Alexei Navalny.
Wakuu wa mahakama Nchini Urusi wanatoa hukumu katika kesi dhidi ya kiongozi mmoja wa upinzani, Alexei Navalny.
Kesi
hiyo iliyokuwa isikizwe na kuamuliwa tarehe 15 Januari, sasa itasikizwa
leo. Wakili wa Navalny anasema kuwa hatua hiyo imepangwa ili kuwahadaa
tu maelfu ya wafuasi wake, waliokuwa wakiandaa mkutano mkubwa jijini
Moscow tarehe 15.Hata hivyo saa chache baada ya tangazo hilo maelfu ya watu waliingia ktika mtandao wa Facebook na kupanga kuwa na mkutano mkubwa siku ya Jumanne.
CHANZO BBC
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni