Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu
Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin
Netanyahu, ameiweka nchi katika hali ya kufanyika mapema uchaguzi wa
bunge kwa kuwafukuza kazi mawaziri wawili waandamizi ambao ni viongozi
wa vyama katika serikali yake ya mseto. Wakati wa mkutano na waandishi
wa habari kupitia televisheni, Bwana Netayahu amewashutumu mawaziri wote
wawili akiwemo waziri wa Fedha, Yair Lapid, na waziri wa Sheria, Tzipi
Livni, kwa kupanga njama dhidi yake.
Bwana Netanyahu amesema
amechukua hatua hiyo kwa kuzingatia madhara yanayoweza kusababishwa na
kitendo hicho."Katika neno moja yanaitwa maasi, na hayo yanafanya
isiwezekane kuendesha serikali, iwe vigumu kuongoza nchi, kwa hiyo muda
mfupi uliopita nilimwagiza katibu wa baraza la mawaziri kutoa barua za
kuwafukuza kazi mawaziri Livni na Lapid. Pia kutokana na ulazima wa
kuhakikisha kunakuwepo serikali imara na yenye kufuata maadili, nimeamua
kusukuma mbele sheria ya kuvunja bunge na kwenda katika uchaguzi haraka
iwezekanavyo." amesema waziri mkuu Netanyahu.Wanasiasa wote wawili viongozi wa vyama vya mrengo wa kati, wamesema nchi imetumbukizwa katika uchaguzi usio wa lazima. Mwandishi wa BBC nchini Israel amesema Bwana Netanyahu huenda akataka utawala mpya utakaovihusisha vyama vya dini vinavyowakilisha madhehebu ya Wayahudi wa ultra-orthodox.
Yair Lapid waziri wa Fedha wa Israel aliyefukuzwa kazi, ambaye ni mwenyekiti wa chama cha "Yesh Atid" kilicho katika serikali ya mseto ya Bwana Netanyahu
CHANZO BBC
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni