Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Alhamisi, 26 Februari 2015

SAVILE AWADHALILISHA 63,HOSPITAL.

 
 Jimmy Savile, mtangazaji wa zamani wa BBC
Uchunguzi zaidi kuhusu mtangazaji maarufu wa zamani katika vipindi vya BBC, Jimmy Savile umebaini kuwa aliwadhalilisha watu 63 kutoka hospitali ya Stoke Mandeville, nchini Uingereza, lakini malalamiko rasmi yaliyotolewa kutokana na vitendo hivyo yalipuuzwa.
Uchunguzi huo umebaini kuwa sifa ya Savile kama "mpenda ngono" ilikuwa inafahamika miongoni mwa baadhi ya wafanyakazi, lakini tuhuma hizo huenda hazikuwafikia viongozi.
Malalamiko rasmi yaliyotolewa mwaka 1977 na baba wa muathirika yalitakiwa kuripotiwa polisi, imesema ripoti hiyo.
Ripoti nyingine imesema "matendo ya habari ya Savile " ingeweza kutokea tena.
Ripoti ya Stoke Mandeville imesema waathirika, walidhalilishwa kutoka mwaka 1968-92, walikuwa na umri wa kuanzia miaka minane hadi 40.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni