Rais Obama wa marekani ametaka filamu ya ucheshi ya rais wa Korea kazkazini kuonyeshwa
Rais wa marekani Barack Obama
ameimbia Korea Kaskazini kuwa Marekani itajibu kisa ambapo wizi wa
mtandao ulioendeshwa dhidi kampuni ya filamu ya Sony Pictures hali
iliyosababisha kufutiliwa mbali kwa maonyesho ya filamu inayomdhihaki
kiongozi wa korea kaskazini kim jong- un.
Lakini mwandishi wa BBC anasema kuwa hatua hiyo haitakuwa rahisi kwa Marekani kutokana na kujitenga kwa Korea kaskazini.Rais Obama amesema kuwa kampnui ya filamu ya Sony Pictures ilifanya makosa kwa kusitisha kuonyesha filamu hiyo.
Hata hivyo Sony ilisema kuwa ilichukua uamuzi huo kwa kuwa kumbi nyingi kubwa za sinema nchini Marekani zilikataa kuonyesha filamu hiyo.
Sony imesema kuwa ina mipango wa kuionyesha filamu hiyo na kwa sasa inatafuta njia zingine za kuionyesha.
CHANZO BBC.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni