Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Alhamisi, 13 Novemba 2014

MAMBO YA MSINGI UNAYOPASWA KUZINGATIA PINDI UNAPOITAJI KUTAFUTA MTU WA KUISHI NAE



Hili uweze kufurahia maisha ya ndoa ni muhimu kufanya maamuzi ya kumchagua mchumba sahihi.utakapokosea kumchagua basi maisha yako utayaona mabaya na utoweza kufuraia maisha ya ndoa utaishia kujuta siku zote    
Unapoitaji mchumba nivema ukamshirikisha Mungu,ili aweze kukuletea mchumba unaefanana nae .kumpata mchumba si kazi,Kazi kumpata mchumba alie bora.

Ni jambo la kawaida kwa vijana walio wengi, wawe wa kike au wa kiume, kuangalia sura na mwonekano wa mtu. Lakini unapotafuta mchumba kwa malengo ya kuishi naye maisha yako yote kama mume na mke haipendezi kuangalia tu mwonekano, mambo muhimu ya kuangalia na kuzingatia katika suala hil  
  1. UADILIFU 
Pamoja na sifa zote za uzuri zinazoweza kubainishwa na kufanywa kuwa vigezo vya uzuri wa mwanamke na mwanaume na hata zikatumiwa kumpata Miss au Mr Tanzania, sifa kuu impasayo mtu anayefaa kuwa mchumba kuwa nayo ni sifa ya uadilifu.Mtu anapokuwa na uadilifu (pengine uaminifu), maana yake ni kwamba tabia ya mtu huyu anayoionesha nje ndiyo tabia yake halisi na anapofanya jambo jema analifanya kwa roho yake na si kwa unafiki.
Mtu anapokuwa mwadilifu ataheshimu maadili na kufanya wema, hata pale inapokuwa rahisi kwa wengine kukengeuka na kufuata njia za mkato ambazo mara nyingi si za halali.
Mtu mwadilifu pia huwa na sifa za ukweli na kujitolea kuwasaidia watu wengine bila kujali faida – haya yote ni mambo muhimu ambayo mtu mwenye kuwa nayo huwa na msingi wa ujenzi wa uhusiano imara na wa kudumu.
Watu wanaoweza kujivunia furaha ya kweli katika maisha yao ya ndoa, ni watu ambao wamekutana wote wakiwa na sifa ya uadilifu ambayo hujumuisha mambo mengi.
Zipo ndoa nyingi zenye furaha ya bandia. Furaha hii mara nyingi hutokana na ridhiko la kimwili alipatalo mtu kutokana na kukidhiwa kwa mahitaji yake ya kimwili yanayohusiana na haki za msingi za binadamu – yaani chakula, mavazi na malazi. Lakini furaha ya kweli ya maisha ya ndoa, watu hawaipati isipokuwa katika uhusiano ambao wenza wamethibitishana kuwa waadilifu.
2. HEKIMA
INAENDELEA PAGE YA MAHUSIANO.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni