Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Ijumaa, 3 Aprili 2015

LADY JAYDEE NA ATEMI WATOA KIBAO KIPYA.

 Wasanii Lady Jaydee na mwenzake Atemi
Msanii wa Kenya, Atemi na mwanamuziki wa Tanzania Lady Jaydee wametoa kibao kipya kwa jina 'MOYO'.
'Moyo' ni wimbo kuhusu mapenzi ya matukio tofauti .
Katika wimbo huu Atemi anasema kuwa haijalishi penzi lina mvuto wa kiasi gani mwishowe bado linasalia kuwa penzi.
Wimbo huo uliotungwa na Atemi Oyungu ni 'single' ya kwanza kutoka album yake mpya ya tatu.
Wimbo huo umeandaliwa na R-kay ambaye pia aliandaa wimbo mwengine wa Atemi 'Usijali' akiimba na Delvin Savara wa Sauti Sol.
CHANZO BBC.

YEME;JUMBA LA RAIS LAACHILIWA NA WAASI.

Jumba la rais wa Yemen 
Ripoti kutoka Yemen zinasema kuwa waasi wa Houthi wameondoka nyumba ya rais waliokuwa wameiteka katika mji muhimu wa kusini wa bandari ya Aden baada ya mshambulizi ya ndege za taifa la saudia kulenga eneo hilo.
Wapiganaji walio watiifu kwa rais Abd Rabbuh Mansur Hadi wanasema kuwa wamepokea zana za kijeshi zilizoangushwa kutoka ndege za kijeshi za saudia wakati ambapo mapigano yanaendelea katika mji huo.
China imewaondoa zaidi ya raia wa kigeni 200 kutoka bandari hiyo.
Makumi ya raia yameripotiwa kuuawa siku chache zilizopita katika mapigano ya Aden.
CHANZO  BBC

NYUKLIA;IRAN YAAPA KUTEKELEZA MAKUBALIANO.

Hassan Rouhani 
Rais wa Iran Hassan Rouhani amesema nchi yake itatekeleza wajibu wake kikamilifu kuhusiana na muafaka uliofikiwa kuhusiana na mpango wake wa kupata nguvu za nyuklia mradi tu wahusika wengine kwenye makubaliano hayo watekeleze wanayopasa kuyafanya.
Akihutubia taifa hilo kupitia runinga ya nchi hiyo, rais Rouhani ameongeza kusema mataifa 6 makuu duniani yaliyoshiriki katika majadiliano hayo walikubali kuwa Iran ina haki ya kuendelea na mpango huo ndani ya mipaka yake na bila kuhatarisha usalama wa mataifa mengine.
Chini ya makubaliano hayo Iran imekubali kupunguza kiwango cha mradi huo kwa zaidi ya theluthi mbili.
CHANZO BBC.

WAJIVUNA KUWA MAKAHABA AUSTRALIA.

Wafanya biashara ya ngono wakiwa kazini
Hivi umeshawahi kujiuliza kwamba wafanyabiashara ya ngono ni watu wa namna gani? Ama biashara hiyo ni biashara kama biashara zingine kivipi? Nchini Australia,maelfu ya wafanyabiashara ya ngono bila soni wameweka bayana namna wanavyotumia mitandao ya kijamii na kuueleza ulimwengu jinsi wanavyo fanikisha biashara hiyo.
Huwa hawachagui wateja,Mwanafunzi mwenzangu? Mwanasheria nimtakaye,mwanaharakati,binti yangu?dada yangu, mfanya biashara mwenzangu wa ngono? Familia yangu! Sihitaji msaada wao.
Huo ni baadhi ya maelfu ya ujumbe kutoka nchini Australia kwa wafanya biashara ya ngono wanaojieleza huku wakitumia ukurasa wa #facesofprostitution hashtag.Fukuto hili lilianza tangu mwishoni mwa juma lililopita katika Instagram na mfanya biashara wa ngono mwenye umri wa miaka 21 ambaye ni mhitimu wa masuala ya Historia anayejulikana kama Tilly Lawless.
Aliamua kuzungumzia blog moja iliyoamua kurudia kuweka kwenye ukurasa wake taarifa iliyorushwa wiki iliyopita katika ukurasa wa gazeti maarufu lenye kuandika habari za akina mama liitwalo, Mamamia.Blog hiyo iliandika katika maadhimisho ya miaka ishirini na mitano mkutano wa wafanya biashara ya ngono na filamu yao ya ‘prince-charming Pretty Woman' na kudai kuwa shuhguli nzima ya biashara ya ngono haina mvuto kama ilivyo katika filamu hiyo.
Tilly Lawless alichukizwa na namna taarifa hiyo ilivyoweka mambo kirahisi rahisi na kuijumuisha biashara ya ngono na kuiona biashara hiyo kama yenye madhara .bibi huyo anashuhudia kuwa ameifanya biashara hiyo ya ngono kwa miaka miwili lakini amejulikana hadharani miezi miwili iliyopita mjini Sydney,mahali ambako biashara ya ngono ruksa kuifanya kisheria . na alichukua maamuzi ya kuweka picha yake bayana katika ukurasa wake wa Instagram kuonesha uzuri na upande wa pili wa biashara ya ngono ,sura ya mwanamke mrembo,ambaye anajitambua na aliyechagua kuwa mfanyabiashara ya ngono kwa mantiki ya kukipinga kilichoandikwa katika jarida la Mamamia na blog pia.
CHANZO BBC.

FAMILIA KUTAMBUA MIILI YAWALIOUAWA KENYA.

Wanafunzi wa chuo kikuu cha Garissa 
Familia za wanafunzi waliouawa katika chuo kikuu kazkazini mashariki mwa Kenya zimeenda katika eneo la mkasa ili kuitambua miili ya waliouawa.
Zaidi ya watu 140 waliuawa katika shambulizi lililotekelezwa na wapiganaji wa Al shabaab mjini Garissa siku ya alhamisi ambapo wapiganaji hao waliwatenganisha wanafunzi hao kwa misingi ya kidini kabla ya kuwaua wanafunzi wa kikristo.
Wakati huohuo mamlaka nchini Kenya imetoa mabasi ili kuwasafirisha wanafunzi walionusurika hadi makwao,huku miili ya waliofariki ikisafirishwa hadi mjini Nairobi.
Rais wa Somali Hassan Sheikh Mohamoud,amesema kuwa Somalia na Kenya lazima ziimarishe ushirikiano wao dhidi ya Ugaidi baada ya shambulizi hilo.
CHANZO BBC.

ZIMBABWE; ZANU-PF CHAMTIMUA BIMUJURU.

Bi Joice Mujuru
Aliyekuwa makamu wa rais nchini Zimbabwe Joice Mujuru amefukuzwa katika chama tawala ZANU-PF.
Chama hicho kinasema alipanga njama za kumuondoa mamlakani rais Robert Mugabe mbali na kukiharibia jina chama hicho- madai ambayo ameyakana hapo mbeleni .
Bi Mujuru alipigana vita vya Guerilla pamoja na Mugabe miaka ya sabini dhidi ya uongozi wa weupe na alionekana kama mrithi wake,kabla ya kukosana naye mwaka uliopita swala lililomfanya kufutwa kazi kama makamu wa rais mnamo mwezi Disemba.
Waandishi wanasema alishtumiwa sana na mke wa Mugabe, Grace ambaye anaongoza wanawake katika chama hicho.
CHANZO BBC.

MTOTO MPYA AMTESA KIM KARDASHIAN.

Kim akimpa taarifa mumewe Kanye West juu ya tatizo linalomkabili.
Mwanamama nguli na nyota wa kipindi cha runinga cha The Keeping Up with the Kardashians,Kim West ambaye ana mtoto mwenye umri wa miezi 21 North West aliyezaa na mumewe Kanye West,imeelezwa na mumewe huyo Kanye ,mkewe hataki chochote katika ulimwengu huu zaidi ya kupata mtoto mwingine ,lakini madaktari wamemuonya anaweza kukabiliwa na hatari kiafya.
Katika kipande cha kipindi kinachofuata cha kipindi cha mwanamama huyo ambacho kitarushwa katika runinga ya E’ inayojihusisha na masuala ya burudani na huenda kipande hicho kitarushwa mwishoni mwa wiki hii ,kipande hicho kinamuonesha Kim akielezea alichoambiwa na daktari wake kuwa anajaribu kumficha Kanye West anachotakiwa kwenda kufanyiwa na madaktari kuondoa kitu kilichoko kwenye kizazi chake.
Na ilipobidi kumkabili mumewe huyo, ambaye ni nguli wa muziki wa tambo,alipomwambia juu ya suala hilo tete, alikubaliana nalo na kumwambia endapo atafanikiwa kupata mtoto wa pili atakuwa wa mwisho kwasababu kondo la uzazi linakua kwenye kizazi chake.

Mke wa Kanye West
lakini baadaye mrembo huyo alionekana kukata tamaa ya kupata mtoto mwingine,na akaeleza wazi kuwa alipokuwa mjamzito wa mtoto wao wa sasa North,alikuwa akiwaambia watu wake wa karibu kwamba hakuna kiwango cha pesa duniani atakachoweza kulipwa kurejea tena katika maumivu ya uchungu wa kuzaa.
Lakini,kwasasa hakuna kitu ninachokihitaji zaidi ulimwenguni kama kuwa mjamzito tena,nina pata hasira kidogo kwamba watoto wangu wataachana miaka kadhaa.
Siku za karibuni Kim alitoa ya moyoni kwa kueleza kwamba ulikuwa ni muujiza kuipata mimba ya mtoto wake North kwasababu madaktari walisha mwambia kuwa milele hataweza kubeba ujauzito .
chanzo bbc.

WAKWE WANYWESHA MKOJO KWA MWAKA MMOJA.

Machoni anatazamika, lakini moyoni alikuwa hana raha.
Mwanamke mmoja nchini India amekuwa na mazoe na tabia kujengeka ya kukojolea vikombe vya wakweze kila iitwapo leo kwa muda wa mwaka mmoja ,zake zilitimia baada ya kufumwa na mama mkwe wake jikoni akiwa amekinga buli la chai anakojoa ndaniye.
Chanzo kisa na sababu ya kadhia hiyo kutokea ni wakweze kumpiga marufuku mtoto wao wa kiume kufanya kazi za nyumbani na ndipo mkwe huyo alipoamua kujilipiza kisasi kwa kukojolea vikombe vya wakweze kwa zaidi ya mwaka mmoja.Rekha Nagvanshi, mwenye umri wa miaka 30,alikuwa akiishi nyumba moja yeye na mumewe Deepak,mwenye miaka 34, katika wilaya ya Indore jimbo la Madhya Pradesh,pamoja na wakweze .
Mwanamke huyo alidai kwamba ingekuwa bora angeishi na nduguze kuliko kuishi kwa wakeze,na alisema kwamba hakuwa na furaha namna ndoa yake ilivyoendeshwa na alikuwa akijihisi anatendewa visivyo na hapati matunzo muafaka.Rafiki wa mwanamke huyo , Alia Kohli, mwenye umri wa miaka 32, alisema kwamba rafikiye hakuwa na furaha na ndoa yake tangu siku ya kwanza ya harusi na mumewe alikuwa akimtenda kama mtumwa na mwanamke huyo ameamua kuwa imetosha.
Lakini chakushangaza baada ya kuondoka kuelekea kwa wazazi wake , mara aliomba kurejea ukweni ati tu kwasababu ya majaaliwa ya mtoto wao wa kike aliye na umri wa miaka minne ili aendelee kumpa malezi yake,na alipo rejea kwa wakweze aliweka masharti ya mumewe kumpikia chakula,kumkandakanda miguu yake na kumfulia nguo zake zote lakini wazazi wa kijana huyo hawakuridhishwa na masharti hayo ,hivyo waliweka mpango wa kukomesha masharti hayo.

Tabasamu usoni rohoni anakereketwa
Mume wa mwanamke huyo Deepak anasema kwamba yeye alikuwa radhi na masharti ya mkewe lakini wazazi wake walimjia juu na kumsema kwamba hiyo haikubaliki kwani anamshurtisha mtoto wao kama mtumwa.
hata hivyo inaelezwa kwamba,wazazi wa mwanaume huyo walikuwa na kawaida ya kuwatembelea watoto wao mara moja kwa wiki, kitendo kilichokuwa kikimkera mno mkamwana wao na akaamua kuwatenda, wazazi walipogundua hila yake walisema kwamba walijua mkwe wao hawapendi lakini hawakufikiria kwamba anaweza kuwatenda namna hiyo,maana alikuwa akitabasamu na kuwapa chai nao waliipokea,lakini siku moja mamake Deepak niliingia ghafla jikoni na kumfuma mkwe akikojolea birika ya chai.
wazazi hao mke Suraj na mume waliamua kwenda kutoa taarifa polisi ,na huko wakatwambia masuala ya namna hiyo hawashughuliki nayo,wazazi wa mwanaume huyo wakadai sheria ichukue mkondo wake maana si jambo rahisi kwa mwaka mmoja mtu akojolee birika yenye chai na aachiliwe hivi hivi, wanataka haki itendeke.
Kufuatia kisanga hicho imejulikana familia iko mbioni kulipeleka mahakamani suala hilo na kwamba Rekha na mumewe Deepak wametengana.
CHANZO BBC.

WAANDANA DHIDI YA AL-SHABAAB GARISSA.


Maandamano Garissa 
Wananchi wa mji wa Garissa nchini Kenya wamefanya maandamano kupinga vitendo vya kundi la Al Shabaab, lililoshambulia chuo kimoja kikuu mjini humo na kuwaua watu 147 wengi wao wakiwa wanafunzi hapo jana.
Waandamanaji pia wameelezea kutoridhika na vyombo vya usalama nchini humo wakisema havikuchukua hatua za kutosha kutoa ulinzi kwa waliouawa na kwa raia wengine kwa jumla.
Wazazi, jamaa na marafiki wa wanafunzi waliouawa katika chuo kikuu cha Garissa wamekuwa wakiendelea kuwasili katika eneo hilo kuitambua miili ya wapendwa wao.
Waliojeruhiwa wanaendelea kupata matibabu .

Garissa
Serikali ya Kenya imekuwa ikiwasafirisha manusura wa shambulio hilo kwa mabasi kuelekea makwao huku miili ya waliouawa ikisafirishwa mjini Nairobi.
Wakati huo huo rais wa Somalia, Hassan Sheikh Mohamoud, amesema Somalia na Kenya zinafaa kuimarisha uhusiano wao katika mapambano dhidi ya ugaidi.
Tamko hilo linajiri siku moja baada ya shambulio hilo la Alshaabab katika chuo kimoja kikuu mjini Garrisa.
chanzo bbc.

SIMBA SC YAPATA PIGO, WANACHAMA WAKE 7 WAFA AJALINI

 
Wanachama Saba (7) wa klabu ya Simba ya Dar es salaam kutoka tawi la Mpira na Maendeleo (maarufu kama Simba UKAWA) ambalo limewahi kutangazwa kufutwa wamefariki dunia katika ajali ya basi mkoani Morogoro.
Wanachama hao wakiwa katika basi lao walikuwa wakielekea Shinyanga kwa ajili ya kuipa nguvu Simba ambayo inatarajiwa kushuka katika dimba la CCM Kambarage kuikabili Kagera Sugar katika mchezo wa ligi Kuu Tanzania Bara kesho..
Vifo hivyo vimefikia 7 baada ya watano kufa palepale na wengine wawili waliokuwa majeruhi kufariki katika hospitali ya mkoa wa Mororgoro.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro SACP Leonard Paul amethibitisha habari hizi na kusema kuwa majeruhi wamebaki 13 na kufanya vifo kufikia saba hadi majira ya saa 2 usiku wa April 03.

Alhamisi, 2 Aprili 2015

GOA HAWATAKI WAPENZI KUBUSIANA HADHARANI.

sherehe za hadhara.
Kijiji kimoja nchini India kilichoko pwani ya Goa kimeweka sheria ya kuzuia wanandoa ama wapenzi kubusiana hadharani ,kwa madai kuwa wenyeji wa maeneo hayo hawapendi tabia za kimagharibi kwenye eneo lao.
Bunge la kijiji hicho liitwalo Salvador-de-Mundo,ambalo liko kilomita nane Kaskazini ya mji wa Goa kwenye mji wa Panaji, azimio hili limepitishwa mapema wiki hii likiwaonywa wenye kufanya sherehe za hadhara wasijisahaulishe sheria hiyo na kuoneshana mahaba hadharani.
Tumeamua kulipitisha azimio hili baada ya kupokea malalmiko kutoka kwa wanakijiji juu ya watu wanaobusiana hadharani.hii ndio njia pekee ya kulimaliza suala hili anasema chifu msaidizi wa kijiji hicho Reena Fernandes .
Bibi huyo ambaye ni chifu msaidizi ameongeza kwamba malalamiko yao waliyapeleka kwa viongozi wa kijamii lakini hawakupata mrejesho wala hatua zozote kuchukuliwa na hivyo wakaamua kuchukua sheria mikononi na kupasisha azimio la marufuku ya kunywa pombe hadharani na kupiga muziki hadharani kwa sauti kubwa.
Hata hivyo ,amekataa kuzungumzia chochote juu ya hatua za adhabu zitakazo chukuliwa kwa wataovunja sheria hiyo .
Mwanakijiji mmoja Savio Rebeiro amesema kwamba tumezizuia pwani zinazovutia utalii,maana mara kwa mara huwa tunashuhudia wapenzi wawili wafanyao matendo yanayo tukera .

rahaje???????
Ukanda huo wa bahari ya hindi wenye biashara kubwa ya uvuvi kwa sasa wamesambaza mabango yenye ujumbe wa elimu juu ya katazo hilo.
Pwani za Goa zimejaa mchanga zenye mvuto wa kipekee kwa mamilioni ya watalii kutoka Magharibi na katazo hilo limetia doa utalii.
Naye waziri mkuu Narendra Modi mwenye asili ya Kihindu wa chama cha Bharatiya Janata wiki hii aliweka marufuku ya wanawake waajiriwa kuvaa suruali za jinzi na singilendi katika ofisi za serikali.
Mwaka uliopita waziri wa Goa alitaka itungwe sheria ama amri ya katazo la uvaaji bikini katika pwani zote na alipokea upinzani mkubwa kutoka kwa jamiina tasnia ya utalii.
CHANZO BBC.

KESI YA KUJIUNGA NA UGAIDI YAONGEZEKA.

Wapiganaji wa kundi la Islamic State
Zaidi ya wapiganaji wa kigeni elfu ishirini na watano kutoka mataifa mia moja walisafiri kwa nia na malengo ya kujiunga na makundi ya kijeshi kama al-Qaeda na Islamic State (IS), taarifa ya umoja wa mataifa imeeleza hayo.
Taarifa hiyo imeeleza pia kwamba wapiganaji wageni ulimwenguni idadi yao imeongezeka mpaka kufikia asilimia sabini na moja katikati ya mwaka 2014 na march mwaka huu.
Nchi za Syria na Iraq ndizo nchi zinazolengwa kwa ukaribu zaidi na ndicho kitovu cha vijana wanaomaliza mazomo yao na kugeuka kuwa wenye msimamo mkali wa kidini.
Na pia taarifa hiyo imebainisha kuwa endapo kundi la IS lingeshindwa nchini Syria na Iraq,sasa wapiganaji hao kutoka nchi za kigeni wamesambaa ulimwenguni .
Nalo baraza la usalama la umoja wa mataifa liliwaomba wataalamu wa masula ya kijeshi miezi sita iliyopita kuchunguza vitisho vya askari wa kigeni wanaojiunga na kundi la Is na makundi mengine ya kigaidi.
Katika ripoti iliyowasilishwa kwenye baraza hilo mwishoni mwa mwezi uliopita ,na wataalamu wakaeleza kuwa ongezeko la wapiganaji wa nchi za kigeni zinazidi kuongezeka kulinganisha na muongo mmoja uliopita .
Maelfu ya wapiganaji wa kigeni ambao hufanya safari hadi nchini Syria ,Falme za Kiarabu na Iraq huko hufanya makao na kufanya kazi na kumalizia masomo ya elimu ya juu kwa wenye msimamo mkali kamalivyowahi kutokea kwatika nchi ya Afghanistan miaka ya 1990 .
Syria na Iraq inasemekana ina makaazi elfu ishirini na mbili kwa wapiganaji hao wa kigeni ,pia nchini Afghanistan makaazi elfu sita na mia tano na maelfu ya makaazi nchini Yemen, Libya, Pakistan na Somalia.
CHANZO BBC.

KANISA KATOLIKI LINAUTAZAMAJE USHOGA??

Raymond Burke
Kadinali Raymond Burke mwenye asili ya Marekani ameenguliwa na Papa Francis katika wadhifa wake wa mwenyekiti wa bodi katika kanisa katoliki,ametoa onyo kwamba kuna viashiria vya kanisa hilo kuupigia chapuo ushoga, kauli hii Burke aliiotoa wakati alipokuwa akihojiwa na tovuti moja ya Italy ya La Nuova Bussola Quotidiana mara baada tu ya kuenguliwa kwenye wadhifa wake.
Mwandishi wa BBC anasema hii ni ishara nyingine ya jinsi viongozi wa dini waandamizi wanavyochukulia hatua juu ya masuala kama vile ushoga na talaka , wakati wengine wanatakiwa kuyachukulia mambo kwa utuvu na uangalifu wa hali ya juu.
chanzo bbc.

HABARI ZA MOJA KWA MOJA KUTOKA GARISSA

Idhaa yako ya kiswahili ya BBC imekuandalia ukurasa wa habari za moja kwa moja kufuatia shambulizi la chuo kikuu nchini Kenya.

14.00pm:Kwa ufupi

wanafunzi wa chuo kikuu cha Garissa
Takriban watu 15 wanaodaiwa kufinika nyuso zao wameshambulia chuo kikuu cha Garrissa Kaskazini mashariki mwa Kenya.
Watu hao wanaodaiwa kuingia katika taasisi hiyo mwendo wa saa kumi asubuhi wakati ambapo waislamu walikuwa wakifanya sala yao ya alfajiri.
Hatahivyo maafisa wa polisi wanasema kuwa shambulizi hilo lilifanyika mwendo wa saa kumi na moja unusu.


Baadhi ya wanafunzi wa chuo hicho waliosalimika
Mwandishi wa BBC mjini humo anasema kuwa walinzi wawili waliuawa katika lango la chuo hicho huku maafisa wawili wa polisi waliokuwa wakilinda chuo hicho pamoja na wanafunzi wakijeruhiwa.
Walioshuhudia wanasema kuwa kumekuwa na majeruhi mengi ndani ya chuo hicho.
Mwandishi wetu anasema kuwa wapiganaji hao bado wako ndani ya chuo hicho na wamewateka nyara watu kadhaa.

Wanafunzi waliotoroka shambulizi mjini Garissa Kenya
Jeshi la Kenya KDF ,maafisa wa polisi na amabulansi wamefika katika eneo la tukio na sasa wameingia ndani ya majengo ya chuo hicho ambapo kumekuwa na ufyatulianaji wa risasi kati ya washambuliaji na maafisa wa jeshi.


13.40pm:Waislamu na wakristo waliotekwa ndani ya Jumba hilo la Chuo kikuu cha garissa wamedaiwa kutawanywa kabla ya waislamu 15 kuwachiliwa huru kulingana na msemaji wa kundi hilo la Alshabaab.

13.35pm:Serikali ya kenya
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta anatarajiwa kulihutubia taifa kufuatia shambulizi hilo la chuo kikuu cha Garrisa mapema leo.

13.30pm:Alshabaab:

Maafisa wa Polisi wa kenya
kundi la wapiganaji wa Alshabaab limesema kuwa liko ndani ya Chuo hicho kikuu na limewatawanya waislamu na wakristo

13.20pm:Wapiganaji wamedaiwa kuwateka nyara wanafunzi na kuwaua watu 14 katika chuo hicho kulingana na wafanyikazi wa msaada na maafisa wa polisi.Takriban watu 65 wengine wamejeruhiwa baada ya washambuliaji kuvamia chuo hicho.Vituo vya habari nchini kenya hatahivyo vinaiweka idadi hiyo kuwa watu 16.

13.05pm:Idadi ya watu waliouawa kufuatia shambulizi la wapiganaji wa kundi la alshabaab imefikia 14

13.03pm:Al shabaab


Alshabaab lakiri kutekeleza shambulizi 

Kundi la wapiganaji wa Al-shabaab limekiri kutekeleza shambulizi katika chuo kikuu cha Garissa Kaskazini mashariki mwa Kenya huku likiwaua watu 14

12.47pm:Wanafunzi

 
wanafunzi wa chuo kikuu cha Garissa nchini Kenya
Chuo hicho cha Garissa kina takriban wanafunzi 1000, na wafanyikazi wengine.


12.30pm Wanafunzi:
 

 Wanafunzi waliodaiwa kutoroka
Baadhi ya wanafunzi wamedaiwa kutoroka kutoka mabweni waliokuwa wakilala


12.20pm:Wapiganaji

Wapiganaji
Wapiganaji hao wanaodaiwa kuwa watano wanaaminika kuwa ndani ya jengo hilo la Chuo kikuu .


12.18pm:Kenya Red Cross
 
Maafisa wa polisi wakikabiliana na wapiganaji huko Garissa kenya
Shirika la msalaba mwekundu nchini Kenya linasema kuwa watu 30 wamejeruhiwa huku wanne kati yao wakiwa na majeraha mabaya..Kwa sasa shirika hilo linawasafirisha madaktari katika eneo hilo.
11.30am Idadi ya watu waliouawa kufuatia shambulizi la chuo kikuu cha Garrissa Kaskazini mashariki mwa Kenya imefikia watu sita huku wengine 29 wakidaiwa kujeruhiwa.
 CHANZO BBC.

BREAKING NEWS;


Tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC) imesema kuwa kura ya maoni ya katiba inayopendekezwa, haitaweza kufanyika tena tarehe 30 April hadi hapo itakapotangazwa tarehe nyingine tena.
NEC imesema sababu ya kuhairisha kura hiyo April 30 ni kutokana na kutokamilika kwa zoezi la uboreshaji daftari la kudumu la wapiga kura.

WABUNGE WA UPINZANI WAJA NA MBINU MPYA BUNGENI.

 
Unakumbuka zamani Wabunge wa upinzani walikuwa wakiona hawatendewi haki na Spika wanasusa na kuondoka Bungeni, kwahiyo mambo mengi yanajadiliwa bila wao kuwepo. Ila kwa sasa wanambinu tofauti ambayo wakiona hawatendewi haki wanasimama juu na kuanza kugonga gonga meza na kupiga kelele hadi Bunge linaharishwa

MSALA ULIOMPATA MCHUNGAJI GWAJIMA,MUME WA FLORA MBASHA AVUNJA UKIMYA.


Msala uliompata Mchungaji Gwajima wa kumtolea maneno yenye kuudhi Askofu wa Kanisa Katoliki Mwadhama Polycap Kadinali Pendo na kisha kuhojiwa polisi na kupata mshtuko, kuzimia hadi kulazwa, Mume wa Flora Mbasha, anasema hayo ni malipo ya Mungu kwake kutokana na kilio chake baada ya Mchungaji huyo kusambaratisha ndoa yake .
“Ile hali ya Gwajima ni malipo. Mimi nilishasema jamani, mtu akikutendea ubaya malipo ni hapahapa duniani, hakuna kwingine. Mimi ndoa yangu haipo, mke wangu anajua yeye anavyoishi. Kwa hivyo mimi nimekuwa nikiishi kwa manung’uniko kila siku, unadhani nini kitatokea kwake?” amefunguka Emmanuel Mbasha

MELI YA UVUVI YA URUSI YAZAMA.

Meli ya uvuvi ya Urusi iliyozama kwa dakika kumi na tano tu
Boti ya uvuvi ya Urusi imezama katika visiwa vya Kamchatka , ikiwa na mabaharia wapatao hamsini na wanne ambao inadhaniwa kuwa wamekufa maji wote.
Watu wapatao sitini na watatu wameopolewa ambao nao walikuwa ndani ya boti hiyo ya uvuvi,wengine wamekumbwa na homa ya mapafu na wengine kumi na watano wameripotiwa kuwa hawaonekani.
Taarifa za awali zinasema kwamba kabla meli hiyo ya uvuvi haijazama ilikuwa na watu wapatao miamoja na thelathini na mbili ,uchambuzi unaeleza kuwa sabini na nane kati yao ni raia wa Urusi na arobaini na wawili ni raia wa Myanmar. Wengi wao walikuwa wanatokea maeneo ya Vanuatu, Latvia na Ukraine na nahodha ni miongoni mwa waliopoteza maisha.
Kikosi cha uopoaji kinaendelea na kazi ya oukozi ambapo mpaka sasa wanatafuta abiria hao waliopotea wapatao kumi na watano .
Nahodha wa kikosi cha uongozi ambaye ni miongoni mwa mabaharia wa kikosi cha uopoaji ishirini na sita anasema kwamba pengine chanzo cha ajali hiyo ni hali mbaya ya hewa, na wakati meli hiyo ilipokuwa ikizama ,kulikuwa na barafu,upepo mkali, mawimbi yenye urefu wa futi kumi. Na maji ya bahari yalikuwa karibu yanaganda kwa nyuzi joto 32 .
Inaelezwa kwamba manusura wa ajali hiyo walikuwa wanauwezo wa kudumu katika maji hayo kwa dakika ishirini tu,ingawa mpaka sasa chanzo cha ajali hiyo ni cha kukisia tu.
Maji yalifurika kwenye chumba cha ingini ya meli hiyo na kuanza kuzama ndani ya dakika kumi na tano kimesema kitengo cha dharula cha Urusi,na kusema kwamba pengine meli hiyo iligonga eneo la karibu na chumba cha ingini na kuwa sababu ya ajali hiyo.
Sergei Khabarov amesmea kwamba kiwango cha abiria na mizingo katika meli za wavuvi lazima kizingatiwe na kisizidi uwezo wa vyombo hivyo.
chanzo bbc.

HABARI ZA HIVI PUNDE;-WATU 2 WAUAWA KUFUATIA SHAMBULIZI KENYA

Garissa Kenya 
Wapiganaji waliofunika nyuso zao wameshambulia eneo la chuo kikuu cha Garissa kaskazini mwa Kenya karibu na mpaka wa taifa hilo na Somalia.Milio mikali ya risasi pamoja na milipuko imesikika katika chuo kikuu cha Garissa mjini humo.
Maafisa wa usalama wa Kenya wamethibitisha kuwa watu wawili wamefariki huku wanne wakijeruhiwa.
Wakaazi wa eneo hilo wametakiwa kukaa mbali na eneo la chuo hicho.
Haijulikani ni nani aliyekusika na shambulizi hilo ,lakini kundi la wapiganaji wa Somalia Al shabaab limetekeleza misururu ya mashambulizi mjini Garissa pamoja na maeneo mengine ya Kenya tangu mwaka 2011 wakati wanajeshi wa kenya walipopelekwa Somalia.
CHANZO BBC.

Jumatano, 1 Aprili 2015

CHEZEA MAHABA WEWE,,,,,KWA HALI HII MWENYEWE UNAKABIDHI KADI YA BANK NA NO YA SIRI.




BINTI AIBA KITENGE CHA MGONJWA,ACHEZEA KICHAPO KUTOKA KWA WAGONJWA.


Binti aliyejulikana kwa jina la Mariam Moshi (23), mkazi wa Mwananyamala Ujiji, aliponea chupuchupu kuuawa na wagonjwa wenye hasira kali waliolazwa katika hospitali ya Mwananyamala baada ya kudaiwa kuiba nguo za wagonjwa. Mariam anadaiwa kuiba Kitenge kipya na taulo. Mwenyewe alipoulizwa alisema Kitenge tu ndio amekiiba hospitalini hapo ila taulo alilokuwa amejifunga ndani ya dera alilovaa, alisema aliliiba katika gesti aliyokuwa amelala siku hiyo.. Aliomba msamaha kwa kitendo alichokifanya, akisema kinatokana na maisha magumu

TAARIFA KUHUSU ASKARI KUUAWA.


Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na Polisi Mkoa wa Pwani linaendesha oparesheni kali ya aina yake ya kuwasaka watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi waliowavamia, kuwauwa askari wawili na kumjeruhi mmoja na kisha kupora bunduki aina ya SMG.
Tukio hilo limetokea tarehe 30/03/2015 majira ya saa mbili usiku huko barabara ya Kilwa Kata ya Vikindu Wilaya ya Mkuranga Mkoa wa Pwani. Katika tukio hilo majambazi wapatao 8 hadi 10 wakiwa na mapanga na silaha zingine waliwavamia ghafla askari watatu waliokuwa kazini katika eneo la kizuizi cha Polisi kilichopo kijiji cha Kipara mpakani Kata ya Vikindu Wilaya ya Mkuranga Mkoa wa Pwani. Majambazi hao wakiwashambulia ghafla askari hao kisha kupora silaha aina ya SMG ikiwa na risasi 30 ndani ya magazine na kutokomea kusikojulikana.
Majina ya askari wa Wilala ya Kipolisi ya Mbagala waliouawa ni kama ifuatavyo:
D.2865 SGT FRANCIS,
E.177 CPL MICHAEL,

CHANZO 5EATV.

NEC ITATOA RATIBA KAMILI KUHUSU BVR NA KURA YA MAONI – PINDA


Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema kuwa serikali imeiagiza Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutoa ratiba kamili kuhusu zoezi la uandikishwaji Wapiga Kura kwa BVR pamoja na hatma ya Kura ya Maoni ya Katiba Mpya.
Pinda ameyasema hayo wakati akiahirisha Bunge majira ya saa 6 usiku wa kuamkia Alhamis tarehe 02 April, 2015 ambapo amedai kuwa tayari serikali imekwisha lipia pesa zote kwa ajili ya mashine zote za kuandikishia (BVR).
“Serikali imekwishatoa pesa kwa ajili ya mashine zote za BVR kilichobaki ni kwa Tume kupanga ratiba yao, tuna imani kuwa mashine zote zikifanya kazi zoezi la uandikishwaji wapiga kura litamalizika kwa wakati” Amesema Pinda
Amesema ameongea na Mwenyekiti wa tume hiyo leo (April 01) na imemuhakikishia kuwa itatangaza ratiba nzima kabla ya Pasaka.
Kuhusu ugawaji wa Katiba Pendekezwa amesema kuwa tayari nakala 1,141,300 kwa upande wa Tanzania Bara na nakala 210,000 kwa upande wa Zanzibar zimekwisha sambazwa.
Kuhusu muswada wa mahakama ya Kadhi, Pinda amesema serikali imefurahishwa na uamuzi wa muswada huo kuondolewa kwa kuwa itapata muda wa kutosha kujadiliana na wadau na kutoa elimu zaidi kuhusu umuhimu wa Mahakama hiyo.
Bunge limeahirishwa hadi tarehe 12 Mei, 2015 kwa ajili ya mkutano wa 20 likiwa limejadili na kupitisha miswada 14 kati ya 21 iliyokuwa imepangwa katika mkutano huu uliomalizika leo.
Kabla ya kuahirishwa, bunge limefanya maamuzi ya kupitisha muswada wa uhalifu wa kimitandao huku likiwa na wabunge wasiofikia nusu ya wabunge wote kama inavyotakiwa kwa mujibu wa kanuni.

YOUSSOU NDOUR NDIYE MWANAMUZIKI TAJIRI

Youssou Ndour ndiye mwanamuziki tajiri barani Afrika
Usanii wa muziki ni miongoni mwa kazi zinazolipa vizuri duniani.
Hatahivyo si kila mtu anayefanikiwa katika sekta ya muziki.
Kulingana na mtandao wa capital Fm nchini Kenya,kwa wewe kufanikiwa ni sharti uipende sekta hii pamoja na uwajue wateja wako.
Hivyo ndivyo wasanii wengi wa muziki wameweza kujitengezea jina duniani.
Na je, unawajua wanamuziki tajiri barani Afrika?Orodha ya wanamuziki 10 walio matajiri barani afrika kulingana na Answers Afrika itakushangaza.
Hii Hapa.
01.Youssou N'Dour - Senegal.
02.P-Square- Nigeria
03.D'banj - Nigerian
04.Koffi Olomide - DRC
05.Salif Keita - Mali
06.Fally Ipupa DRC
07.Face Idibia - Nigeria
08.Hugh Masekela - South Africa
09.Banky W - Nigeria
10.Jose Chameleon - Uganda

MTU MWENYE UMRI MKUBWA DUNIANI AFARIKI.

Okawa
Mtu aliyekuwa na umri mkubwa duniani kutoka nchini Japan amefariki wiki kadhaa baada ya kusherehekea miaka 117 tangu azaliwe.
Misao Okawa alifariki katika kituo cha uangalizi mjini Osaka,mji ambao alizaliwa mwaka wa 1898.
Okawa amewaacha vitukuu sita na wajukuu wanne .
Kufuatia kifo chake kuna madai kwamba kumesalia watu wanne pekee wanaodaiwa kuwa hai ambao walizaliwa karne ya kumi na tisa.
Wote ni Wanaume huku mwanamume wa mwisho akifariki mwaka 2013.
CHANZO BBC.

RAIA WA YEMEN WAKIMBILIA SOMALIA.


Raia wa Yemen wakikatika Ghuba ya Aden kwa boti ndogo
Mashirika ya umoja wa mataifa yamesema kuwa mamia ya raia wa Yemen wamevuka ghuba ya Aden kwa kutumia boti ndogo na kuingia nchini Somalia, Djibouti na Somaliland wakikimbia mapigano nchini mwao. Shirika la umoja wa mataifa la UNHCR limesema kuwa linaangalia eneo zuri kwaajili ya kuweka kambi ya wakimbizi kwaajili ya raia hao. Wakati huo huo wakimbizi kutoka nchini Somalia bado wanaendelea kuingia nchini Yemen kuepuka njaa na machafuko nchini mwao. Shirika hilo la UNHCR linasema kuwa Yemen inawahifadhi wakimbizi wapatao 238,000 kutoka Somalia. Mwandishi wa BBC Africa Mary Harper anasema wazo la Yemen kufikiria kuwa na kambi za wakimbizi nchini Somalia si la kawaida kwa kuwa ni kawaida kwa raia nchini humo kuikimbia nchi yao kutokana na machafuko ya mara kwa mara hali ambayo haiwezi kuwa eneo zuri kwa wakimbizi kuhifadhiwa.
chanzo bbc.

MAMA AWAFUNGIA NDANI WANAYE 3 KWA MIAKA 10!


Katika Kisiwa cha Mafia mkoa wa Pwani mama aitwaye Mwasiti Ally amekuwa akiwafungia ndani watoto wake ndani kwa muda wa miaka 10 sasa kwa madai kuwa ni wagonjwa wa akili. Watoto hao huko ndani ya chumba wote wamebadilika na kuwa na afya mbaya huku kucha za mikononi na miguuni kurefuka sana, nywele zimekua ndefu kiasi cha kutisha na sura zao kuonekana kama za misukule na kuwa kama walemavu wa miguu. Alianza kuugua mtoto mmoja ambaye ni wa kwanza kuzaliwa, cha ajabu, kila mwaka mwingine akafuatia hadi wa tatu. Mama huyo anadai Sababu kubwa ya kuwafungia ndani tangu mwaka 2005 anasema ni kwaajili ya usalama wao maana anaamini kwa kuwaachia tu wangeweza hata kupotea.

BUHARI AAPA KULITOKOMEZA BOKO HARAM

Goodluck Jonathan na Muhammadu Buhari
Mshindi wa uchaguzi wa urais nchini Nigeria Muhammadu Buhari ameelezea mashambulizi yanayotekelezwa na kundi la wapiganaji wa Boko Haram kama tatizo kuu linalokabili taifa hilo.
Katika hotuba aliyotoa katika runinga za Nigeria,kiongozi huyo wa kijeshi zamani amesema kuwa serikali yake itafanya kila juhudi kuangamiza ugaidi.
Vilevile amesema kuwa atakabiliana na jinamizi la ufisadi.
Bwana Buhari ambaye anachukua wadhfa wa urais kuanzia mwezi ujao,alimsifu mpinzani wake na rais anayeondoka Goodluck Jonathan.
Alimtaja kuwa kiongozi anayehitaji heshima.
CHANZO BBC.