Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Ijumaa, 3 Aprili 2015

WAANDANA DHIDI YA AL-SHABAAB GARISSA.


Maandamano Garissa 
Wananchi wa mji wa Garissa nchini Kenya wamefanya maandamano kupinga vitendo vya kundi la Al Shabaab, lililoshambulia chuo kimoja kikuu mjini humo na kuwaua watu 147 wengi wao wakiwa wanafunzi hapo jana.
Waandamanaji pia wameelezea kutoridhika na vyombo vya usalama nchini humo wakisema havikuchukua hatua za kutosha kutoa ulinzi kwa waliouawa na kwa raia wengine kwa jumla.
Wazazi, jamaa na marafiki wa wanafunzi waliouawa katika chuo kikuu cha Garissa wamekuwa wakiendelea kuwasili katika eneo hilo kuitambua miili ya wapendwa wao.
Waliojeruhiwa wanaendelea kupata matibabu .

Garissa
Serikali ya Kenya imekuwa ikiwasafirisha manusura wa shambulio hilo kwa mabasi kuelekea makwao huku miili ya waliouawa ikisafirishwa mjini Nairobi.
Wakati huo huo rais wa Somalia, Hassan Sheikh Mohamoud, amesema Somalia na Kenya zinafaa kuimarisha uhusiano wao katika mapambano dhidi ya ugaidi.
Tamko hilo linajiri siku moja baada ya shambulio hilo la Alshaabab katika chuo kimoja kikuu mjini Garrisa.
chanzo bbc.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni