Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumamosi, 15 Novemba 2014

WATU 18.WAKAMTWA KWA UFISADI BRAZILI.

 
Raia waandamana Brazil kupinga ufisadi serikalini
Polisi nchini Brazil wamefanya uvamizi kwenye majimbo sita katika oparesheni kubwa ya kuchunguza ufisadi kwenye kampuni ya mafuta ya serikali ya Petrobras.
Watu 18 walikamatwa wakiwemo wakurugenzi wakuu wa makampuni makubwa ya ujenzi nchini brazil wanaoshutumiwa kwa kutoa hongo ili kujishindia kandarasi za pesa nyingi za kampuni hiyo ya mafuta.
Mkurugenzi wa zamani wa Perobras Renato Duque pia alikamatwa kwenye oparesheni hiyo iliyowajumuisha zaidi ya polisi 300.
Uchunguzi huo ulianza mapema mwaka huu wakati mkurugenzi mkuu wa zamani wa kampuni hiyo ya mafuta aliposema kuwa moja ya idara za kampuni ililipa mamilioni ya dola kwa wanasiasa wakiwemo wanachama wa chama tawala cha workers party
chanzo BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni