Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatatu, 29 Desemba 2014

TIMU NANE ZA TENNIS KUCHUANA TANZANIA


Binti akirudisha majibu mchezoni
Timu kutoka nchi za Burundi, Ethiopia, Kenya, Rwanda, Shelisheli, Sudan, visiwa vya Comoro zitashindana nchini Tanzania hapo mwakani katika michuano ya tennis ya Afrika kwa watoto chini ya miaka 12, 14 na 16.
Shirikisho la tennis Tanzania (TTA) limesema lipo tayari kwa uwenyeji katika michuano hiyo itakayochezwa kuanzania January 11-19 katika viwanja vya Gymkhana Dar es Salaam.
Kocha Majuto Majaliwa, anayetambulika na shirikisho la tennis duniani (ITF) amesema wachezaji wa Tanzania wataanza mazoezi Jumamosi ili kujiweka tayari.
“Tumechagua timu yenye wachezaji wazuri ambao wataweza kuipeperusha bendera ya Tanzania nyumbani”.
‘Kuwa wenyeji ni furaha kwetu kwa sababu wachezaji watakuwa wakicheza nyumbani katika viwanja walivyovizoea”, alisema Majaliwa.
Hii ni mara ya pili kwa Tanzania kuandaa michuano hiyo mikubwa barani Afrika.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni