Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatano, 1 Aprili 2015

BUHARI AAPA KULITOKOMEZA BOKO HARAM

Goodluck Jonathan na Muhammadu Buhari
Mshindi wa uchaguzi wa urais nchini Nigeria Muhammadu Buhari ameelezea mashambulizi yanayotekelezwa na kundi la wapiganaji wa Boko Haram kama tatizo kuu linalokabili taifa hilo.
Katika hotuba aliyotoa katika runinga za Nigeria,kiongozi huyo wa kijeshi zamani amesema kuwa serikali yake itafanya kila juhudi kuangamiza ugaidi.
Vilevile amesema kuwa atakabiliana na jinamizi la ufisadi.
Bwana Buhari ambaye anachukua wadhfa wa urais kuanzia mwezi ujao,alimsifu mpinzani wake na rais anayeondoka Goodluck Jonathan.
Alimtaja kuwa kiongozi anayehitaji heshima.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni