Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumanne, 23 Desemba 2014

SONY YAMFURAISHA RAIS OBAMA


Kampuni ya Sony
Rais wa Marekani amelipokea kwa furaha tangazo la kampuni ya Sony kuamua kuonyesha filamu ya kuchekesha yenye utata 'The Interview
Filamu hiyo itaoneshwa katika baadhi tu ya kumbi za sinema nchini Marekani mnamo siku ya Krismas.
Rais Obama awali aliikosoa kampuni hiyo kwa kusitisha mpango wake wa uzinduzi wa filamu hiyo inayohusu kuuawa kwa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un, baada ya shambulizi la mtandao dhidi ya kampuni ya Sony linaloaminika kufanywa na Korea Kaskazini.
Baadhi ya watu waliokuwa wakisubiri kununua tiketi katika jimbo la Virginia wameelezea kwa nini wanataka kuiona sinema hiyo;
Nadhani ina hamasa fulani, na nadhani itafurahisha kuona nini kitatokea baadae, kisiasa na katika ulimwengu wa sasa ambapo jamii na kila mmoja anaishi. Nitapenda kuitizama hiyo sinema. Nadhani itakuwa ni vizuri sana kuangalia sinema inayochekesha lakini pia ina ukweli ndani yake. anasema Spencer James.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni