Waendesha mashtaka wamesema, shambulizi hilo linafanana na lile lililotokea katika mji wa Dijon siku ya Jumapili ambapo dereva wa gari aliyekuwa akisema kwa sauti maneno ya kiislamu mfululizo alipowagonga wapita kwa miguu katikati mwa mji.
Na siku ya Jumamosi, mtu mmoja alipigwa risasi na kufariki baada ya kumchoma kisu afisa wa polisi karibu na mji wa Tours.
Hata hivyo, wachunguzi wamesema matukio hayo hayana uhusiano na waislamu wenye msimamo mkali, lakini mwandishi wa BBC amesema hofu imetanda nchini Ufaransa kuhusiana na idadi ya watu wanaojiunga na makundi ya kiislamu yenye msimamo mkali.
Kwa upande wake, waziri wa mambo ya ndani wa Ufaransa Bernard Cazeneuve, amesema tishio lipo nchini humo na kuwahakikishia wafaransa kwamba kila kitu kinafanywa ili kuhakikisha usalama wa raia wake.
CHANZO BBC
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni