Sultan wa Sokoto aitwaye Muhammad Sa'ad Abubakar
Viongozi wa juu wa dini ya kiislam
nchini Nigeria wameli shambulia jeshi nchi hiyo na pia kuwashutumu kuwa
hukimbia mashambulio yanayofanywa na kundi la kigaidi la kiislam la Boko
Haram.
Bodi hiyo inayoongozwa na Sultan wa Sokoto,imesema kwamba
jeshi hilo limekuwa na tabia ya kutelekeza silaha zao kwa jeshi na
kukimbialia mafichoni , na pindi mambo yanapotulia hurejea uraiani na
kuwatishia raia.Maelfu ya raia wa Nigeria wamekimbilia Niger kufuatia shambulio la hivi karibuni kutoka kwa kundi hilo la Boko Haram.
Waasi hao hujifanya kuwa ni wafanyabiashara walobebelea maboksi yenye bidhaa sokoni katika mji wa Damasak mji ulio Kaskazini mwa nchi ya Nigeria.
Lakini imebainika kwamba boksi hizo huwa zimesheheni bunduki,ambazo hutumika kushambulia raia wasio na hatia.
chanzo BBC.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni