Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatatu, 8 Desemba 2014

WANAJESHI KUONGEZWA KUPAMBANA NA ISL

Wanamgambo wa Islamic State, wanaolengwa kushambuliwa. 
Muungano wa majeshi yanayopambana dhidi ya Islamic State yakiongozwa na Marekani, yako tayari kupeleka vikosi zaidi nchini Iraq.
Kamanda wa muungano wa majeshi hayo, Jenerali James Terry kutoka Marekani amesema kiasi cha wanajeshi elfu moja na mia tano wataanza kupelekwa kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa wanajeshi ya Iraq, wanaopambana na wanamgambo wa kiislamu.
Idadi ya washauri hao wa kijeshi itaongezwa kati ya wanajeshi wa Marekani zaidi ya elfu tatu, ambao Rais Obama tayari amewaidhinisha kupelekwa Iraq.
Bado haijawekwa wazi wanajeshi wengine wa ziada watatoka katika mataifa yapi.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni