Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Alhamisi, 20 Novemba 2014

GHARAMAZA KULEA KITAMBI NI SAWA NA ZA UVUTAJI SIGARA

Gharama za unene wa kupitiliza duniani ni karibu sawa na utumiaji wa bidhaa za tumbaku ukiwemo uvutaji wa sigara au sawa na gharama za vita na kubwa kuliko unywaji wa pombe au mabadiliko ya tabia nchi, unasema utafiti.
Taasisi ya The McKinsey Global Institute imesema inagharimu pauni za Uingereza trilioni £1.3, au asilimia 2.8% ya shughuli ya kiuchumi kwa mwaka - inagharimu pauni za Uingereza bilioni £47.
Watu wapatao bilioni 2.1 - kiasi cha asilimia 30% ya idadi ya watu duniani- wana uzito wa kupita kiasi au wana vitambi, watafiti hao wamesema.
Wamesema hatua ambazo ni wajibu wa mtu binafsi, zinatakiwa kutumiwa ili kutatua tatizo hili.
Mtu mwenye kitambi akipima tumbo lake
Ripoti hiyo inasema kuna "gharama kubwa za kiuchumi", na uwiano unaweza kukua kufikia karibu nusu ya idadi ya watu duniani ifikapo mwaka 2030.
Gharama ya fedha kwa wenye vitambi inazidi kuongezeka- kwa huduma za afya na kwa upana zaidi katika uchumi. Kwa kusababisha maradhi, kitambi kina madhara katika utendaji wa kazi na kupotea kwa tija.
Watafiti wanasema kuwa sera zenye mwelekeo zinahitajika kufikiriwa.
Dr Alison Tedstone, mkuu wa masuala ya lishe katika Public Health England (PHE), amesema: "Ripoti hiyo ni mchango mzuri katika mjadala wa vitambi. PHE imesema ujumbe wa elimu pekee haisaidii kutatua tatizo la unene wa kupitiliza."
Dr Tedstone amesema unene wa kupita kiasi unataka hatua za kitaifa na serikali za mitaa, viwanda na jamii kwa ujumla, na hakuna jibu moja katika kukabiliana na hali hiyo".
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni