Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatatu, 29 Desemba 2014

MOURIHO ALAUMU VYOMBO VYA HABARI NA WAAMUZI


Jose Mourinho 
Meneja wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho anaamini kuwa kuna kampeni zinaendelea kuwashawishi waamuzi kutoa mamuzi tofauti dhidi ya timu yake.
Mourinho amekasirishwa na mwamuzi Anthony Taylor kwa kushindwa kutoa penati katika mchezo dhidi ya Southampton ulomalizika kwa sare ya bao 1-1.
Kiungo Cesc Fabregas alipewa kadi ya njano baada ya kuanguka katika eneo la hatari la Southampton, kwa kukwatuliwa na Matt Target na kuoneka na kama amemuhadaa mwamuzi kwa kujiangusha.
Baada ya mchezo huo Mourinho alilamika kuwa vyombo vya habari, watangazaji mameneja wa timu zingine wote wanatoa shinikizo kwa waamuzi hivyo anadhani kuna kampeni inaoendelea dhidi ya timu yake.
"Sijui kwa nini kuna kampeni inaendelea dhidi ya timu yangu ila sijali,kila mtu anajua ile ilikua ni penati."
Mourinho anafahamika Zaidi kwa kwa kauli zake tata ambazo amekua akizitoa mbele ya waandishi wa habari.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni