Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatatu, 29 Desemba 2014

MAREKANI YATUMA MELI YA KIVITA INDONESIA


Manowari ya Marekani
Wanamaji kutoka Marekani wamesema kuwa wanapeleka moja ya Manowari ya kivita kutafuta ndege ya AirAsia iliyopotea tangu jumapili katika Bahari za Indonesi.
Manowari hiyo ijulikanayo kwa jina la USS Sampson inatarajiwa kufika leo katika eneo la Java Sea today ikiwa ni siku ya tatu tangua kuanza msako dhidi ya ndege hiyo. Idadi ya wataalamu wa kimataifa wanaoitafuta ndege hiyo imeongezeka ambapo kwa sasa nchi za Singapore, Malaysia ,Australia,Korea Kusini,Thailand na China wanashiriki katika kazi hiyo. Mkuu wa Operesheni ya uokoaji na utafutaji ndege hiyo Henry Bambang Soelistyo amesema kwa sasa kuna jumla ya Meli 30,ndege 15 na Helkopita katika eneo la tukio. Ndege hiyo ilipotea ilipokuwa ikisafiri kutoka Surabaya Indonesia kuelekea Singapore ikiwa na abiria 162.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni