Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache
Msanii wa Kenya, Atemi na mwanamuziki wa Tanzania Lady Jaydee wametoa kibao kipya kwa jina 'MOYO'.
'Moyo' ni wimbo kuhusu mapenzi ya matukio tofauti .
Katika wimbo huu Atemi anasema kuwa haijalishi penzi lina mvuto wa kiasi gani mwishowe bado linasalia kuwa penzi.
Wimbo huo uliotungwa na Atemi Oyungu ni 'single' ya kwanza kutoka album yake mpya ya tatu.
Wimbo huo umeandaliwa na R-kay ambaye pia aliandaa wimbo mwengine wa Atemi 'Usijali' akiimba na Delvin Savara wa Sauti Sol.
CHANZO BBC.
Ripoti kutoka Yemen zinasema kuwa
waasi wa Houthi wameondoka nyumba ya rais waliokuwa wameiteka katika mji
muhimu wa kusini wa bandari ya Aden baada ya mshambulizi ya ndege za
taifa la saudia kulenga eneo hilo.
Wapiganaji walio watiifu kwa
rais Abd Rabbuh Mansur Hadi wanasema kuwa wamepokea zana za kijeshi
zilizoangushwa kutoka ndege za kijeshi za saudia wakati ambapo mapigano
yanaendelea katika mji huo.
China imewaondoa zaidi ya raia wa kigeni 200 kutoka bandari hiyo.
Makumi ya raia yameripotiwa kuuawa siku chache zilizopita katika mapigano ya Aden.
CHANZO BBC
Rais wa Iran Hassan Rouhani amesema
nchi yake itatekeleza wajibu wake kikamilifu kuhusiana na muafaka
uliofikiwa kuhusiana na mpango wake wa kupata nguvu za nyuklia mradi tu
wahusika wengine kwenye makubaliano hayo watekeleze wanayopasa
kuyafanya.
Akihutubia taifa hilo kupitia runinga ya nchi hiyo,
rais Rouhani ameongeza kusema mataifa 6 makuu duniani yaliyoshiriki
katika majadiliano hayo walikubali kuwa Iran ina haki ya kuendelea na
mpango huo ndani ya mipaka yake na bila kuhatarisha usalama wa mataifa
mengine.
Chini ya makubaliano hayo Iran imekubali kupunguza kiwango cha mradi huo kwa zaidi ya theluthi mbili.
CHANZO BBC.
Hivi umeshawahi kujiuliza kwamba
wafanyabiashara ya ngono ni watu wa namna gani? Ama biashara hiyo ni
biashara kama biashara zingine kivipi? Nchini Australia,maelfu ya
wafanyabiashara ya ngono bila soni wameweka bayana namna wanavyotumia
mitandao ya kijamii na kuueleza ulimwengu jinsi wanavyo fanikisha
biashara hiyo.
Huwa hawachagui wateja,Mwanafunzi mwenzangu?
Mwanasheria nimtakaye,mwanaharakati,binti yangu?dada yangu, mfanya
biashara mwenzangu wa ngono? Familia yangu! Sihitaji msaada wao.
Huo
ni baadhi ya maelfu ya ujumbe kutoka nchini Australia kwa wafanya
biashara ya ngono wanaojieleza huku wakitumia ukurasa wa
#facesofprostitution hashtag.Fukuto hili lilianza tangu mwishoni mwa
juma lililopita katika Instagram na mfanya biashara wa ngono mwenye umri
wa miaka 21 ambaye ni mhitimu wa masuala ya Historia anayejulikana kama
Tilly Lawless.
Aliamua kuzungumzia blog moja iliyoamua kurudia
kuweka kwenye ukurasa wake taarifa iliyorushwa wiki iliyopita katika
ukurasa wa gazeti maarufu lenye kuandika habari za akina mama liitwalo,
Mamamia.Blog hiyo iliandika katika maadhimisho ya miaka ishirini na
mitano mkutano wa wafanya biashara ya ngono na filamu yao ya
‘prince-charming Pretty Woman' na kudai kuwa shuhguli nzima ya biashara
ya ngono haina mvuto kama ilivyo katika filamu hiyo.
Tilly Lawless
alichukizwa na namna taarifa hiyo ilivyoweka mambo kirahisi rahisi na
kuijumuisha biashara ya ngono na kuiona biashara hiyo kama yenye madhara
.bibi huyo anashuhudia kuwa ameifanya biashara hiyo ya ngono kwa miaka
miwili lakini amejulikana hadharani miezi miwili iliyopita mjini
Sydney,mahali ambako biashara ya ngono ruksa kuifanya kisheria . na
alichukua maamuzi ya kuweka picha yake bayana katika ukurasa wake wa
Instagram kuonesha uzuri na upande wa pili wa biashara ya ngono ,sura ya
mwanamke mrembo,ambaye anajitambua na aliyechagua kuwa mfanyabiashara
ya ngono kwa mantiki ya kukipinga kilichoandikwa katika jarida la
Mamamia na blog pia.
CHANZO BBC.
Familia za wanafunzi waliouawa
katika chuo kikuu kazkazini mashariki mwa Kenya zimeenda katika eneo la
mkasa ili kuitambua miili ya waliouawa.
Zaidi ya watu 140 waliuawa
katika shambulizi lililotekelezwa na wapiganaji wa Al shabaab mjini
Garissa siku ya alhamisi ambapo wapiganaji hao waliwatenganisha
wanafunzi hao kwa misingi ya kidini kabla ya kuwaua wanafunzi wa
kikristo.
Wakati huohuo mamlaka nchini Kenya imetoa mabasi ili
kuwasafirisha wanafunzi walionusurika hadi makwao,huku miili ya
waliofariki ikisafirishwa hadi mjini Nairobi.
Rais wa Somali
Hassan Sheikh Mohamoud,amesema kuwa Somalia na Kenya lazima ziimarishe
ushirikiano wao dhidi ya Ugaidi baada ya shambulizi hilo.
CHANZO BBC.
Aliyekuwa makamu wa rais nchini Zimbabwe Joice Mujuru amefukuzwa katika chama tawala ZANU-PF.
Chama
hicho kinasema alipanga njama za kumuondoa mamlakani rais Robert Mugabe
mbali na kukiharibia jina chama hicho- madai ambayo ameyakana hapo
mbeleni .
Bi Mujuru alipigana vita vya Guerilla pamoja na Mugabe
miaka ya sabini dhidi ya uongozi wa weupe na alionekana kama mrithi
wake,kabla ya kukosana naye mwaka uliopita swala lililomfanya kufutwa
kazi kama makamu wa rais mnamo mwezi Disemba.
Waandishi wanasema alishtumiwa sana na mke wa Mugabe, Grace ambaye anaongoza wanawake katika chama hicho.
CHANZO BBC.
Kim akimpa taarifa mumewe Kanye West juu ya tatizo linalomkabili.
Mwanamama nguli na nyota wa kipindi
cha runinga cha The Keeping Up with the Kardashians,Kim West ambaye ana
mtoto mwenye umri wa miezi 21 North West aliyezaa na mumewe Kanye
West,imeelezwa na mumewe huyo Kanye ,mkewe hataki chochote katika
ulimwengu huu zaidi ya kupata mtoto mwingine ,lakini madaktari
wamemuonya anaweza kukabiliwa na hatari kiafya.
Katika kipande cha
kipindi kinachofuata cha kipindi cha mwanamama huyo ambacho kitarushwa
katika runinga ya E’ inayojihusisha na masuala ya burudani na huenda
kipande hicho kitarushwa mwishoni mwa wiki hii ,kipande hicho
kinamuonesha Kim akielezea alichoambiwa na daktari wake kuwa anajaribu
kumficha Kanye West anachotakiwa kwenda kufanyiwa na madaktari kuondoa
kitu kilichoko kwenye kizazi chake.
Na ilipobidi kumkabili mumewe
huyo, ambaye ni nguli wa muziki wa tambo,alipomwambia juu ya suala hilo
tete, alikubaliana nalo na kumwambia endapo atafanikiwa kupata mtoto wa
pili atakuwa wa mwisho kwasababu kondo la uzazi linakua kwenye kizazi
chake. Mke wa Kanye West
lakini baadaye mrembo huyo
alionekana kukata tamaa ya kupata mtoto mwingine,na akaeleza wazi kuwa
alipokuwa mjamzito wa mtoto wao wa sasa North,alikuwa akiwaambia watu
wake wa karibu kwamba hakuna kiwango cha pesa duniani atakachoweza
kulipwa kurejea tena katika maumivu ya uchungu wa kuzaa.
Lakini,kwasasa
hakuna kitu ninachokihitaji zaidi ulimwenguni kama kuwa mjamzito
tena,nina pata hasira kidogo kwamba watoto wangu wataachana miaka
kadhaa.
Siku za karibuni Kim alitoa ya moyoni kwa kueleza kwamba
ulikuwa ni muujiza kuipata mimba ya mtoto wake North kwasababu madaktari
walisha mwambia kuwa milele hataweza kubeba ujauzito .
chanzo bbc.