Kadinali Raymond Burke mwenye asili
ya Marekani ameenguliwa na Papa Francis katika wadhifa wake wa
mwenyekiti wa bodi katika kanisa katoliki,ametoa onyo kwamba kuna
viashiria vya kanisa hilo kuupigia chapuo ushoga, kauli hii Burke
aliiotoa wakati alipokuwa akihojiwa na tovuti moja ya Italy ya La Nuova
Bussola Quotidiana mara baada tu ya kuenguliwa kwenye wadhifa wake.
Mwandishi
wa BBC anasema hii ni ishara nyingine ya jinsi viongozi wa dini
waandamizi wanavyochukulia hatua juu ya masuala kama vile ushoga na
talaka , wakati wengine wanatakiwa kuyachukulia mambo kwa utuvu na
uangalifu wa hali ya juu.chanzo bbc.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni