Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Alhamisi, 13 Novemba 2014

MSF KUJARIBU TIBA MPYA DHIDI YA EBOLA

 
Tiba mpya huenda ikaleta matumaini kwa Wagonjwa wa Ebola

Shirika la Madaktari wasio na mipaka, MSF limesema litafanya majaribio ya tiba mpya ya Ebola katika vituo vitatu Afrika Magharibi.
Wafanyakazi hao watatumia dawa aina mbili zilizoainishwa na Shirika la Afya duniani, WHO.
Sababu ya kufanyika kwa majaribio hayo ni kuwafanya Wagonjwa kuendelea kuwa hai wakati wa siku 14 za mwanzo tangu maambukizi ya ugonjwa huo.
Taarifa hii inakuja wakati idadi ya waliopoteza maisha kutokana na Ebola kufikia 5,160.
Ugonjwa huo umeelezwa kuathiri zaidi ya watu 14,000, karibu wote kutoka Afrika Magharibi.
Msemaji wa MSF Annick Antierens amesema hatua hiyo mpya inafanywa kwa kushirikiana na watafiti kutoka Uingereza,Ufaransa na Ubelgiji kwa lengo la kutoa nafasi ya waathirika kuwa na matumaini ya kuishi.
CHANZO.BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni