Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Alhamisi, 15 Januari 2015

MCHEZAJI WA ZAMANI KUWANIA URAISI FIFA


Sepp Blatter anawania tena urais ukiwa muhula wa tano
Mchezaji wa zamani wa Ufaransa David Ginola atasimama dhidi ya Sepp Blatter kuwania Urais wa shirikisho la kandanda duniani,Fifa.
Ingawa imetangazwa hivyo hakuna uhakika kama Ginola ataendelea na nia yake.
Anahitaji kuungwa mkono na vyama vitano vya soka na kigezo kingine anapaswa kuwa amejihusisha na soka kwa miaka miwili kati ya mitano iliyopita
Ginola mwenye miaka 47 , aliichezea Ufaransa, pia club ya nchi hiyo Paris St Germain kabla ya kujiunga na New Castle United kwa kitita cha Pauni milioni 2.5 mwaka 1995.
Zoezi la Uteuzi wa nafasi ya urais wa fifa litafungwa tarehe 29 mwezi huu.Blatter amekuwa Rais wa Fifa tangu mwaka 1998 anawania muhula wa tano sasa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni