Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumanne, 30 Desemba 2014

NDEGE ILIYOPOTEA;UTAFUTAJI WACHELEWA.


Ndugu wa abaria waliopotea kwenye ndege ya AirAsia wakilia kwa uchungu
Hali mbaya ya hewa imechelewesha zoezi la anga na majini la utafutaji wa ndege ya AirAsia aliyoanguka ikiwa na watu 162 baada ya kuwepo kwa dhoruba katika pwani ya eneo la Borneo siku ya jumapili.
Kufuatia kupatikana kwa vipande vya mabaki ya ndege hiyo siku ya jumannne, kiongozi wa taasisi ya uokoaji na utafutaji amesema miili mitatu imepatikana hadi sasa kutoka katika eneo la bahari ya Java.
Wapiga mbizi wa kikosi cha maji cha jeshi wanatarajiwa kuanza kutafuta miili na kinasa sauti cha ndege hiyo katika kina cha chini cha maji katika eneo linalosadikiwa ndipo ndege hiyo ilipoangukia.
Ndege hiyo ilipotea ikiwa safarini ikitokea mji wa Surabaya nchini Indonesia kuelekea nchini Singapore.
chanzo bbc.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni