Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumapili, 30 Novemba 2014

CHEZEA MTOTO WA TANDALE NA HIZI NDO FURAHA ZA KUTWAA TUZO.


MAKINDA;HAKUTOKUWA NA HURUMA WALA KINGA YA UBUNGE,MTAWEKWA NDANI NA UBUNGE WENU UTAKWISHA.


Makinda: Watu wenye mapesa yao wanaokuja kuwarubuni humu ndani kataeni mkiendekeza mchezo huu mtajikuta mko ndani wote
Makinda: Hakuta kuwa na huruma wala kinga ya Bunge, mtawekwa ndani na ubunge wenu utakwisha, kuweni makini na hawa matajiri
Makinda: Bunge limeahirishwa hadi Tarehe 27, January 2015.. Wabunge wanatawanyika wakiwa wamoja

FURAHIA JUMAPILI YAKO KWA KUTIZAMA PICHA KALI ZA KUCHEKESHA.

Jumamosi, 29 Novemba 2014

MTOTO WA TANDALE AFANYA KWELI.ATWAA TUZO 3.KWA MPIGA.

BINTI WA KAZI ALIEMPIGA MTOTO,AVUNJA UKIMYA




Baada ya story ya yule msichana kwa anayefanya kazi za ndani Uganda kuchukua headlines katika vyombo mbalimbali vya Kimataifa Duniani, leo kipo ambacho amekizungumza kwa mara ya kwanza tangu afanye kosa hilo.
Msichana huyo Jolly Tumuhiirwe ambaye kwa sasa amekamatwa na Polisi amesema sababu iliyomfanya amtese mtoto Arnella Kamanzi, ni kutokana na kuchanganyikiwa baada ya waajiri wake kutompatia pesa ili amtumie baba yake ambaye alikuwa anaumwa.
Amesema anajiona mwenye hatia kwa alichokifanya japo anadhani alifanya hivyo kama njia ya kumkanya mtoto huyo kwa kuwa alikuwa akimuona mama wa mtoto huyo akimpiga kama njia ya kumkanya.
Jolly amelalamika kuwa anajisikia vibaya pale ambapo wafungwa wenzake wamekuwa wakimtenga sana na kutaka kumpiga.

WASIRA AAMUA KUSEMA.


Wasira: CAG sio mara ya kwanza kuchunguza na kuleta taarifa bungeni, na PAC nao hii ni kazi yao kuchunguza na kuleta Bungeni
Wasira: Jambo la pili ni wajibu sasa wa Bunge hili kutazama ripoti hizi na kuzifanyia kazi.
Wasira: Kama kuna mtu anataka kuwa Rais na mbinu zake ni kuondoa wengine huyo hafai kabisa kuwa Rais wa Tanzania
Wasira: Sisi bunge hili lazima tunangalie maslahi ya Watanzania, hatuwezi kutumiwa na mtu.
Wasira: Afadhali kuwa maskini mwenye heshima kuliko tajiri anayetukanwa
Wasira: Tutakuwa Bunge la ajabu kama maneno haya yameandikwa na vyombo hivi vya Bunge halafu sisi tukalifumbia macho.
Wasira: Nchi ambayo unaenda na sandarusi, mabox kubeba hela, hapa hatuna nchi, inabidi TAKUKURU watutajie ni kina nani hawa
Wasira: TAKUKURU iwachambue watu wote bila kujali vyama au nini ili tuwapeleke kwenye sheria
Mwandosya: Suala hili linatuondolea sifa kama nchi, linatuondolea heshima kama taifa, kimataifa na mbele za wananchi

HAYA NDIO MAAZIMIO YA KAMATI YA MARIDHIANO


1- Andrew Chenge, mwambalaswa na William ngereja
waondolewa uenyekiti wa kamati zao
2- prof.Muhongo,AG werema, katibu mkuu maswi, prof.Tibaijuka, waondoke
3-Bodi ya tanesco ivunjwa
4- serikali iwasilishe bungeni mapitio yote ya mikataba ya umeme
5-majaji waliohusika kwenye ufisadi wasimamishwe kupisha uchunguzi
6- stanbic bank na mkombozi au benki nyingine yoyote zitangazwe
kuwa institute of money laundering (taasisi ya kutakatisha fedha haramu)
7-kuitaifisha mitambo ya iPTL kwa Tanesco
8- TAKUKURU na Polisi wamchukuliehatua bwana Sethi, na kumfungulia
mashitaka

ZITTO ASEMA AMEWAMISS SANA UKAWA.


Zitto: Nimekuwa na mgogoro na chama changu lakini kwenye hili wameniunga mkono, kwa mara ya kwanza nimehudhuria kikao cha UKAWA
zittokabwe : Wabunge wa Chama changu wamekuwa na mimi na kwa mara ya kwanza nimeudhuria kikao cha UKAWA, nawashukuru sana
zittokabwe Kwa mara ya kwanza nilihudhuria kikao cha UKAWA hapo jana, niliwamiss sana na ninashukuru kuniunga mkono

WALIOKUFA KWA EBOLA WAFIKIA 7,000 SASA.

 Guinea

Takwimu mpya zilizotolewa na Shirika la Afya Duniani, WHO, zinaonesha kuwa watu karibu 7,000 wamefariki hadi sasa kutokana na Ebola, karibu wote Afrika Magharibi.
Hao ni watu zaidi ya elfu moja kuliko idadi iliyotangazwa na WHO Jumatano tu.
Vifo vingi zaidi vimesajiliwa Liberia.
WHO inasema watu zaidi ya 16,000 wameugua Ebola hadi sasa.
Waandishi wa habari wanasema kuongezeka kwa idadi ya waliokufa siyo lazima inamaanisha ugonjwa unazidi kutapakaa kwa kasi kwa sababu takwimu nyengine ni za zamani.
Na Rais Francois Hollande wa Ufaransa amezuru Guinea, kiongozi wa kwanza asiyekuwa Muafrika kuzuru moja kati ya nchi tatu za Afrika Magharibi zilizoathirika sana na Ebola.
Bwana Hollande alisema alitaka kuleta ujumbe wa matumaini kwa watu wa Guinea:
"Ufaransa inaweka mfano - tumefanya hivyo kifedha kwa kutoa dola 125 milioni.
Lakini mbali ya msaada wa mali, utu ndio muhimu zaidi.
Na Guinea inapochukua hatua za kuuguza na kuzuwia Ebola isisambae, hivyo inasaidia ulimwengu, Ulaya pamoja na Ufaransa zisije nazo zikapata virusi hivyo vibaya.
Kwa hivyo tuko nanyi katika mapambano haya, vita hivi.
Na ni muhimu kuwa miaka 15 baada ya rais wa mwisho wa Ufaransa kuzuru Guinea, kuwa nami niko hapa kuonesha urafiki, umoja na matumaini."
Rais Alpha Conde wa Guinea alisema Rais Hollande amefika wakati mzuri ili kuonesha kuwa mtu yoyote anaweza kuzuru Guinea.
CHANZO BBC.

NA HIVI NDIVYO WABUNGE WALIVYOKUBALIANA KUHUSU SAKATA LA FEDHA ZA AKAUNTI YA ESCROW


zittokabwe
Mwenyekiti wa PAC Zitto Kabwe amesoma maazimio mapya ya Bunge kwa mujibu wa kamati maalumu iliyoundwa leo na kuhusisha CCM, PAC na UKAWA
Azimio: Mamlaka ya uteuzi iwawajibishe na inashauriwa kutengua uteuzi wa Waziri wa Nyumba, ardhi na makazi Prof Tibaijuka, Waziri wa Nishati na Madini Prof Muhongo, Mwanasheria Mkuu wa serikali Jaji Werema, na Katibu Mkuu wa wizara ya Nishati na Madini Maswi
Azimio: Bunge liwawajibishe wabunge ambao ni sehemu ya bodi ya TANESCO na viongozi wa Kamati za Bunge
Azimio: Mamlaka husika ziitangaze Benki ya Stanbic, Mkombozi na benki yoyote nyingine itakayogundulika kuwa zinahusika na utakatishaji wa fedha haramu
Azimio: Kwa kuwa majaji walihusika, Rais aunde Tume ya kijaji ya uchunguzi na kuwasimamisha jaji Mujulusi na Prof Luhangisa
Azimio : Serikali ipitie upya mikataba ya Umeme na itoe taarifa kabla ya kumalizika kwa mkutano ujao wa bunge la Bajeti
Azimio : Serikali ichukue mitambo ya IPTL na iikabidhishe kwa TANESCO
Azimio: TAKUKURU na Polisi wamchukulie hatua bwana Sethi, na kumfungulia mashitaka akithibitika
Wasira: Tuamini kwamba haya yote ni kwa maslahi ya watanzania, CCM imeshirikiana na kambi ya upinzani kufanya maamuzi sahihi
Spika awahoji wabunge, na wao wamepitisha azimio la bunge kama lilivyosomwa na @zittokabwe

MC NAPIA NI MCHEKESHAJI RAY.AKIWA NA MCHEKESHAJI MAARUFU KUTOKA NIGERIA SOMA KILICHOJIRI


Show ya Ence bukuku iliyofanyika golden tulip,usiku wa kuamkia leo show ambayo iliudhuruwa na watu wengi kupita kiasi.show ilianza majira ya saa tatu usiku.na aliyefungua show ni mchekeshaji anaechipukia ajulikanae kama dr.mjusi aliyeigiza sautiya MH.J MRISHO KIKWETE,na kufuatiwa na mchekeshaji kutoka VUVUZELA COMEDY SHOW anaetambulika kwa jina la Side story.balaa lilianza pale alipo panda mchekeshaji mkongwe na bingwa wa kuiga sauti za watu mashuhuri Ray,alikonga nyoyo ya mashabiki hasaalipoigiza sauti ya mtangazaji maarufu wa kituo cha TV,bwana Godwin Gondwe,alizidi kukonga nyoyo ya mashabiki pale alipoigiza sauti ya mwenyekiti wa chadema MH.MBOWE, kelele  za vicheko vilisikika pale alipoigiza sauti ya MH.MKAPA.
msanii huyu aliweza kukonga nyoyo za mashabiki na kuwagusa hasa pale alipoigiza sauti ya mfanyabiashara maarufu bwana MENGI.
show ikafuatiwa na msanii muimbaji bora wa kike Tanzania Enika likonga nyoyo za mashabiki kwa kuimba nyimbo mbili na baadae akafuatiwa na msanii oscer.balaa likarudi tena pale alipopanda msanii anaefanya show za ucheshi nje ya Tanzania ambae ni mtanzani ajulikanae Keptain khaleed,aliweza kuwakamata watanzania kisawasawa mwanzo mwisho watanzania ni kufurai,
Baadae alipanda DOGO PEPE.alipoitwa tu kelele zilisikika na alipoingia jukwaani alifanya kweli DOGO PEPE alifunika sana.
ilikuwa ni balaa pale alipopanda the best comedian kutoka Nigeria Basket Mouth.atakama ulikuwa mgumu vipi kucheka ni lazima utacheka tu.watanzania walilipuka kwa vicheko kiasi kwamba wengie walishindwa kuvumilia na kutoka nje ya ukumbi uku machozi yakiwatoka kwa kucheka.
Mshereheshaji alikuwa ni the best comedian kutoka Tanzania EVANSE BUKUKU.alikonga nyoyo za mashabiki kisawasawa kiasi kwamba Basket Mouth alishindwa kuvumilia akaanza kucheka mpaka machozi yakimtoka akiwa Backstage kabla ajapanda na kumwambia Host wake BUCH,kwamba EVANSE kashamaliza kazi sasa yeye ataenda kufanya nini?

RAISI KIKWETE ASEMA AMEPONA SARATANI.

 


Rais kikwete akitoa hotuba yake kwa taifa .Amesema kuwa amepona saratai ya kibofu.

Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania amesema amepona saratani baada ya kufanyiwa upasuaji mapema mwezi huu nchini Marekani.
Kiongozi huyo wa Tanzania mwenye umri wa miaka 64 ametoa hotuba kwa taifa kuelezea afya yake..
"Niligundulika kuwa na hatua ya pili ya saratani ya kibofu, ambayo baadaye ikaonekana kuwa ni hatua ya kwanza," alisema Kikwete katika hotuba iliyotangazwa moja kwa moja kupitia televisheni akiwa uwanja wa ndege wa Dar Es Salaam baada ya kurejea kutoka Marekani.
Aliongeza kuwa madaktari wamesema sasa hali yake shwari: "Madaktari walisema saratani haikuenea katika sehemu nyingine za mwili na baada ya upasuaji sasa wamesema nimepona saratani."
Alisema aligundulika kuwa na saratani ya kibofu zaid ya mwaka mmoja uliopita na alifanyiwa upasuaji katika hospitali ya Johns Hopkins Hospital tarehe nane Novemba.
Kikwete ambaye anamaliza muhula wake wa pili mwakani amesema wananchi wajenge tabia ya kupima afya zao ili wagundue maradhi mapema.

Ijumaa, 28 Novemba 2014

IKULU YAHUSISHWA NA ESCROW.


 



Ikulu ya rais nchini Tanzania
Bunge la Tanzania hapo jana liliambiwa kwamba afisa mmoja wa ikulu ya rais bwana Prosper Mbena aliandika barua ili kushinikiza hatua ya kutolewa kwa billioni 306 fedha za Escrow kutoka banki kuu ya Tanzania.
Bwana Mbena ambaye anafanya kazi kama katibu katika afisi ya rais aliandika barua mwaka uliopita akiiagiza wizara ya fedha kuzitoa fedha hizo kama ilivyoamrishwa na mwanasheria mkuu.
Kushirikishwa kwa ikulu ya ya rais kulizuka baada ya wabunge kujadili ripoti kuhusu kashfa hiyo ambayo imeikumba serikali ya Tanzania katika miezi kadhaa iliopita.
Kiongozi wa upinzani katika bunge,Bwana Freeman Mbowe pamoja na kinara wa bunge upande wa upinzani bwana Tandu Lissu alifichua jukumu lililochukuliwa na afisa huyo wa ikulu kushinikiza madai kwamba baadhi ya maafisa wakuu serikalini walihusika katika utoaji wa mabilioni hayo ya fedha.
Ripoti hiyo imesema kuwa fedha hizo za Escrow ni za walipa ushuru wa Tanzania na kwamba zilitolewa kwa njia ya ufisadi na kugawanywa miongoni mwa watu maarufu.

WAFANYABIASHARA WA UG WAIONYA KENYA,LASIVYO WATAAMIA TZ.



Wafanyibiashara wa Uganda wameonya kuihama bandari ya Mombasa kutokana na ada mpya za mara kwa mara.
Wafanyibiashara wa Uganda chini ya muungano wa Wanabiashara wa mji wa Kampala Uganda KACITA wamelipa Shirika la ukusanyaji Ushuru nchini kenya KRA wiki mbili kuitoa mizingo yote inayoelekea Uganda la sivyo waigomee bandari ya Mombasa.
Ilani hiyo iliafikiwa siku ya Alhamisi baada ya saa kadhaa za majadiliano kuhusu athari za hatua ya KRA ya kutoza kodi bidhaa zote zinazoingia katika badari hiyo.
Awali ,wafanyibiashara walikuwa wakilipa ada wanayotozwa wakati wanapochukua mizigo yao pamoja na ada nyenginezo.
Hatua hiyo kulingana na KACITA si kinyume na matarajio ya jumuiya ya Afrika mashariki pekee bali pia inawaumiza wafanyibiashara wa Uganda pamoja na uchumi.
Mwenyekiti wa KACITA Everest kayondo amesema kuwa kufikia jumatano kulikuwa na makasha 4,000 yanayozuiliwa katika Bandari ya Mombasa kutokana na ada za mara kwa mara zinazotolewa na KRA.
''Kwa hivyo tunaipa KRA wiki mbili kutoa mizigo yote ya Uganda la sivyo tuhame hadi katika bandari ya Dar es Salaam'',.aliongezea
Wafanyibiashara hao pia walikubaliana kwamba iwapo mahitaji yao hayataafikiwa ,wataishinikiza serikali ya Uganda kuzuia bidhaa za kenya zinazoingia katika soko la Uganda

BUNGE LASAMBARATIKA.


Mzozo mkubwa umesababisha Bunge la Tanzania kuvunjika usiku wajana wakati likiendelea na mjadala wa kashfa ya Escrow, baada ya wabunge kushindwa kukubaliana njia sahihi ya kuwawajibisha baadhi ya viongozi wa kisiasa wanaotuhumiwa kuhusika na sakata la wizi wa Zaidi ya fedha za Tanzania shilingi bilioni 300 kutoka Benki Kuu ya nchi hiyo.
Taarifa ya mwandishi wetu imesema kuwa Bunge hilo, jana
limeweka rekodi ya kuwa na mjadala wa muda mrefu Zaidi kuliko wakati mwingine wowote. Hadi kufikia kuvunjika kwa kikao hicho ilikuwa ni saa 4.30 usiku kwa saa za Afrika Mashariki. Spika wa Bunge hilo Anne Makinda karibu muda wote wa kikao hicho alijikuta akitoa tahadhari kwa wabunge wake kujilinda na hatua za kuingilia mihimili mingine ya utawala ya Tanzania ambayo ni Mahakama na Serikali. Hatua hiyo kwa namna Fulani iliamsha hisia tofauti kutoka upande wa kambi ya upinzani pamoja na wajumbe wa kamati ya hesabu za Serikali ambao walitishia kutoka nje hadi viongozi wanaodaiwa kulindwa na bunge hilo wawajibike wenyewe. Bunge hilo linategemewa kuendelea na kikao chake hapo kesho.

BI HARUSI WA MIAKA 14,AMPA SUMU MUMEWE.

 
Msichana mdogo alieolewa 
Bi harusi wa miaka 14 nchini Nigeria ameshtakiwa kwa kuwaua watu wanne akiwemo mumewe wa miaka 35 baada ya kuweka sumu ya panya katika chakula alichoandaa kwa sherehe za haruysi yake.
Kesi hiyo imewashangaza wahaharakati wa haki za kibinaadamu ambao wamesema kuwa msichana aliyeozwa kwa mume aliye mara mbili umri wake anafaa kuchukuliwa kama mwathiriwa na wala sio muhalifu.
Wasila tasiu kutoka familia masikini katika eneo la waislamu la kazkazini huenda akakabiliwa na kifo iwapo atahukumiwa.
Shahidi wa kwanza wa kiongozi wa mashtaka Lamido Abba Sorron-Dinka alikuwa msichana wa miaka 7 anayejulikana kama hamziyya,ambaye alikuwa akiishi katika nyumba moja na Tasi'u pamoja na mumewe Umar sani,wakati bi haru huyo alipoweka sumu ya panya katika chakula hicho.
Hamziyya alijulikana tu kama dadaake mke wa kwanza wa bwana Sani,mwanamke aliyeolewa na marehemu awali katika eneo ambapo ndoa za wake wengi zimekithiri.
Msichana huyo wa miaka 7 alisema kwamba Tasi'u alimpa fedha ili kununua sumu ya panya kutoka duka moja jirani mnamo tarehe 5 mwezi Aprili,siku ambayo bwana Sani alifariki.
''Alisema kuwa panya wanamsumbua katika chumba chake'',Hamziyya aliiambia mahakama.Upande wa mashtaka baadaye ulisema kuwa badala yake Tas'u aliweka sumu hiyo ya panya katika chakula ambacho alikuwa amekiandaa kwa sherehe za baada ya harusi kwa kuwa alijuta uamuzi wake wa kumuoa bwana Sani.
Msichana huyo alikataa kuzungumza mahakamani.
Jaji Mohammed Yahaya,katika mahakama ya Gezawa alitoa hukumu kwamba Tasi'u ambaye alikataa kuongea katika mahakama hana hatia katika kusikizwa kwa kesi mnamo mwezi Octoba ambapo alisomewa mashtaka.
Jaji huyo alikataa ombi la upande wa mshtakiwa la kesi hiyo kupelekwa katika mahakama ya watoto.
Ushahidi wa Hamziyya uliungwa mkono na Abuwa Yussuf muuzaji duka katika mji wa Unguwar Yansoro ambaye alithibitisha kuuza sumu hiyo kwa mtoto huyo.
Jirani ya Bwana Sani mwenye umri wa miaka 30 ambaye ni mkulima, Abdulrahim Ibrahim alitoa ushahidi ambapo alisema kwamba alipewa chakula hicho kilichopikwa na Tasiu.''Nilipoletewa chakula hicho niliona vipande vipande vyeusi''aliiambia mahakama.
Alikula vipande vinne vya madonge vilivyotengezwa na maharagwe lakini hakupendelea ladha yake'',alisema na kuongezea kuwa ni Umar pekee aliyeendelea kula.
Baadaye alisema kuwa alimuona bwana Sani katika bustani ,akiwa mgonjwa na kumpeleka nyumbani.
Lakini alipokuwa akijaribu kumuuguza bwana sani ,aligundua kwamba watu wengine watatu ambao walikuwa wamekula chakula hicho wamefariki kwa ghafla.
Viongozi wa mashtaka walidai kwamba chakula cha Tasiu kilichowekwa sumu kiliwaua watu wanne na hivyobasi kuwajumuisha wanne hao katika kesi moja ya mauaji.
Nigeria haijawahi kumyonga mtoto aliyefanya uhalifu tangu mwaka 1997,ambapo taifa hilo liliongozwa na dikteta Sani Abacha,kulingana na shirika la kibinaadamu la Human Rights Watch.
CHANZO BBC.

Alhamisi, 27 Novemba 2014

ASKFU KILAINI AZUNGUMZIA TUHUMA ZA ESCROW

 
ASKOFU KILAINI AKIRI KUPOKEA MILIONI 80.5
Askofu msaidizi wa jimbo la Bukoba Methodius Kilaini amekiri kupokea milioni 80.5 kutoka kwa James Rugemalira na akisema hii si mara yake ya kwanza kupokea fedha toka kwa mfanyabiashara huyo kwakuwa mara nyingi huwa anachangia kwa uwazi miradi ya jamiii. Na amesema michango inayopelekwa kwake haina siri hivyo washikwe wezi halisi sio yeye

NGOJA NIVAE BUTI NIENDE ZANGU SHAMBANI........

HAYA NDIO MAAJABU,MAHARUSI WAOANA NDANI YA BWAWA LA MAJI.


Maharusi wawili walifanya harusi yao katika bwawa lenye lita milioni 1.5 za maji ya bahari .
Bwawa hilo hutumiwa kutoa mafunzo ya kupiga mbizi katika kituo cha Fort William.

 Bi Dorota Bankowska mpiga mbizi mzoefu aliolewa na mpenzi wake ambaye ni mwalimu James Abbot nyumbani kwao mjini Plock , Poland mwezi jana lakini akataka sana kufanya jambo la kipekee wanakoishi kama ishara ya kusherehekea harusi yao.


Bi Abbott alipokea mafunzo ya upigaji mbizi katika kituo hicho kilicho katika ufuo wa bahari ya Loch Linnhe mnamo mwaka 2007 na kuwaomba wafanyakazi wa kituo hicho wamruhusu afanye harusi yake chini ya maji hayo.
Bwawa hilo, hutumiwa kutoa mafunzo kwa wapiga mbizi pamoja na kufanyia majaribio vifaa vipya. Picha hizi zimetolewa na kituo hicho.
Bi harusi alivalia gauni nyeupe huku bwana harusi akivalia sketi ambayo huvaliwa na waskochi ijulikanao kama 'Kilt'.
Maharusi hao waliungana na marafiki wao Ala Bankowska na Charlie Cran-Crombien chini ya maji hayo.
Wote wanne walivalia vifaa vya kupigia mbizi pamoja na mavazi yao ya harusi.
Takriban wageni 100 walitazama harusi hio wakiwa nje
Bi Abbott anafanya kazi katika kiwanda cha mafuta na gesi.
CHANZO BBC.

MABOMU YARINDIMA NIGERIA


Taharuki ya mabomu
Watu wapatao ishirini na watano wamekufa kufuatia shambulio la bomu katika jimbo la Adamawa Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.
Imetaarifiwa kwamba wote waliouawa katika shambulio hilo ni raia na watano askari.tukio hilo limetokea karibu na mji wa Mubi ambao mwezi huu ulikuwa ukishikiliwa na vikosi vya serikali ya nchi hiyo baada ya kuukomboa kutoka katika himaya ya wanamgambo wa kikundi cha kiislam cha Boko Haram.
Kuna matukio kadhaa ya mashambulizi yanayofanywa na kundi la Boko Haram katika siku za hivi karibuni ikiwemo na matukio mawili ya kujitoa muhanga kaskazini Mashariki mwa mji wa Maiduguri,shambulio ambalo liligharimu uhai wa watu nane.
CHANZO BBC.

VIONGOZI VING'ANG'ANIZI WAPEWA SOMO.


 
Raisi wa Ufaransa Francois Hollande 
Raisi wa Ufaransa Francois Hollande amewapa somo viongozi wa bara la Afrika,kwamba wanapaswa kujifunza kwa yale yaliyotokea nchini Burkinafaso na sio kung'ang'ania madarakani.
Kauli ya raisi Hollande imetoka katika mkutano wa nchi zinazozungumza kifaransa ,unaofanyika nchini Senegal,na kutolea mfano kwa kile kilichomkuta na kumuondoa madarakani Blaise Compaore na kutilia mkazo suala la katiba kuheshimiwa.
Akiipigia chapuo nchi yake ,Raisi Hollande amesema nchi yake iliepusha umwagikaji wa damu na kumsaidia Compaore kuokoa jahazi lililokuwa likielekea kuzama.
Maandamano makubwa yamepangwa kufanyika hivi leo nchini Togo wakati ambapo raisi Faure Gnassingbe anataka kuibadili katiba ya nchi hiyo ili aendelee kusalia madarakani.
Kufuatia kitendo hicho, raisi Hollande amesema kwamba muda wa Ufaransa kuingialia migogoro ya nchi zilizokuwa makoloni yake umekwisha kilichosalia ni kuona wale wote wanaozungumza kifaransa nchi zao zinafuata utawala wa kidemkrasia.
CHANZO BBC

ESCROW: WAZIRI MKUU AWAJIBISHWE.

Mizengo Pinda waziri mkuu wa Tanzania ametajwa kwenye ripoti hiyo iliyowasilishwa bungeni 
Ripoti ya Kamati ya bunge ya Hesabu za Serikali imewataja baadhi ya vigogo wanaohusika na kashfa ya IPTL Nchini Tanzania akiwemo Waziri Mkuu na kuwataka kuwajibika kisiasa na kisheria.
Sakata hiyo ya IPTL inahusihswa na upotevu wa mamilioni ya fedha na kwa muda mrefu umezusha mjadala mzito katika bunge la Tanzania.
Katika ripoti hiyo iliyowasilishwa na mwenyekiti wa kamati hiyo Zitto Kabwe na makamu mwenyekiti Deo Filikunjombe, imethibitisha kuwepo mazingira ya udanganyifu na ufisadi katika mchakato wa malipo yaliyofanyika na kueleza kuwa upotevu huo wa fedha ungeweza kudhibitiwa kama kungekuwa na uwajibikaji wa kutosha kwa baadhi ya viongozi.
Zitto Kabwe
Kamati hiyo imewataja viongozi wengine wanaotakiwa kuwajibika kutokana na kashfa hiyo kuwa ni mwanasheria,Waziri wa nishati na Madini, Naibu Waziri wa Nishati pamoja na viongozi wengine wa bodi.
Ripoti hiyo ilitokana na ukaguzi uliofanywa na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ambayo ilianika ukiukwaji mkubwa wa taratibu wakati wa uchotaji wa fedha hizo pia mahojiano na mkurugenzi mkuu wa Takukuru na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Waziri Pinda amelimbikizwa lawama ikidaiwa kuwa alijua kuwapo kwa ufisadi huo na matamshi yake kuwa fedha hizo hazikuwa mali ya umma, wakati Mwanasheria Mkuu Jaji Frederick Werema ameonekana kutoishauri vizuri Serikali na pia kuagiza fedha hizo zitolewe kwenye akaunti hiyo.
Waziri Sospeter Muhongo amelaumiwa kwa kukosa kuchukua hatua wakati akijua kuwapo kwa sakata hilo, huku naibu wake, Stephen Masele akitiwa hatiani kwa kulidanganya Bunge.
Kashfa nyingine zilizowahi chukua uzito mkubwa katika bunge la Tanzania na kusababisha viongozi kuwajibika wakiwemo Waziri Mkuu ni pamoja na kashafa ya Richmond,EPA na sasa hii ya ESCROW ambayo kwa mara nyingine kamati hiyo imeonyesha wazi mapendekezo yake ya kutaka kuwajibika kwa waziri mkuu, Mawaziri na viongozi wengine.

TUNDU LISSU AMEFUNGUKA BUNGENI NA AMESEMA MH.MUHONGO AMESEMA UONGO


Lissu: Naomba niseme kuwa Bunge lako limepotoshwa moja kwa moja na Mh. Muhongo
Lissu: Kiambatanisho namba 2 sio ushahidi wa standard charted Hong Kong kutambua chochote ila ni hati ya madai.
Lissu: Vitambulisho viwili alivyoleta Muhongo ni kesi za mahakama kuu za mwaka huu, hazina ushahidi wowote wa tuhuma zake
Lissu: Kwa ushahidi wa taarifa ya kamati na CAG hizi ni pesa za umma, kama zisingekuwa za umma Rais asingeelekeza zilipwe
Lissu: Inakuwaje pesa za binafsi zitolewe maamuzi na Rais, Mawaziri, na Magavana?
Lissu: PAP waweze kupewa hizi pesa ilibidi wapewe kibali na Waziri Muhongo, lakini haijapata usajili hivyo si kampuni halali.
Lissu: Ndani ya siku moja zimetoka bilioni 78, na kama fedha zinazodaiwa ni binafsi kwanini wapewe Viongozi wa Umma na dini?
Lissu: Kuna ushahidi wa kutosha unaothibitisha kuwa hizi ni fedha za umma. TRA, TAKUKURU na CAG wamekiri ni fedha za umma
Lissu: Rushwa tupu imetambaa hadi mahakamani, Majaji wanapewa fedha tukiuliza mnasema ahahahha.
Lissu: Waziri Mkuu, Tibaijuka , Muhongo na wote waliotajwa walioko humu ndani, tuanze nao maana hawa tunawaweza
Lissu:Kuna la kusisitizwa hapa kuhusu BOT,Benki kuu ni huru na haiwezi ikajificha nyuma ya ushauri mbovu wa Mwanasheria mkuu.
Lissu: TRA pekee ndio chombo kikuu chenye mamlaka hapa nchini kutoa ushauri juu ya ushuru upi wa kodi ulipwe
Lissu: Mwanasheria Mkuu sio mshauri mkuu wa maswala ya kodi hapa nchini ila TRA.
Lissu: Kamati inasema Waziri Mkuu awajibike kwakuwa ndiye mwajibikaji mkuu wa shughuli za serikali, hii ni sahihi kabisa.
Lissu: Tunamwachaje Waziri wa wizara ya fedha ambaye ndiye mhusika mkuu wa masuala ya fedha?
Lissu: Mkuu wa Kitengo cha Financial Intelligence Unit ndani ya Wizara ya Fedha anatakiwa kuwajibika
Lissu: Leo yametokea yaliyozungumzwa toka mwaka 1994 kuwa IPTL itakuja kutuumiza
Lissu: Tunataka fedha zetu zirudi maana leo haya yanatokea Jakaya Kikwete ndiye Rais wa nchi
Lissu: Wakati IPTL inakuja, Rais Kikwete alikuwa Waziri wa Nishati na Madini, wakati wanasaini mkataba alikuwa Waziri wa Fedha
Lissu: Hakuna jambo baya kama Hakimu kupewa milioni 400, na hiyo sio dhihaka ila ni wajibu wetu kuyasema haya

MKE ASIPOPEWA HESHIMA HAWEZI KUMTHAMINI MWANAUME



Kuna wanaume ambao kwa kutokujua wanadhani mwanamke anachohitaji ni ‘fidia’ baada ya kuvunjiwa heshima, hivyo huwa wanawavunjia heshima wake zao na baadae kujitoza ‘fidia’ kwa kuwanunulia zawadi kubwakubwa wanawake hao.
Wanawake huwa wanapokea zawadi hizi, lakini hii haina maana kwamba ndoa itaendelea kuwa ya amani na upendo. Mwanamke hata kama atapewa dhahabu yote duniani, kama atajua kwamba mumewe hamheshimu, ni wazi kwamba hatakuwa na furaha ya ndoa. Miongoni mwa mambo sita ambayo mwanamke akiyakosa huhisi kutindikiwa na kukosa furaha ya uhusiano ni heshima.

Kama haki ya mwanamke hailindwi na mwanaume, hata kama kuna kitu gani, ndoa ni lazima itakuwa ni ya kubahatisha. Mwanume anapokuwa na uhusiano wa kipapenzi nje ya ndoa yake, mwanaume anapomzuia mkewe kuamua masuala yake mwenyewe ambayo ni haki yake, kamwe mwanamke hawezi kuridhishwa na hayo na hata kama ndoa imejaa watoto wazuri wenye afya na akili na fedha nyingi zimeipamba nyumba yake.
 Kama mwanaume ataonyesha kutojali kuhusu matamanio au ndoto za mkewe kamwe mwanaume huyo asitarajie kuwa mkewe atakuwa na upendo naye. Mwanamke huwa anatamani sana kuona mumewe anajali na kuyapa uzito matamanio au ndoto za mkewe. Kwa mfano mwanamke anapoonyesha kwamba, angependa kuanzisha shughuli labda ya biashara au wangependa wapate mtoto na mwanaume akaonyesha kutojali kuhusu matamanio hayo, kamwe mwanamke hawezi kutulia na kuwa na amani.

Kuna vitu au mambo ambayo mwanmke anayahitaji maishani, mahitaji hayo ni mengi yakiwemo yale ya msingi katika maisha na yale ya kawaida. Inatosha kusema kwamba, mwanamke anapogundua kwamba mumewe hajali juu ya mahitaji yake huwa hajisikii vizuri.
Kwa ujumla tunaweza kusema kwamba mwanamke huhitaji heshima katika utashi na matamanio yake. Anapogundua kwamba utashi na matamanio yake havizingatiwi na mumewe hawezi hata mara moja kumkubali mume huyo. Kumkubali hapa ina maana ya kumkubali na kumtambua.

Hapo ndipo tatizo ambalo ni la upande wa pili huanza. Kwa maumbile mwanaume huwa anataka sana mkewe akimuonyesha kwamba anamthamini na kumtambua. Labda hii inatokana na ubabe wa asili wa wanaume ambapo kila wakati angependa kuona mwanamke akimgwaya na kuonyesha kwamba anamtambua kama ‘mwokozi’ wa aina fulani.

Kama mwanamke anataka kumfanya mumewe amsikilize na kujali matamanio na ndoto zake anachotakiwa kufanya ni kumuonyesha mumewe kwamba anamthamini na kumtambua. Kwa mfano mwanaume anapofanya jambo ambalo hata kama halina faida, lakini halina madhara, inabidi mkewe aonyeshe kuzitambua juhudi hizo na kuonyesha kwamba, mume huyo anajitahidi sana katika kufanya mambo yake.
Mwanaume anahitaji sana kuona mwanamke akimsifu kwa juhudi anazofanya, iwe ni za kitabia au za shughuli. Mwanaume anapokuwa na tabia nzuri, ni lazima mwanamke atafute kila njia ya kumuonyesha kwamba ameitambua tabia yake hiyo, kamwe asimuonyeshe kwamba juhudi anazofanya ni kupoteza muda. Pale ambapo mwanaume huonyesha heshima kwa mkewe kwa kuzijali ndoto na matamanio yake ya kimaisha, huhitaji sana kuonyeshwa kwamba heshima yake hiyo imepokelewa. Kwa kawaida mume anapotimiza wajibu wake lazima mke naye atimize wajibu wake.

Kuna wakati na karibu mara zote, mwanamke huwa anamlaumu mwanaume na mwanaume kumlaumu mwanamke kwa kila mmoja kudhani kwamba mwenzake ndio chanzo cha matatizo. Hii ni kwa sababu wote wawili hawajui namna nadharia hii inavyofanya kazi. Huyu anataka kuthaminiwa wakati hampi mwenzake heshima na huyu anataka kupewa heshima wakati hamthamini mwenzake.
Ili kuondoa kulaumiana huko inabidi kila mmoja ajue wajibu wake, kwani kama mmoja ataanza kumpa mwingine kile anachohitaji ni wazi huyu mwingine atajibu kwa kumpa mwenzake kile kinachomstahili mwenzake ambacho ni heshima.

MC.RAY
WHATSAPP 0659/375263
INSTAGRAM MC.RAYMONDMUSHI
FACE BOOK Raymond Mushi
PAGE Rayshughuli