Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Ijumaa, 5 Desemba 2014

KAULI YA UHURU KENYATTA KWENYE TWITTER


Taarifa ya mahakama ya ICC, kutupilia mbali kesi dhidi ya Uhuru Kenyatta, imepokelwa na watu wengi nchini Kenya kwa hisia mseto.
Baadhi wanahisi kuwa waathiriwa wa ghasia za baada ya uchaguzi watakosa haki ingawa baadhi wanahisi kwua Uhuru Kenyatta hakupaswa hata kufikishwa ICC tangu hapo.
Lakini swali ni jee Rais Kenyatta alipokea vipi habari hiyo?
Rais Uhuru Kenyatta
Haya ndio aliyokuwa nayo ya kusema kwenye akaunto yake ya Twitter:
  • ''Nimepokea habari kwamba kiongozi wa mashitaka ICC ametupilia mbali kesi dhidi yangu ........''
  • ''Daima nimekuwa nikisema kuwa kesi za Kenya ICC ziliharakishwa sana kupelkewa katika mahakama ya ICC bila kufanyiwa uchunguzi wa kina.
  • "moyo wangu hauna shauku hata kjidogo. ''
  • "mara kwa mara nimekuwa nikiwasisitizia wakenya na dunia nzima kuwa sina hatua. ''
  • "uamuzi huu ni afueni kubwa sana kwangu kwani ulipaswa kutolewa miaka sita iliyopita. Umechelewa sana ''
  • ''Nimefurahishwa sana na habari hizi ambazo nimekuwa nikizisubiri tangu jina langu kuhusishwa na kesi iliyowasilishwa Hague dhidi yangu.''
  • ''Kadhalika Naibu wangu William Ruto ni kiungo muhimu sana kwa serikali yangu na ninathamini umuhimu wake''
  • CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni