Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumapili, 16 Novemba 2014

KIKAO CHA BUNGE CHATIBUKA SOMALI

 
Kikao cha wabunge wa Somali Chatibuka mjini Mogadishu.kikao hicho kilitarajiwa kujadili hatma ya waziri mkuu Abdiweli Sheikh Ahmed 
Kwa mara ya pili katika kipindi cha juma moja ,kikao cha wabunge wa Somali kilichoitishwa ili kuijadili hatma ya waziri mkuu nchini humo kimeisha kwa kelele na ghasia.
Wabunge walitarajiwa kupiga kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu Abdiweli Sheikh Ahmed ,lakini wafuasi wake walikataa kukaa na kuanza kuimba na kubeba mabango.
Bunge la Somali limelemazwa na mgogoro uliopo kati ya waziri mkuu na rais Hassan Sheikh Mhamud.
Marekani imesema kuwa kura hiyo ya kutokuwa na imani haina maslahi ya raia.
Umoja wa mataifa nao umesema kuwa una wasiwasi kuhusu ufisadi wa ununuzi wa kura unaokabili kura hiyo.
chanzo BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni