Kuna
wanaume ambao kwa kutokujua wanadhani mwanamke anachohitaji ni ‘fidia’ baada ya
kuvunjiwa heshima, hivyo huwa wanawavunjia heshima wake zao na baadae kujitoza
‘fidia’ kwa kuwanunulia zawadi kubwakubwa wanawake hao.
Wanawake huwa wanapokea zawadi hizi,
lakini hii haina maana kwamba ndoa itaendelea kuwa ya amani na upendo. Mwanamke
hata kama atapewa dhahabu yote duniani, kama atajua kwamba mumewe hamheshimu,
ni wazi kwamba hatakuwa na furaha ya ndoa. Miongoni mwa mambo sita ambayo
mwanamke akiyakosa huhisi kutindikiwa na kukosa furaha ya uhusiano ni heshima.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni