Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Ijumaa, 3 Aprili 2015

FAMILIA KUTAMBUA MIILI YAWALIOUAWA KENYA.

Wanafunzi wa chuo kikuu cha Garissa 
Familia za wanafunzi waliouawa katika chuo kikuu kazkazini mashariki mwa Kenya zimeenda katika eneo la mkasa ili kuitambua miili ya waliouawa.
Zaidi ya watu 140 waliuawa katika shambulizi lililotekelezwa na wapiganaji wa Al shabaab mjini Garissa siku ya alhamisi ambapo wapiganaji hao waliwatenganisha wanafunzi hao kwa misingi ya kidini kabla ya kuwaua wanafunzi wa kikristo.
Wakati huohuo mamlaka nchini Kenya imetoa mabasi ili kuwasafirisha wanafunzi walionusurika hadi makwao,huku miili ya waliofariki ikisafirishwa hadi mjini Nairobi.
Rais wa Somali Hassan Sheikh Mohamoud,amesema kuwa Somalia na Kenya lazima ziimarishe ushirikiano wao dhidi ya Ugaidi baada ya shambulizi hilo.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni