Rais wa Algeria Abdelaziz Bouteflika
akitembea kwa kutumia kiti cha magurudumo.kiongozi huyo wa miaka 77
adaiwa kulazwa katika hospitali moja nchini Ufaransa.
Rais wa Algeria Abdelaziz Bouteflika amelazwa katika hospitali moja nchini Ufaransa.
Kulingana
na maafisa wa Ufaransa kiongozi huyo ambaye aliugua kiharusi mwaka
uliopita kwa sasa anapata matibu katika mji wa Gronoble maafisa wa
serikali na polisi wamesema.Maafisa hao hatahivyo hawakutoa maelezo zaidi kuhusu afya ya Bouteflika.
Bouteflika mwenye umri wa miaka 77 na ambaye ameiongoza Algeria tangu mwaka 1999 amekuwa haonekani hadharani tangu achaguliwe kwa muhula wake wa nne mamlakani mnamo mwezi Aprili.
Gazeti la kijimbo Le Dauphine Libere limesema kuwa Bouteflika alilazwa katika kitengo cha kukabiliana na magonjwa yamoyo katika mji wa kusini mashariki mwa Ufaransa.
Gazeti hilo limesema kuwa vyumba vyote katika ghorofa alikolazwa vilichukuliwa ili kuimarisha usalama.
Hatahivyo serikali ya Algeria haijatoa tamko lolote kuhusu ripoti ya rais huyo kulazwa.
Kiongozi wa chama tawala cha FNL hatahivyo amekana ripoti hizo.
chanzo bbc
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni