Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumamosi, 22 Novemba 2014

TAARIFA YA (CAG) YAKUTWA IKISAMBAZWA MITAANI IKIWA IMENYOFOLEWA KURASA

 


 Taarifa ya mdhibiti na mkaguzi wa hesabu za serikali kuhusiana na kashfa ya wizi wa bilioni 321 kwenye akaunti ya tegeta Escrow iliyokabidhiwa kwa katibu wa bunge imekutwa inasambazwa mitaani huku ikiwa imenyofolewa kurasa tatu za mwisho zenye majina ya waliohusika na mgawo wa fedha hizo kwa lengo la kutengeneza propaganda ili kuwadanganya wananchi kuwa taarifa hizo hazijawataja wahusika.

Akizungumza na waandishi wa habari mwenyekiti mwenza wa ukawa Mh. James Mbatia amesema zipo taarifa za baadhi ya waliokuwa wanasambaza taarifa hizo kuwa wamekamatwa na jeshi la polisi na kuwataka wananchi kutoa taarifa kituo cha polisi ili waweze kuchukuliwa hatua haraka ambapo amesesistiza kwamba (UKAWA) wanataka taarifa hiyo iwasilishwe bungeni kwa ajili ya kujadiliwa Jumatatu .

ITV imemtafuta kamanda wa polisi mkoa wa dodoma David Misime na katibu wa bunge Dr.Thomas Kashilillah ambao wamesema nao wanazisikia taarifa hizo na wanazifanyia kazi ili kutoa taarifa yao.

Chanzo: ITV

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni