Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumamosi, 20 Desemba 2014

UCHAGUZI WA MASINETA WAFANYIKA LIBERIA


Uchaguzi wa msineta umeanza hii leo licha ya kuwa huenda ukasababisha kuenea kwa ugonjwa wa Ebola

Shughuli za upigaji kura zinaendelea nchini Liberia kuwachagua maseneta wapya licha ya kuwepo kwa hofu kwamba kura hiyo huenda ikachangia kusambaa kwa ugonjwa wa ebola.
Uchaguzi huo umehairishwa mara kadha lakini rais Ellen Johnson - Sirleaf anasema kuwa kura hiyo ni lazima ifanyike wakati huu ili kuzuia msukosuko .
Mikutano ya kisiasa ilipigwa marufuku kufuatia hatari iliyotokana na ugonjwa wa ebola ambao umewaua maelfu ya watu magharibi mwa afrika.
Mwandishi wa BBC anasema kuwa watu wengi nchini Liberia wanaamini kuwa kura hiyo ni hatari sana na kesi ya kuizuia isifanyike imepelekwa kwenye mahakama ya juu.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni