Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumanne, 18 Novemba 2014

WANAUME ZAIDI YA MMOJA HULIPIA NGONO UK.

Sehemu kubwa ya Watu wanaonunua ngono ni Vijana
Zaidi ya mwanaume mmoja kati ya 10 wanaelezwa kulipia vitendo vya ngono, utafiti kuhusu tabia za ngono nchini Uingereza.
Asilimia 11 ambao wamefanya hivyo walitembelea maeneo ambapo kuna vivutio vya biashara ya ngono kama vile mjini Bangkok na Amsterdam.
Ripoti kutoka jarida liitwalo Sexually Transmitted Infections inasema tabia za kulipia ngono zina uhusiano na tabia nyingine zilizo hatarishi kama vile ulevi na matumizi ya dawa za kulevya.
Ripoti imeeleza kuwa vijana wadogo kuliko watu wazima wanalipia ngono.
Kati ya wanaume 6,108, asilimia3.6 wamelipia ngono kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita na asilimia 1.1 mwaka jana.
Kiongozi wa utafiti huo,Dr.Cath Mercer ameiambia BBC kuwa watu hawa wanaonesha kuwa wana wenzi wengi.
Hata hivyo hali hiyo imeonesha uwepo wa madhara, wanaume waliolipia ngono kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita wako hatarini kukutwa na maradhi ya zinaa na Ukimwi.
Kundi kubwa ambalo hivi karibuni lililipia biashara ya ngono nchini Uingereza ni vijana wa umri wa kati ya miaka 20 na 30,miongoni mwa hawa wengi wao hawajaoa,wakiwa na weledi mzuri,ajira na matumizi ya dawa za kulevya.
chanzo BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni