita 10 na kuwaondoa ndege wote katika shamba kuzuia uwezekano wa kusambaa kwa mambukizi. Uchunguzi wa kina kuhusu ugonjwa huo unaendelea.
Tuna rekodi nzuri ya udhibiti na utokomezaji wa milipuko ya ugonjwa wa ndege iliyowahi kutokea siku za nyuma nchini Uingereza."

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni