Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Ijumaa, 3 Aprili 2015

LADY JAYDEE NA ATEMI WATOA KIBAO KIPYA.

 Wasanii Lady Jaydee na mwenzake Atemi
Msanii wa Kenya, Atemi na mwanamuziki wa Tanzania Lady Jaydee wametoa kibao kipya kwa jina 'MOYO'.
'Moyo' ni wimbo kuhusu mapenzi ya matukio tofauti .
Katika wimbo huu Atemi anasema kuwa haijalishi penzi lina mvuto wa kiasi gani mwishowe bado linasalia kuwa penzi.
Wimbo huo uliotungwa na Atemi Oyungu ni 'single' ya kwanza kutoka album yake mpya ya tatu.
Wimbo huo umeandaliwa na R-kay ambaye pia aliandaa wimbo mwengine wa Atemi 'Usijali' akiimba na Delvin Savara wa Sauti Sol.
CHANZO BBC.

YEME;JUMBA LA RAIS LAACHILIWA NA WAASI.

Jumba la rais wa Yemen 
Ripoti kutoka Yemen zinasema kuwa waasi wa Houthi wameondoka nyumba ya rais waliokuwa wameiteka katika mji muhimu wa kusini wa bandari ya Aden baada ya mshambulizi ya ndege za taifa la saudia kulenga eneo hilo.
Wapiganaji walio watiifu kwa rais Abd Rabbuh Mansur Hadi wanasema kuwa wamepokea zana za kijeshi zilizoangushwa kutoka ndege za kijeshi za saudia wakati ambapo mapigano yanaendelea katika mji huo.
China imewaondoa zaidi ya raia wa kigeni 200 kutoka bandari hiyo.
Makumi ya raia yameripotiwa kuuawa siku chache zilizopita katika mapigano ya Aden.
CHANZO  BBC

NYUKLIA;IRAN YAAPA KUTEKELEZA MAKUBALIANO.

Hassan Rouhani 
Rais wa Iran Hassan Rouhani amesema nchi yake itatekeleza wajibu wake kikamilifu kuhusiana na muafaka uliofikiwa kuhusiana na mpango wake wa kupata nguvu za nyuklia mradi tu wahusika wengine kwenye makubaliano hayo watekeleze wanayopasa kuyafanya.
Akihutubia taifa hilo kupitia runinga ya nchi hiyo, rais Rouhani ameongeza kusema mataifa 6 makuu duniani yaliyoshiriki katika majadiliano hayo walikubali kuwa Iran ina haki ya kuendelea na mpango huo ndani ya mipaka yake na bila kuhatarisha usalama wa mataifa mengine.
Chini ya makubaliano hayo Iran imekubali kupunguza kiwango cha mradi huo kwa zaidi ya theluthi mbili.
CHANZO BBC.

WAJIVUNA KUWA MAKAHABA AUSTRALIA.

Wafanya biashara ya ngono wakiwa kazini
Hivi umeshawahi kujiuliza kwamba wafanyabiashara ya ngono ni watu wa namna gani? Ama biashara hiyo ni biashara kama biashara zingine kivipi? Nchini Australia,maelfu ya wafanyabiashara ya ngono bila soni wameweka bayana namna wanavyotumia mitandao ya kijamii na kuueleza ulimwengu jinsi wanavyo fanikisha biashara hiyo.
Huwa hawachagui wateja,Mwanafunzi mwenzangu? Mwanasheria nimtakaye,mwanaharakati,binti yangu?dada yangu, mfanya biashara mwenzangu wa ngono? Familia yangu! Sihitaji msaada wao.
Huo ni baadhi ya maelfu ya ujumbe kutoka nchini Australia kwa wafanya biashara ya ngono wanaojieleza huku wakitumia ukurasa wa #facesofprostitution hashtag.Fukuto hili lilianza tangu mwishoni mwa juma lililopita katika Instagram na mfanya biashara wa ngono mwenye umri wa miaka 21 ambaye ni mhitimu wa masuala ya Historia anayejulikana kama Tilly Lawless.
Aliamua kuzungumzia blog moja iliyoamua kurudia kuweka kwenye ukurasa wake taarifa iliyorushwa wiki iliyopita katika ukurasa wa gazeti maarufu lenye kuandika habari za akina mama liitwalo, Mamamia.Blog hiyo iliandika katika maadhimisho ya miaka ishirini na mitano mkutano wa wafanya biashara ya ngono na filamu yao ya ‘prince-charming Pretty Woman' na kudai kuwa shuhguli nzima ya biashara ya ngono haina mvuto kama ilivyo katika filamu hiyo.
Tilly Lawless alichukizwa na namna taarifa hiyo ilivyoweka mambo kirahisi rahisi na kuijumuisha biashara ya ngono na kuiona biashara hiyo kama yenye madhara .bibi huyo anashuhudia kuwa ameifanya biashara hiyo ya ngono kwa miaka miwili lakini amejulikana hadharani miezi miwili iliyopita mjini Sydney,mahali ambako biashara ya ngono ruksa kuifanya kisheria . na alichukua maamuzi ya kuweka picha yake bayana katika ukurasa wake wa Instagram kuonesha uzuri na upande wa pili wa biashara ya ngono ,sura ya mwanamke mrembo,ambaye anajitambua na aliyechagua kuwa mfanyabiashara ya ngono kwa mantiki ya kukipinga kilichoandikwa katika jarida la Mamamia na blog pia.
CHANZO BBC.

FAMILIA KUTAMBUA MIILI YAWALIOUAWA KENYA.

Wanafunzi wa chuo kikuu cha Garissa 
Familia za wanafunzi waliouawa katika chuo kikuu kazkazini mashariki mwa Kenya zimeenda katika eneo la mkasa ili kuitambua miili ya waliouawa.
Zaidi ya watu 140 waliuawa katika shambulizi lililotekelezwa na wapiganaji wa Al shabaab mjini Garissa siku ya alhamisi ambapo wapiganaji hao waliwatenganisha wanafunzi hao kwa misingi ya kidini kabla ya kuwaua wanafunzi wa kikristo.
Wakati huohuo mamlaka nchini Kenya imetoa mabasi ili kuwasafirisha wanafunzi walionusurika hadi makwao,huku miili ya waliofariki ikisafirishwa hadi mjini Nairobi.
Rais wa Somali Hassan Sheikh Mohamoud,amesema kuwa Somalia na Kenya lazima ziimarishe ushirikiano wao dhidi ya Ugaidi baada ya shambulizi hilo.
CHANZO BBC.

ZIMBABWE; ZANU-PF CHAMTIMUA BIMUJURU.

Bi Joice Mujuru
Aliyekuwa makamu wa rais nchini Zimbabwe Joice Mujuru amefukuzwa katika chama tawala ZANU-PF.
Chama hicho kinasema alipanga njama za kumuondoa mamlakani rais Robert Mugabe mbali na kukiharibia jina chama hicho- madai ambayo ameyakana hapo mbeleni .
Bi Mujuru alipigana vita vya Guerilla pamoja na Mugabe miaka ya sabini dhidi ya uongozi wa weupe na alionekana kama mrithi wake,kabla ya kukosana naye mwaka uliopita swala lililomfanya kufutwa kazi kama makamu wa rais mnamo mwezi Disemba.
Waandishi wanasema alishtumiwa sana na mke wa Mugabe, Grace ambaye anaongoza wanawake katika chama hicho.
CHANZO BBC.

MTOTO MPYA AMTESA KIM KARDASHIAN.

Kim akimpa taarifa mumewe Kanye West juu ya tatizo linalomkabili.
Mwanamama nguli na nyota wa kipindi cha runinga cha The Keeping Up with the Kardashians,Kim West ambaye ana mtoto mwenye umri wa miezi 21 North West aliyezaa na mumewe Kanye West,imeelezwa na mumewe huyo Kanye ,mkewe hataki chochote katika ulimwengu huu zaidi ya kupata mtoto mwingine ,lakini madaktari wamemuonya anaweza kukabiliwa na hatari kiafya.
Katika kipande cha kipindi kinachofuata cha kipindi cha mwanamama huyo ambacho kitarushwa katika runinga ya E’ inayojihusisha na masuala ya burudani na huenda kipande hicho kitarushwa mwishoni mwa wiki hii ,kipande hicho kinamuonesha Kim akielezea alichoambiwa na daktari wake kuwa anajaribu kumficha Kanye West anachotakiwa kwenda kufanyiwa na madaktari kuondoa kitu kilichoko kwenye kizazi chake.
Na ilipobidi kumkabili mumewe huyo, ambaye ni nguli wa muziki wa tambo,alipomwambia juu ya suala hilo tete, alikubaliana nalo na kumwambia endapo atafanikiwa kupata mtoto wa pili atakuwa wa mwisho kwasababu kondo la uzazi linakua kwenye kizazi chake.

Mke wa Kanye West
lakini baadaye mrembo huyo alionekana kukata tamaa ya kupata mtoto mwingine,na akaeleza wazi kuwa alipokuwa mjamzito wa mtoto wao wa sasa North,alikuwa akiwaambia watu wake wa karibu kwamba hakuna kiwango cha pesa duniani atakachoweza kulipwa kurejea tena katika maumivu ya uchungu wa kuzaa.
Lakini,kwasasa hakuna kitu ninachokihitaji zaidi ulimwenguni kama kuwa mjamzito tena,nina pata hasira kidogo kwamba watoto wangu wataachana miaka kadhaa.
Siku za karibuni Kim alitoa ya moyoni kwa kueleza kwamba ulikuwa ni muujiza kuipata mimba ya mtoto wake North kwasababu madaktari walisha mwambia kuwa milele hataweza kubeba ujauzito .
chanzo bbc.