Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatatu, 24 Novemba 2014

USAFIRISHAJI WATOTO WA MAGENDO WAONGEZEKA

Thuluthi moja ya wahanga wa biashara ya kusafirisha binaadamu kwa magendo ni watoto na idadi yao kwa jumla imekuwa ikizidi kuongezeka.Ripoti iliyotolewa leo hii na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Madawa ya Kulevya na Uhalifu (UNODC) na kuhusisha kipindi cha mwaka 2010 hadi 2012 imekadiria kwamba wahanga wote wa biashara ya kusafirisha binaadamu waliogundulika walikuwa na umri mdogo. Kiwango hicho ni asilimia tano zaidi kuliko ilivyokuwa kati ya mwaka 2007 na 2010.  Tatizo hilo ni sugu zaidi barani Afrika na Mashariki ya Kati ambapo wengi wa watu wanaosafirishwa kwa magendo ni wavulana na wasichana, ingawa kwa ujumla uhalifu huo hufanyika dunia nzima. Shirika hilo la UNODC limekusanya taarifa kutoka takribani mataifa 152 ambako wahanga wamelazimishwa kuingia kwenye kazi za ngono, vibaruwa vigumu na shughuli nyenginezo. Wanaofanya biashara hiyo ya kusafirisha binaadamu mara nyingi huwaandama wanawake na wasichana.
CHANZO DW.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni