Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumapili, 28 Desemba 2014

ALIPANDA KRENI KUMPOSA MPENZI.YALIYOMKUTA NI HAYA


'Kreni' ilitumbukia ndani ya nyumba wakati ikimbeba mwanamume aliyekuwa anamposa mpenzi wake
Mwanamume mmoja raia wa udachi amejikuta akikimbilia usalama wake baada ya jaribio la kutaka kumposa mpenzi wake kwa mbwembwe kwenda mrama.
Mtu huyo ambaye hakutajwa kwa jina anayeishi mjini Ijsselstein alikodisha 'kreni' au Crane na kuipanda akipanga kwamba kreni hilo imtoe chini na kumpanidhs hadi dirishani mwa mpenzi wake ambapo angemchezea wimbo na kisha kumposa.
Badala yake yaliyomkuta hakuyatarajia kabisa.Kreni hiyo ilianguka chini na kupita dirishani kwa mpenzi wake huku ikiangukia nyumba za majirani.
Mwanamume huyo alilazimika kukimbilia usalama wake na hakuna aliyejeruhiwa katika tukio hilo lililowaacha wengi wakiangua kicheko.
Kwa mujibu wa jarida la Algemeen Dagblad, mpenzi wake mwanamume huyo alimkubali na kusema yuko radhi kuolewa naye licha ya tukio hilo.
Baada ya kuongea na polisi, wawili hao walisafiri kwenda mjini Paris Ufaransa kusherehekea.
Kreni hio ilianguka tena kwa mara ya pili ilipokuwa inainuliwa na hata kuharibu zaidi nyumba za majirani. Meya wa mji huo, amezomewa na wengi baada ya eneo hilo kusemekana kutokuwa salama.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni