Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumanne, 23 Desemba 2014

EBOLA BADO TISHIO


Peter Piot
Shirika la Afya Duniani limesema ugonjwa wa Ebola hautaweza kudhibitiwa kikamilifu katika kipindi cha mwaka mmoja unaokuja.
Mwenyekiti kutoka kitengo maalumu kinachoshughulikia ugonjwa huo, kutoka katika Shirika la Afya Duniani Profesa Peter Piot anasema hali halisi kwa sasa ya ugonjwa huo ni kama ugonjwa utakaodumu muda mrefu.
Profesa Peter Piot ambaye amerejea kutoka nchini Sierra Leone, nchi ambayo imeathiriwa zaidi na ugonjwa huo, ameiambia BBC kwamba amehamasishwa na ahadi za kupatikana kwa kinga mpya ambayo inaaminika itakuwa tayari katika kipindi cha miezi mitatu.
Hata hivyo Profesa Piot ambaye aligundua virusi vya ugonjwa wa Ebola mwaka 1976, ameonya pia kwamba janga lililopo sasa halitakuwa la mwishon na chanjo kudhibiti kirusi hicho itachukua muda kufanya kazi
chanzo bbc

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni