Watu wapatao bilioni 2.1 - kiasi cha asilimia 30% ya idadi ya watu duniani- wana uzito wa kupita kiasi au wana vitambi, watafiti hao wamesema.
Wamesema hatua ambazo ni wajibu wa mtu binafsi, zinatakiwa kutumiwa ili kutatua tatizo hili.
Mtu mwenye kitambi akipima tumbo lake |
Watafiti wanasema kuwa sera zenye mwelekeo zinahitajika kufikiriwa.
Dr Alison Tedstone, mkuu wa masuala ya lishe katika Public Health England (PHE), amesema: "Ripoti hiyo ni mchango mzuri katika mjadala wa vitambi. PHE imesema ujumbe wa elimu pekee haisaidii kutatua tatizo la unene wa kupitiliza."
Dr Tedstone amesema unene wa kupita kiasi unataka hatua za kitaifa na serikali za mitaa, viwanda na jamii kwa ujumla, na hakuna jibu moja katika kukabiliana na hali hiyo".
CHANZO BBC.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni