DADA WA KAZI.JE KWA MAVAZI HAYA NDOA INAUSALAMA
Kuna jambo nimekuwa nikiliwaza na pia nimekuwa nikitumiwa
barua pepe na wasomaji wa blog hii ya rayshuhuli.blogspot.com. Wakitaka
niandike kuhusu kwa nini tunawatumia sana ma-housegirl/boy(wasaidizi wa
nyumbani)kama sio binadamu.
DADA WA KAZI AKIWAJIBIKA
Kuhusu wasaidizi wa nyumbni sitakikusema kuwa watu wasiwe na
wasaidizi la hasha! Ila tu kuna wakati utakuta wengine wanawatumia wasaidizi
hao kama mashine na sio binadamu. Yaani atafanya vijikazi hata ambavyo mke
/mume au mtoto angeweza kufanya mwenyewe kwa mfano kufua nguo za ndani(chupi)
kuchota/kuchukua maji ya kunywa. Nimewahi. Na halafu la kusikitisha zaidi
utakuta msaidizi huyohuyo anatamaniwa na mwisho kupachikwa mimba. nimewahi
kusikiliza wimbo mmoja wa Dr Remmy Ongala Hamisa ukisema hivi "Akina mama
nao jamani eti mfanyakazi wake anaanguka naye" au pia ni kinyume
"akina baba nnao jamani eti mfanyakazi wake anaanguka naye". Na hii
inatokea mara nyingi na bado tatizo hili linatokea kila siku katika jamii/ndoa
zetu.Naweza nikasema maisha ya ndoa au maisha kwa ujumla kikubwa zaidi ni KUSAIDIANA:- Nikiwa na maana ni vizuri sana kusaidiana kwani ukimwacha mwanamke afanye kila kitu ndani ya nyumba atakuwa anachoka na mwisho wake atashindwa kuitumikia ndoa yake. Na matokeo yake mume ataanza kutafuta nyumba ndogo. Lakini kama kungekuwa na umoja haingetokea hivi.
Tuwe waaminifu na ndoa zetu zitadumu na tuwatumie wasaidizi wetu kama binadamu, tuaache utumwa.
MC.RAY
WHATSAPP 0659/375263
INSTAGRAM MC.RAYMONDMUSHI
FACE BOOK Raymond Mushi
PAGE Rayshughuli
WHATSAPP 0659/375263
INSTAGRAM MC.RAYMONDMUSHI
FACE BOOK Raymond Mushi
PAGE Rayshughuli

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni