Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumanne, 25 Novemba 2014

PAPA FRANCIS HAUTUBIA BUNGE STRASBOURG


Kiongozi  wa  kanisa  Katoliki Papa  Francis  amelitaka bara  la  Ulaya  kutayarisha  sera  moja  na ya haki  katika suala la  uhamiaji, akisema  mamia  kwa  maelfu  ya wahamiaji  wanaowasili  katika  mataifa  hayo kila  mwaka kupitia  baharini  wanahitaji  kukubalika na  msaada, na  sio kuwa  na  sera  zenye  maslahi  binafsi  ambazo zinahatarisha  maisha na  kuchochea  mzozo  wa  kijamii.
Papa Francis  ametoa  matamshi  hayo  katika  bunge  la Ulaya  wakati  wa  ziara  fupi  iliyokuwa  na  lengo  la kuelezea  mtazamo  wake  kwa  Ulaya  robo  karne  baada ya  Papa John Paul  wa  pili  kuzuru  Strasbourg  na kulihutubia  bara  ambalo  bado  limegawanywa  na  pazia la  chuma.
Papa  Francis  amesema  anataka  kuleta  ujumbe  wa matumaini  kwa  watu  wa  bara  la  Ulaya  ambao hawaziamini taasisi  zao ,  zinazolemewa na  mzozo  wa kiuchumi na zikiwa  mbali  na  mtazamo  wa  kiroho katika utamaduni  ambao  amesema  hauthamini  tena  maadili  ya hadhi  ya  binadamu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni