Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumanne, 18 Novemba 2014

DRC;POLISI WALIWAUA VIJANA KIHOLELA


Polisi wakipambana na vijana DRC
Ripoti ya shirika la kimataifa la kutetea haki za binaadamu Human Rights Watch inasema polisi katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo kwa jumla wamewaua vijana wapatao 51 katika operesheni ya kupambana na uhalifu Kinshasa.
Watu wengine 33 hawajulikani waliko tangu operesheni hiyo ilopewa jina "Operation Likofi", ilioidhinishwa Kinshasa mwaka uliopita kufanyika.
Human Rights Watch liliwahoji zaidi ya maafisa 100 wa polisi, watu walioshuhudia nauaji hayo pamoja na jamaa wa waathiriwa.
Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch, liliwahoji zaidi ya maafisa 100 wa polisi , walioshuhudia matukio pamoja na jamaa wa waathiriwa waliotoa taarifa ya kile kilichosemekana kuwa mauaji ya kiholela.
Msemaji wa shirika la hilo,(Anneke Van Woudenberg), alituhumu serikali kwa kuficha taarifa kuhusu mauaji hayo na kusema familia za waathiriwa zilikuwa zimetishwa na kuonywa dhidi ya kufichua taarifa za mauaji hayo.
Ripoti iliyotolewa na umoja wa Mataifa mwaka jana pia ilielezea kuhusu mauaji hayo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni