Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Ijumaa, 10 Oktoba 2014

ASKARI WATATU WA USALAMA BARABARANI WAFUKUZWA KAZI

Jeshi la Polisi limewafukuza kazi askari watatu kwa utovu wa nidhamu mkoani Kagera.

Jeshi la Polisi mkoani Kagera limewafukuza kazi askari watatu wenye vyeo na nafasi mbalimbali katika jeshi hilo kutokana na utovu wa nidhamu na ukosefu wa maadili mema kazini.

Akiongea mjini Bukoba kamanda wa jeshi la Polisi mkoani Kagera Henri Mwaibambe amesema askari hao walipiga picha mbaya na kuziweka kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii na kwamba picha hiyo walipiga kinyume na maadili ya jeshi la Polisi ambapo ameongeza kuwa picha hiyo walipiga wakiwa kazini.

Kamanda Mwaibambe amewataja kwamajina askari wote waliofukuzwa kazi kuwa Mpaji Asuma Mwasumbi, Fadhili Linga, Veronika Nazaremo   wote walikuwa askari wa usalama barabarani.

Aidha kamanda Mwaibambe amesema maadili ya kijeshi yapo kisheria na askari wote wanafundishwa namna ya kuishi katika maisha ya utumishi wa jeshi la Polisi lakini kwa kitendo walichokifanya jeshi hilo limeamua kuchukua hatua ya kuwafukuza kazi ili liwefundisho kwa askari wengine.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni