Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumapili, 23 Novemba 2014

MABAKI YA MH17KUREJESHWA UHOLANZI


 
Shirika la ulinzi la ulaya,limearifu kwamba mabaki ya ndege ya shirika la ndege la Malaysia yaliyookotwa huko mashariki mwa Ukraine hatimaye yanarejeshwa Uholanzi.
Mkuu wa shirika hilo Michael Bociurkiw ameiambia BBC mabaki yaliyokusanywa na timu ya uchunguzi kutoka Ujerumani, ambao wamekwisha ingia katika ardhi inayo dhibitiwa na serikali ya Ukraine na mabaki hayo yatasafirishwa kwa ndege kutoka katika mji wa Kharkiv.
Timu hiyo ya watafiti wa Kijerumani inaongoza timu ya watafiti wa kimataifa kufuatia ajali hiyo ya ndege iliyotokea mwezi July kutokana na maombi maalumu ya serikali ya Ukraine.
Ndege hiyo iliondoka katika uwanja wa Amsterdam na idadi kubwa kati ya abiria 298 ya waathirika wa tukio hilo ni Wajerumani .
Juhudi za uchunguzi huo zinakwamishwa na mgogoro unaoendelea huko Mashariki mwa Ukraine kati ya Urusi na nchi hiyo mgogoro ambao unaungwa mkono na askari wa majeshi ya nchi hiyo.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni