Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatano, 19 Novemba 2014

FAMILIA YA BOB MARLEY KUUZA BIDHAA YA BANGI


Familia ya aliyekuwa mwanamuziki wa Jamaica, Bob Marley imezindua kampuni ambayo wanaitaja kama ya kwanza duniani kuuza bidhaa za Canbbisa au marujuana au Bangi kama wanavyoijua wengi.
Bidhaa hizo zitajulikama kama 'Marley Natural' na na zitajumuisha mafuta ya urembo pamoja na manukato mengine ya wanawake na bidhaa nyinginezo.
Bidhaa hizo zitatengezwa na kampuni kubwa ijulikanano Privateer Holdings iliyo mjini Washington Marekani, ikisisitiza kutaka kudumisha kumbukumbu ya mwanamuziki huyo aliyesifika kote duniani.
Bidhaa hizo zitauzwa nchini Marekani na kwingineko duniani kunzia mwaka jana.
Mwanawe Bob Marley, Cedella Marley, alisema hayati babake angekuwa hai angefurahishwa sana na wazo hilo.
 Bidhaa hizo zitakuwa za urembo kama vile mafuta na manukato
 ''Babangu angekuwa na fahari kubwa kuona watu wakitambua uwezo wa kuponya wa Bangi,'' alisema Cedella.
Mkuu wa kampuni hiyo, Brendan Kennedy alisema Marley alikuwa mtu ambaye kwa njia nyingi alisaidia kuanzisha harakati za kupinga juhudi za kuharamisha Bangi miaka 50 iliyopita.
"Marley alipenda sana kutumia Bangi na hakuna aliyemshinda kwa hilo duniani kote. ''
Bob Marley alifariki mwezi Mei mwaka 1981, kutokana na Saratani.Alipenda sana kutumia Bangi kama sehemu ya imani yake ya Rastafarian na kuunga mkono kuhalalishwa kwake.
Matumizi ya Bangi kwa ajili ya kujiburudisha yamehalalishwa katika majimbo ya Colorado na Washington nchini Marekani.
Majimbo mengine huenda yakaidhinisha matumizi ya Bangi nchini Marekani na mengine tayari yanaruhusu utumiaji wa bidhaa hiyo kwa sababu za matibabu.
chanzo BBC.
 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni