Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Alhamisi, 2 Aprili 2015

HABARI ZA HIVI PUNDE;-WATU 2 WAUAWA KUFUATIA SHAMBULIZI KENYA

Garissa Kenya 
Wapiganaji waliofunika nyuso zao wameshambulia eneo la chuo kikuu cha Garissa kaskazini mwa Kenya karibu na mpaka wa taifa hilo na Somalia.Milio mikali ya risasi pamoja na milipuko imesikika katika chuo kikuu cha Garissa mjini humo.
Maafisa wa usalama wa Kenya wamethibitisha kuwa watu wawili wamefariki huku wanne wakijeruhiwa.
Wakaazi wa eneo hilo wametakiwa kukaa mbali na eneo la chuo hicho.
Haijulikani ni nani aliyekusika na shambulizi hilo ,lakini kundi la wapiganaji wa Somalia Al shabaab limetekeleza misururu ya mashambulizi mjini Garissa pamoja na maeneo mengine ya Kenya tangu mwaka 2011 wakati wanajeshi wa kenya walipopelekwa Somalia.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni