Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumapili, 23 Novemba 2014

UCHAGUZI WA RAISI TUNISIA.


 

  Raia wa Tunisia katika zoezi la upigaji kura
Wananchi wa Tunisia leo wanapiga kura katika uchaguzi wa kwanza wa Rais tangu kutokea vuguvugu la mapinduzi mwaka 2011.
Mapinduzi hayo yalisababisha vuguvugu hilo la mabadiliko kutabakaa katika nchi nyingine za Kiarabu.
Miongoni mwa wagombea katika kinyang'anyoro hicho ni mwanasiasa mkongwe Beji Essabsi, aliyewahi kushika nafasi muhimu wakati wa utawala kabla ya kutokea mapinduzi.
Bwana Beji Caid Essabsi anayepewa nafasi kubwa ya kushinda uchaguzi huo ameahidi kurejeha kiwango cha juu cha utulivu wa kisiasa na kiuchumi.
Mpinzani wake wa karibu ni Rais wa mpito wa sasa Moncef Marzouki ambaye amejenga jina lake kama mpigania haki za binadamu na kama msimamizi wa moyo wa mapinduzi na anayetamani mabadiliko. Waziri wa Ulinzi wa Tunia Ghazi Jeribi amesema ana matumaini nchi itasonga mbele kidemocrasia.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni