Eneo la tukio St Louis
maandamano makubwa yametokea nchini
Marekani katika mji wa St Louis yaliyosababishwa na askari kumpiga
risasi kijana mweusi akiwa katika kituo cha mafuta .Polisi wanamtetea
afisa mwenzao ya kwamba alitenda kitendo hicho kama njia ya kujihami
,baada ya marehemu kumnyoonyeshea bunduki katika kitongoji cha Berkeley.Waandamanaji
waliyaanza maandamano hayo mara tu baada ya taarifa za mauaji hayo
kusambaa,kutokana na hasira waliyonayo waandamanaji hao picha za video
zinawaonesha baadhi yao wakivuka mpaka waliowekewa na polisi .kitongoji cha Berkeley kiko umbali wa kilomita tatu kutoka mjini Ferguson, Missouri, mahali ambako yalifanyika mauaji ya kijana mwingine mweusi aliyekuwa na umri wa miaka kumi na nane Michael Brown , aliyepigwa risasi na askari wa kizungu,mauaji yaliyoibua hisia za ubaguzi wa rangi ,mauaji ambayo yalitokea mwezi August mwaka huu .hata hivyo Brown hakuwa na silaha yoyote wakati akiauwa.
CHANZO BBC
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni