Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumamosi, 31 Januari 2015

SAUDIA YAAHIRISHA VIBOKO VYA MWANABLOGU


Maandamano ya Raif Badawi
Mamlaka nchini Saudi Arabia kwa mara nyengine tena imeahirisha adhabu nyengine ya viboko dhidi ya mwanablogu Raif Badawi.
Hakuna sababu iliotolewa,lakini awamu mbili za kutoa adhabu kama hiyo hapo awali ziliahirishwa kutokana na sababu za kiafya.
Bwana Badawi amepewa hukumu ya viboko 1000 pamoja na kuhudumia kifungo cha miaka 10 jela kwa kutusi Uislamu.
Raif Badawi na familia yake
Mwanaharakati wa Saudia ambaye pia ni wakili Suad al Shammary ambaye alifanya kazi na bwana Badawi katika blogi yake ameachiliwa huru.
Alizuiliwa kwa miezi mitatu bila kufunguliwa mashtaka kuhusu matamshi aliotoa katika mtandao wa Twitter ambayo wapinzani wake walisema yanapinga Uislamu.
CHANZO BBC.

MPINZANI WA OBAMA 2012 AJIONDOA



Mitt Romney aliyeshindwa na Obama uchaguzi wa 2012
Mitt Romney, mgombea wa chama cha Republican aliyeshindwa na rais Obama katika uchaguzi wa mwaka 2012 ameamua kutowania tena wadhfa huo.
Bwana Romney mwenye umri wa miaka 67 amesema kuwa ameamua ni muhimu kuwapatia viongozi wengine katika chama hicho fursa ya kuchaguliwa kama wagombea.
Taarifa yake inajiri wiki kadhaa baada ya tangazo lake kwamba atawania kwa mara nyengine.
Hatua yake ya kutowania inawapa fursa wafadhili kuwaunga mkono wagombea wengine.
Aliyekuwa Gavana wa jimbo la Florida Jeb Bush ,gavana wa new Jerzy Chris Christie na seneta Rand Paul ni miongoni mwa wale wanaowania kuingia ikulu ya whitehouse.
CHANZO BBC

MUGABE ATEULIWA KUWA MWENYEKITI WA AU


Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe ndio mwenyekiti mpya wa Umoja wa Afrika -Au 
Rais mkongwe wa Zimbabwe Robert Mugabe, mwenye umri wa miaka tisini, sasa ameteuliwa kuwa mwenyekiti wa muungano wa Afrika-AU.
Wajumbe walimteuwa Mugabe kwa kauli moja katika mkutano wa AU unaoendelea mjini Addis Ababa-Ethiopia.
Uteuzi wa Mugabe kuongoza muungano huo mkubwa ulio na wanachama zaidi ya arubaini, sasa umeingiza doa ndani ya AU, kwani Mugabe hana uhusiano mzuri na mataifa ya Magharibi, hasa baada ya kukaa uongozini tangu Zimbabwe ilipojipatia uhuru mnamo mwaka wa 80.

Ijumaa, 30 Januari 2015

LIPUMBA NI SAWA NA KIKWETE KWANINI APIGWE?

YANAYOJIRI BUNGENI SASA:  MJADALA JUU YA LIPUMBA KUPIGWA!! - LIPUMBA NI SAWA NA KIKWETE KWANINI APIGWE?

Spika Makinda: Hoja hii tunaijadili kwa dakika 3, namuita mchangiaji wa kwanza

Tundu Lissu: Kanuni zinasema tutumie dakika 15, haiwezekani waziri atumie dakika 30, na AG atumie 15 halafu sisi 3. Natumia 15

Spika Makinda: Haya basi tumieni dakika 10 na siyo 15, lakini tuzingatie tahadhari iliyotolewa na Mwanasheria Mkuu

Tundu Lissu: Huyu waziri wa mapolisi amesema uongo na hastahili kuwa katika nafasi kuanzia sasa

 Tundu Lissu: Sasa tumejua kuwa ile kauli ya WAPIGWE TU ni kauli ya serikali na kauli ya CCM, jeshi la polisi ni la ma 'FACIST'

 Tundu Lissu: Bunge lichukue hatua dhidi ya Polisi, waziri Mkuu, Waziri Chikawe, IGP naibu IGP. Tumechoka lazima wawajibike

Tundu Lissu: Tunahitaji tuunde tume teule kuchunguza matukio ya mapolisi kupigwa watu, tumechoka kupigwa

 Tundu Lissu: Tukiendelea hivi na tunaelekea kwenye uchaguzi mkuu Oktoba, kumbukeni nyie ni wanachama wa mahakama ya Kimataifa ICC

 Rashid Abdallah: Mauaji yanafanyika katika nchi hii, watu wanakufa, halafu jeshi la polisi lipo tu linaangalia

 Rashid Abdallah: Waziri Mkuu bado anashabikia watu kuendelea kupigwa, Waziri hafai kuongoza wizara hii

 Rashid Abdallah: Prof Lipumba ni sawa na Kikwete, wote ni wenyeviti wa vyama halali, haiwezekani afanyiwe vitendo kama vile

Mbowe: Nasikitika sana kwa taarifa aliyoitoa Chikawe, tupo kama serikali ilivyo kudharau na kuchukua taarifa ya upande mmoja

Mbowe: tarehe 27, nilipokuwa na Prof Lipumba, askari polisi waliniambia kuwa taarifa hii ya kupiga walipewa kutoka juu. Sitawataja

 Mbowe: Mimi mwenyewe ni muhanga, nilishambuliwa na bomu, nikashambuliwa kwa Machine Gun na nikashambuliwa kwa bastola siku moja

Mbowe: Mnafurahi kwa kuwa hampigwi nyinyi, Rose Kamili alipigwa Iringa na watu wa CCM na Polisi mkafurahi, na sasa amekuwa kilema

Mbowe: Rose Kamili ameigharimu serikali zaidi ya milion 102 kwa matibabu nchini India, hamuoni hasara kwa taifa masikini kama hili
Spika Makinda: Hoja hii tunaijadili kwa dakika 3, namuita mchangiaji wa kwanza
Tundu Lissu: Kanuni zinasema tutumie dakika 15, haiwezekani waziri atumie dakika 30, na AG atumie 15 halafu sisi 3. Natumia 15
Spika Makinda: Haya basi tumieni dakika 10 na siyo 15, lakini tuzingatie tahadhari iliyotolewa na Mwanasheria Mkuu
Tundu Lissu: Huyu waziri wa mapolisi amesema uongo na hastahili kuwa katika nafasi kuanzia sasa
Tundu Lissu: Sasa tumejua kuwa ile kauli ya WAPIGWE TU ni kauli ya serikali na kauli ya CCM, jeshi la polisi ni la ma 'FACIST'
Tundu Lissu: Bunge lichukue hatua dhidi ya Polisi, waziri Mkuu, Waziri Chikawe, IGP naibu IGP. Tumechoka lazima wawajibike
Tundu Lissu: Tunahitaji tuunde tume teule kuchunguza matukio ya mapolisi kupigwa watu, tumechoka kupigwa
Tundu Lissu: Tukiendelea hivi na tunaelekea kwenye uchaguzi mkuu Oktoba, kumbukeni nyie ni wanachama wa mahakama ya Kimataifa ICC
Rashid Abdallah: Mauaji yanafanyika katika nchi hii, watu wanakufa, halafu jeshi la polisi lipo tu linaangalia
Rashid Abdallah: Waziri Mkuu bado anashabikia watu kuendelea kupigwa, Waziri hafai kuongoza wizara hii
Rashid Abdallah: Prof Lipumba ni sawa na Kikwete, wote ni wenyeviti wa vyama halali, haiwezekani afanyiwe vitendo kama vile
Mbowe: Nasikitika sana kwa taarifa aliyoitoa Chikawe, tupo kama serikali ilivyo kudharau na kuchukua taarifa ya upande mmoja
Mbowe: tarehe 27, nilipokuwa na Prof Lipumba, askari polisi waliniambia kuwa taarifa hii ya kupiga walipewa kutoka juu. Sitawataja
Mbowe: Mimi mwenyewe ni muhanga, nilishambuliwa na bomu, nikashambuliwa kwa Machine Gun na nikashambuliwa kwa bastola siku moja
Mbowe: Mnafurahi kwa kuwa hampigwi nyinyi, Rose Kamili alipigwa Iringa na watu wa CCM na Polisi mkafurahi, na sasa amekuwa kilema
Mbowe: Rose Kamili ameigharimu serikali zaidi ya milion 102 kwa matibabu nchini India, hamuoni hasara kwa taifa masikini kama hili

26 WAUAWA KIGAIDI NCHINI MISRI


Gari la kivita la Serikali nchini Misri 
Takriban watu 26 wameuawa katika mfululizo wa mashambulizi yaliyofanywa na kundi la wapiganaji la Islamic State Kaskazini mwa Misri katika eneo Sinai
Gari lililokuwa na mabomu lilipiga kituo cha kijeshi kaskazini mwa Sinai katika mji wa El-Arish na kuwaua wanajeshi kadhaa. Mashambulizi mengine kama hayo yalifanyika katika mji jirani Sheik Zuwayid na mji wa Rafah katika mpaka wa Gaza.
Kundi la wapiganaji la Ansar Beit al-Maqdis ambalo ni mshirika wa wapiganaji wa Islamic State wamekiri kutekeleza shambulio hilo.
Maafisa wa jeshi nchini Misri wanasema gari hilo lililokuwa na mabomu liliegeshwa nje ya ngome ya jeshi ya El-Arish na mashambulizi yake yalilenga hoteli ya jeshi na maeneo mengine mhimu katika kituo hicho.
Hata hivyo kundi hilo lilianza kutekeleza mashambulizi yake nchini Misri tangu kuangushwa kwa utawala wa Rais aliyekuwa na msimamo mkali wa Kiislam Mohammed Morsi mwaka 2013.
Hofu imetawala katika miji kadhaa nchini Misri wiki hii kutokana na sherehe za kumbukumbu za kuangushwa kwa utawala wa aliyekuwa Rais wa Taifa hilo na aliyeondolewa madarakani mwaka 2011 Hosni Mubarak.
Eneo la Kaskazini mwa mji wa Sinai kumekuwa na hofu ya mashambulizi ya kigaidi tangu mwezi Oktobar mwakajana ambapo wanajeshi kladhaa waliuawa katika shambulio.
Jeshi kwa muda mrefu limekuwa likitekeleza opereshen maalumu ili kudhibiti hali hiyo,japo kuwa inaonekana kushindwa kudhibiti hali hiyo.
Wapiganaji wa kundi la Ansar Beit al-Maqdis ni tishio kwa sasa nchini Misri kwani wamekuwa wakiandaa mashambulizi yanayolenga vituo vya kijeshi..
Wachambuzi wa mambo wanasema mashambulizi haya yanabainisha kuwepo kwa mikakati mikali inayopangwa na kundi hilo ambayo huenda vyombo vya usalama havijabaini mbinu zao.
Kundi hili la Ansar Beit al-Maqdis ambalo kuanzishwa kwake ilikuwa ni hamasa ya kundi la kigaidi la Al Qaeda,liliamua kubadili mtazamo wake na kuanza kutekeleza na kutii amri za kundi la wapiganaji wa Islamic state lililoshamiri Iraq na Syria,na malengo ya kundi hili ni kuhamasisha watu kuasi na kuuangusha utawala wa sasa wa Rais Misri Abdul Fattah al-Sisi.
Hata hivyo mtenda naye hutendwa kwani Rais Sisi ndiye kiongozi wa kijeshi aliongoza harakati za kuuangusha utawala wa Morsi kutoka Muslism Brotherhood lakini kwa sasa harakati za kumuangusha na yeye zinaendelea.
CHANZO BBC

AU; 'LAZIMA BOKO HARAM WASHINDWE VITA'


Viongozi barani Afrika wanafanya mazungumzo kuhusu hali ya Bara la Afrika
Mwenyekiti wa muungano wa Afrika, ametoa wito kwa mataifa ya Afrika kuchukua hatua madhubuti za kupambana na tisho la usalama linalotokana na kundi la Boko Haram.
Nkosazana Dlamini-Zuma ameambia kikao cha AU kinachoendelea nchini Ethiopia, kwamba unyama unatotendwa na kundi hilo sio tisho tu kwa Nigeria bali kwa bara zima.
Mkutano wa wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika umeanza leo nchini Ethiopia ambapo viongozi wa Afrika wanatarajiwa kujadili masuala muhimu yanayolikumba bara la Afrika kwa sasa.
Baadhi ya maswala yatakayopewa kipaombele kwenye mkutano huo ni tisho la usalama linalotokana na Boko Haram nchini Nigeria, pamoja na juhudi za kupambana dhidi ya ugonjwa hatari wa Ebola.
Licha ya kauli mbiu ya mkutano huo wa siku mbili kuwa swala la kuwawezesha wanawake, viongozi kutoka nchi 54 wanachama wa Muungano huo watalazimika kuangazia swala la migogoro ambalo limekuwa changamoto kubwa kwa bara la Afrika.
 Wapiganaji wa Boko Haram
Mwenyekiti wa muungano huo, Nkosazana Dlamini-Zuma amepigia debe swala la umoja katika kupambana na wapiganaji wa kiisilamu wanaoendelea kuteteresha amani katika bara hilo.
Mnamo siku ya Alhamisi, baraza la usalama na amani la AU, lilitoa wito wa haja ya kuwepo kikosi cha wanjeshi 7,500 kupelekwa katika maeneo yanayokumbwa na migogoro Afrika.
Wakati huo huo Kenya inatarajia kutuma ujumbe mzito kwenye mkutano huo kama mwanzo wa hatua yake ya kukata uhusiano na Mahakama ya jinai ICC.
Katika kikao kilichopita cha Umoja wa Afrika kilichokaa mjini Malabo Equatorial Guinea wajumbe walisaini mkataba wa uundwaji wa mahakama ya Afrika itakayoshughulikia kesi za Afrika badala ya kuzipeleka kwenye mahakama ya ICC, baadhi yao wakidai kuwa kesi za mahakama hiyo zinawalenga waafrika pekee.
CHANZO BBC

ALIYEKUWA KIONOZI WA MAKABURU AACHILIWA



Eugene Alexander de Kock
Kiongozi wa zamani wa utawala wa kiimla wa makaburu nchini Afrika Kusini na ambaye alikuwa kinara wa kuongoza kitengo hatari cha kuwatesa watu weusi, Eugene de Kock, amesamehewa, kuhurumiwa na kuondolewa gerezani.
Eugene Alexander de KOCK alikuwa akitumikia hukumu ya mauwaji na mateso kwa wakereketwa wengi wa chama cha ANC, lakini sasa waziri wa haki na sheria Nchini Afrika Kusini, Michael Masutha, amesema kuwa de Kock ameachiwa huru kwa manufaa ya umoja wa kitaifa.
Alikuwa ametubu mbele ya tume ya haki na maridhiano kwamba alikuwa amesababisha zaidi ya vifo vya watu mia moja na pia kuhusika katika vitendo vya kuwatesa watu kinyama na ufisadi, hasa akiwalenga waliokuwa wakipinga utawala wa ubaguzi wa rangi.
Kanali huyo wa zamani wa polisi aliyekuwa na mataji mengi mno alisamehewa kwa mengi ya makosa aliyofanya, lakini akazuiliwa gerezani kwa makosa dhidi ya binadamu kabla ya kufungwa jela maisha.
Tarehe ya kuachiwa huru kwake kwa sasa bado ni siri.
chanzobbc

Alhamisi, 29 Januari 2015

BABA AJIUAKUTOKANA NA PICHA ZA MWANAWE


Loredana Chivu ni mwanamitindo nchini Romania
Baba mmoja amejiua baada ya kuona picha za uchi zamwanawe wa kike katika jarida la Playboy nchini Romania.
Loredana Chivu alirarua ukurasa uliokuwa na picha yake akiwa 'amepos' katika jarida hilo la Playboy na punde babake alipogundua kuhusu picha hizo, alizongwa na mawazo na hata kumkana mwanawe.
Kwa mujibu wa mtandao wa Mirror, msichana huyo mwenye umbo la kuvutia alisema, '' babangu aliacha kuongea na mimi na kuonekana mwenye hasira sana''.
"alipogundua kuwa picha hizo zilikua zangu, alijitenga sana na kujaribu kunitenga na mimi''.
Nilidhani labda angesahau na sikudhani hata siku moja angejitoa uhai.
Loredana Chivu anasema anajuta sana kwani babake hakuwahi kuongea naye baada ya kupata picha zake
Mwanamitindo huyo Loredana Chivu mwenye mamia ya picha akiwa nusu uchi kwenye akaunti yake ya Instagram, alikuwa na uhusiano wa karibu sana na babake lakini alisema yote hayo yalibadilika baada ya babake kuona picha zake akiwa nusu uchi.
Alipokwenda kumtembelea babake miezi michache baadaye, baada ya kuamua kwamba kimya kilikuwa kimeendelea kwa muda mrefu sana, alishtuka sana kumpata babake akiwa amejitoa uhai
"nilipata akiwa na kamba shingoni akiwa ananing'inia chumbani''.
Loredana,anayeishi nchini Romania, anasema kuwa tangu kifo cha babake, amekuwa akiwaza na kuwazua kwamba aliamua kujiua kwa sababu ya mgogoro kati yetu na hasa kuhusu picha zangu zilizoziona kwenye jarida la Playboy.
''Najuta sana kwamba hakuwahi kupata muda wa kuzungumza na babangu kuhusu yaliyotokea''.
''Hakuwacha ujumbe wowote kabla ya kujitoa uhai, siku zote tulikuwa na uhusiano mzuri lakini yote yalibadilika baada ya baba kuona picha zangu nikiwa uchi. Bado inaniuma sana na singemtakia mtu yeyote kupatwa na kama yaliyonikuta''.
CHANZO BBC

NSHINDANO YA MAKALIO YAFANYIKA MAREKANI


Mwanamke mwenye makalio makubwa 
Ni swala la kushangaza kwamba shindano la kumtafuta mwanamke mwenye makalio makubwa mjini New York Marekani litatumiwa kama kigezo cha upasuaji wa mapambo ,huku sheria ya wanawake wanaoruhusiwa kushindana wakitakiwa kuwa ambao hawajafanyiwa upasuaji wowote wa mapambo.
Mwandalizi wa shindano hilo ni daktari Michael Jones ambaye anamiliki kampuni ya mapambo ya upasuaji ya Lexington.
Mbali na kandarasi hiyo ya kumodel mshindi atapata dola 2,000 fedha taslimu.
Gazeti la The New York post limeripoti kwamba wanawake 68 wanashiriki katika shindano hilo.
Wanaoshiriki ni pamoja na model warefu kutoka Washington na mkufunzi wa kibinafsi wa mchezaji densi Brenda Monks ,Chelsea Simone.
Ili kufuzu wanaotaka kushiriki waliulizwa ni kwa nini wanajivunia makalio yao?.
Mwanamke wa miaka 20 Derby Pucket alisema kwamba makalio yake makubwa yanatokana na mazoezi ,ulaji wa kuku,biskuti na chakula kinachompa mafuta mengi.
Mwishoni mwa siku,waliofika fainali walipunguzwa hadi kufika watu 13 ambao watatawazwa mwishoni mwa mwezi huu.
CHANZO BBC

WANAWAKE WAKERWA NA MAUJI MISRI


MAANDAMANO MISRI
Zaidi ya wanawake 100 wa Misri wameandamana mjini Cairo, kutaka uchunguzi ufanywe dhidi ya mauaji ya mkereketwa mmoja wa haki za kibinadamu, Shaimaa Sabbagh.
Mkereketwa huyo aliuwauwa wakati wa maadhimisho ya maandamano ya mapinduzi ya kiraia Nchini humo mnamo mwa 2011.
Wanawalaumu walinda usalama kwa kumpiga risasi mkereketwa huyo aliyekuwa na umri wa miaka 32 na ambaye hakuwa amejihami.
Mkereketwa huyo aliuuwawa mwishoni mwa juma lililopita.
Picha ya Shaimaa Sabbagh akifariki iliibua hasira kubwa nje na ndani ya Misri.
Kifo chake pia kiliibua ukosoaji mkubwa dhidi ya polisi na wakuu wa gazeti la serikali la, Al Ahram.
CHANZO BBC

RAIS KIIR ALAZWA HOSPITALINI ETHOPIA


 

 Rais Salva Kiir
Mkutano wa viongozi wa kikanda ulioandaliwa kujadili mgogoro wa mwaka mmoja unaotokota nchini Sudan Kusini, umecheleweshwa baada ya Rais Salva Kiir kuugua na kukimbizwa hospitalini mjini Addis Ababa, Ethiopia.
Afisa mmoja wa shirika la IGAD, ambalo linafanya juhudi za kuwakutanisha viongozi wa Sudan Kusini kwa lengo la kumaliza vita, aliambia BBC kwamba Rais Kiir, alianza kuvuja damu kutoka puani
Kabla ya kuugua, hapo jana Kiir alifanya mazungumzo na kiongozi wa waasi Riek Machar ambapo alimtaka kupuuzilia mbali maswala yanayochochea mgogoro huo ili kumaliza mgogoro huo ambao umedumu mwaka mmmoja
Viongozi wa kikanda, wanakutana baadaye leo, kushinikiza pande zote kufikia makubaliano ili kumaliza vita.
Swala kuu kwenye ajenda, ni kusuluhisha maswala yanayoleta kizungumkuti kuhusu serikali ya muungano kama moja ya suluhu la kupatikana amani.
Pande zote zinazozozana zimekosa kufikia makubaliano kuhusu wadhifa wa waziri mkuu na ikiwa anapaswa kuwa na mamlaka makuu au la.
Maelfu ya watu wamefariki na wengine zaidi ya milioni moja kuachwa bila makao tangu vita vya wenyewe kwa wenyewe kuzuka nchini humo Disemba mwaka 2013.
CHANZO BBC


JESHI LA DRC KUWAKABILI WAASI WA KIHUTU


Wanajeshi wa DRC
Mkuu wa majeshi katika jamhuri ya kidemokrasi ya Congo, ametangaza operesheni kali ya kikosi cha Congo kikishirikiana na Umoja wa mataifa dhidi ya kundi la wapiganaji wa waasi wa kihutu wa Rwanda.
Hii ni hatua iliyosubiriwa kwa muda tangu makataa ya mwisho kutolewa mnamo januari mbili mwaka huu na jumuiya ya kimataifa kwa waasi kusalimu amri na kurejesha silaha au mashambulio makali dhidi yake yaanzishwe.
Maafisa wa Umoja wa mataifa walioko DR Congo, wamesema kuwa operesheni hiyo bado haijaanza.
Jenerali Alberto Dos Santos Cruz, ameiambia BBC kuwa wanaandaa kila kitu tayari ndiposa waanze kuwakabili waasi.
Kwa mjibu wa jenerali Cruz, mianya yote ya kutorokea waasi hao imezibwa na wanajeshi wa Congo huku walinda usalama wa umoja wa mataifa wakitoa usaidizi wa silaha na vifaa vinginevyo.
Awali katika ushirikiano kama huo, umoja wa mataifa ulisaidia kutoa saada wa vifaa, kama vile ndege za kivita na usambazaji wa vyakula, ilihali jeshi la Congo likiwa katika mstari wa mbele katika kukabiliana na waasi.
 Waasi wa kihutu FDLR
Kundi hilo la Democratic Forces for the Liberation of Rwanda-DFLR linakisiwa kuwa na wanajeshi elfu moja mia tano waliotawanyika katika maeneo ya vijijini na kujumuika na raia, na itakuwa vigumu zaidi kukabiliana nalo kuliko lile kundi la M23.
Kundi ambalo jeshi la Congo likisaidiwa na walinda usalama wa umoja wa mataifa walipigana nao mwaka 2013.
Kundi la FDLR limesema kuwa halitajitetea katika vita hivyo, lakini linataka kujadiliana na serikali ya Rwanda mjini Kigali, inayolilaumu kwa kuhusika katika mauaji makubwa ya kimbari nchini Rwanda mwaka 1994.
CHANZO BBC

MSAFARA WA RAIS GOODLUCK WAPIGWA MAWE.


Rais Goodluck Jonathan amelaumiwa kwa kukosa kudhibiti kundi la Boko Haram
Msafara wa magari ya Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan umepigwa kwa mawe na watu wanaioishutumu serikali kwa kukosa kukomesha harakati za wapiganaji wa kiisilamu wa Boko Haram.
Madirisha ya magari kadhaa kwenye msafara huo yalivunjwa kwa mawe, kabla ya polisi kuwafyatulia gesi ya kutoa machozi watau hao huku wakiwacharaza kwa mijeledi.
Shambulizi hili limefanyika katika mji wa Yola Mashariki mwa Nigeria, ambako Rais Jonathan alikuwa anaendesha kampeni yake kabla ya uchaguzi mkuu mwezi ujao.
Maelfu ya wakimbizi wa ndani wanaishi mjini Yola baada ya kutoroka vita kutoka makwao ambako Boko Haram inaendesha harakati zake.
chanzo bbc

Jumatano, 28 Januari 2015

BALE AKANA KUJIUMGA NA MANCHESTER UNITED




Gareth Bale mchezaji wa Real Madrid ya Hispania 
Winga wa Real Madrid Gareth Bale amefutilia mbali uwezekano wa yeye kujiunga na klabu ya Manchester United kwa kusema haoni nafasi yake klabuni hapo na kwamba ana furaha kuendelea kuitumika timu yake ya sasa ya Real Madrid.
Kumekuwa na tetesi kuwa nyota huyo atajiunga na Manchester united huku kipa David De Gea akielekea Real Madrid kama sehemu ya mpango huo. "Siioni nafasi yangu katika timu hiyo, nafurahi kushinda mataji.Nataka kuendelea kufanya hivi nikiwa na Real Madrid."
Bale alijiunga na Real Madrid kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni 85 iliyovunja rekodi ya usajili mwezi septemba 2013.
Mchezaji huyo wa zamani wa Tottenham alilaumiwa na baadhi ya mashabiki wa Madrid kwa kumnyima pasi Cristiano Ronaldo kwenye michezo dhidi ya Espanyol.
Bale anasema "Napata sapoti nikiwa hapa Bernabeu. Nitaendelea kuonyesha nini naweza fanya katika uwanja na kuendelea kutwaa makombe". Sidhani kama nina tamaa uwanjani ninasaidia kufunga magoli na kufunga, ninacheza vile ninavyotakiwa kucheza, acha vyombo vya habari viseme watakavyo".
Akizungumzia uhusiano wake na Ronaldo nyota huyo wa kimataifa wa Wales, aliongeza "hakuna uadui kati yetu."
Bale amefunga mabao 36 na kusaidia kutoa pasi za mabao 26 katika michezo 72 aliyoichezea Real Madrid.
CHANZO BBC

AJIOA BAADA YA KUKOSA MCHUMMBANI



Yasmin Eleby 
Yasmin Eleby hakupata mchumba wa kumuoa mtu ambaye alitaka awe mume wake atakapofikisha miaka 40--kwa hivyo akafanya kitendo ambacho kimewashangaza wengi, aliamua kujioa mwenyewe.
Kwa mujibu wa mtandao wa MySanAntonio.com,Eleby aliahidi kwamba ikiwa hatapata mchumba wakati atakapokuwa ametimiza miaka 40, basi atafanya harusi ya mtu mmoja yaani atajioa ili kusherehekea miaka yake 40.
Duru zinasema kuwa mwanamke Eleby alifanya harusi yake mwenyewe katika makavazi ya Houston akiambatana na jamaa na familia yake na wageni wengine waalikwa.
Kwa sherehe hii, dadake Eleby ndiye aliendesha sherehe hio, kwani ni kinyume na sheria kwa mtu kujioa mwenyewe. Harusi ya kawaida ni kati ya watu wawili.
Katika picha za kanisani sherehe ilionekana kuwa ya kawaida bila ya mchumba.
Kulingana na John Guess Jr afisaa mkuu wa makavazi hayo, sherehe hiyo ilionekana kuwa bila tashwishi na kuonekana kama jambo la kawaida kwani makavazi hayo huwakumbatia watu wa jinsia mbali mbali kuendesha harusi zao hapo.
Aliposikia kwamba Eleby, ambaye anaishi na kufanya kazi ugenini alikuwa anapanga kujioa mwenyewe, aliharakisha kwenda katika eneo hilo kujionea mwenyewe.
"Eleby alipofikisha umri wa miaka 40 bila ya kupata mpenzi na mtu mwenye nia ya kumuoa, aliamua angejioa mwenyewe,''alisema Guess Jr ambaye anasema harusi hiyo imewashangaza wengi na kuwa gumzo katika mitandao ya kijamii.
Anasema anakubaliana na Eleby na mtazamo wake wa mapenzi kwamba mtu anaweza kujipenda na kujioa kwa kukosa wa kumuoa kwani cha muhimu ni mtu kujipenda kwanza kabla ya kupendwa.
"watu wengu huolewa bila ya kutafakari mara mbili kuhusu yule anayemuoa, '' Guess Jr alisema.
Anadhani kwamba pindi watu watakapomuona Eleby anavyojishughulikia mwenyewe, huenda akapata ushindani.
"ni mrembo, anafanya kazi kwa bidii na anasifika duniani na pia anaona uamuzi wake umewapa gumzo watu wengi. ''
CHANZO BBC

HEZBO;;AH LASHAMBULIWA JESHI LA ISRAEL


Wapiganaji wa Hezbollah
Kundi la wapiganaji wa Washia wa Lebanon walio chini ya vugu vugu la Hezbollah, linasema kuwa limetekeleza shambulio dhidi ya msafara wa wanajeshi wa Israeli katika mpaka wa mataifa hayo mawili.
Kwa upande wake, Jeshi la Israeli linasema wanajeshi wake wanne wamejeruhiwa pale kombora lililorushwa kwa kifaru kupiga gari lake la kijeshi karibu na mpaka wa Lebanon.
Taarifa nyingine kutoka kwa Hezbollah zinasema kuwa zaidi ya waisraeli 15 yamkini wameuwawa au kujeruhiwa.
Kundi la Hezbollah linasema kuwa lilikuwa likijibu mashambulio ya angani yaliyofanywa na Israeli yaliyomuua jenerali mmoja wa Iran na wapiganaji kadhaa wa Hezbollah Nchini Syria siku kumi zilizopita.
Israel ilijibu mashambulizi hayo kwa kurusha makombora Kusini mwa Lebanon
Waziri mkuu Benjamin Netanyahu alionya kwamba jeshi la Israel liko tayari kutumia nguvu dhidi ya mashambulizi yoyote kutoka kwa washambuliaji.
CHANZO BBC

KORTI YA KWANZA GOOGLE,YAHOO NA MICROSOFT

Mahakama kuu nchini India imeamrisha kampuni kubwa za internet, Google, Yahoo na Microsoft kubana matangazo ya biashara ya kuwapima wanawake wajawazito ili kubaini jinsia ya mtoto kabla ya kuzaliwa.
Matangazo kama hayo, ni kinyume na sheria nchini India kwa sababu kuna visa vingi vya wanawake kuavya mimba wanapogundua wana mtoto mwenye jinsia wasioitaka.
Hali hii imechochea tatizo la pengo katika jinsia moja kuwa ikilinganishwa na nyingine.
Mahakama ilikuwa inatoa uamuzi katika kesi iliyowasilishwa mbele yake kuhusu kuzagaa kwa matangazo ya biashara ya kubaini jinsia ya mtoto akiwa tumboni kwenye mitandao hio.
CHANZO BBC

AMNESTY YAKOSOA JESHI LA NIGERIA


Wakuu wa jeshi la Nigeria
Shirika la kimataifa la kutetea haki za binaadamu, Amnesty International, limelishutumu jeshi la Nigeria kwa kushindwa kuwalinda raia katika mji wa Baga uliopo kaskazini mashariki mwa Nigeria, licha ya kuwepo onyo kwamba wanamgambo wa Boko Haram wangelitekeleza shambulio.
Linanukuu duru ambayo haikutajwa jina aliyesema kwamba wanamgambo hao waliwaambia wakaazi miezi miwili awali kwamba walikuwa wanapanga shambulio.
Amnesty International linasema waanjeshi walitazama tu jinsi vikosi vya Boko Haram vilivyokuwa vikiongezeka. Inakadiriwa kwamba kati ya watu 150 hadi 2000 waliuawa katika shambulio hilo lililotokea mapema mwezi huu.
Shirika hilo linadai kwamba limeelezea wasiwasi wake mara kadhaa awali kwamba vikosi vya usalama haviwajibiki vya kutosha kuwalinda raia dhidi ya unyanyasaji na ukiukaji wa haki za binaadamu unaotekelezwa na Boko Haram.
Tangu mwaka 2009, Boko Haram limekuwa likiwalenga raia na kufanya uvamizi, kuwateka raia na mashambulio ya mabomu, huku mashambulio yao yakiongezeka kwa idadi na ukubwa. Malefu ya watu wameuawa katika mashambulio hayo, mamia kutekwa na maelfu wengine wameachwa bila makaazi baada ya kulazimika kutoweka mapigano.
CHANZO BBC

PROFESA LIPUMBA AFIKISHWA MAHAKAMANI

 Profesa Ibrahim Lipumba, kiongozi wa chama cha CUF nchini Tanzania akikabiliwa na mashitaka ya kuandamana bila kibali.
Kikao cha Bunge la Tanzania leo kimevurugika kutokana na vurugu za baadhi ya wabunge waliokuwa wakibishana kuhusu suala la kiongozi wa chama cha upinzani cha CUF, Profesa Ibrahim Lipumba kushambuliwa na polisi Jumanne kwa madai kuwa alihusika katika maandamano kinyume cha sheria.
Hoja iliamshwa na mbunge ambaye pia ni kiongozi wa upinzani aliyetaka suala hilo lijadiliwe kwa dharura. Hayo yametokea huku Profesa Lipumba akifikishwa mahakamani kusomewa mashtaka ya jinai.
Chanzo ni pale aliposimama James Mbatia mbunge wa kuteuliwa kutaka suala la polisi kumshambulia na kumdhalilisha Profesa Ibrahim Lipumba, kiongozi wa chama cha CUF lijadiliwe kwa dharura bungeni humo.
Licha ya jitahada za Spika Makinda kueleza kuwa suala hilo litajadiliwa kesho, kwa kuwa serikali inahitaji muda wa kuwasilisha majibu, mambo yakavurugika.
Huku wabunge wakiwa wamesimama wima wakishinikiza hoja hiyo ijadiliwe, Spika Makinda aliendelea na msimamo wake wa kutaka hoja ijadiliwe Alhamisi baada ya serikali kuwasilisha majibu, hapo ndipo mkorogano ulipozidi na kuleta kutoelewana kati ya wabunge wa upinzani na Spika.
Spika Makinda alilazimika kuahirisha kikao hicho mpaka jioni baada ya hali kuwa ngumu, na hata jioni likaahirishwa tena mpaka kesho, Alhamisi.
Kiongozi huyo wa upinzani inadaiwa alifika eneo ambako maandamano yaliyopangwa kufanyika Jumanne yalikuwa yamepigwa marufuku, ingawa uongozi wa chama cha CUF unadai Profesa Lipumba alikusudia kuwashawishi wafuasi wake watawanyike kutii amri ya polisi ndipo akashambuliwa.
Wakati huo huo Profesa Lipumba amefikishwa mahakamani mjini Dar Es Salaam ambako amesomewa mashtaka ya kufanya maandamano bila kuwa na kibali.
Hata hivyo kwa muda Profesa Lipumba alikimbizwa hospitalini baada ya afya yake kudhoofika, ikidaiwa ni sababu ya kupigwa na polisi, madai ambayo BBC haijaweza kuyathibitisha.
Hata hivyo alirejeshwa mahakamani baada ya kupata nafuu, na kesi yake imeahirishwa na itatajwa tena mahakamani tarehe 26 Februari 2015.
Ameachiwa kwa dhamana ya watu wawili kwa kiasi cha shilingi milioni mbili kila mmoja.


Jumatatu, 26 Januari 2015

KASISI WA KWANZA MWANAMKE AAPISHWA UK


Libby Lane kuwa kasisi wa kwanza mwanamke 
Kanisa moja nchini Uingereza hii leo limemuapisha mwanamke wa kwanza kuwa kasisi.
Mchungaji Libby Lane kama anavyojulikana sasa atakuwa kasisi wa Stockport katika sherehe iliofanyika katika eneo la York Minster,ikiwa ni miezi sita tu baada ya kanisa hilo kumpigia kura ili kumaliza utamaduni wake wa wanaume kuwa makasisi.
Kasisi huyo amesema kuwa iwapo uchaguzi wake utawafanya wanawake kubaini uwezo wao basi anafurahia.
Hatua hiyo imeendelea kuzua hisia tofauti miongoni mwa wafuasi wa kanisa hilo la kianglikana duniani.
CHANZO BBC

ONGWEN KUFIKISHWA KATIKA NAHAKAMA YA ICC


ongwen icc
Kiongozi mmoja wa kundi la waasi nchini Uganda, Dominic Ongwen, amekuwa mwanachama wa kwanza wa kundi la Lord's Resistance Army LRA, kufika mbele ya mahakama ya kimataifa ya ICC.
Wakati wa kusikizwa kwa kesi yake huko The Hague, Bwana Ongwen alithibitisha kuwa ndiye, huku akijieleza kuwa ni mwanajeshi wa zamani wa LRA.
 Mahakama ya Icc
Anakabiliwa na makosa ya uhalifu dhidi ya binadamu na makosa mengine ya kivita, ikiwemo mauwaji na utumwa.
Awali mwezi huu alikuwa amezuiliwa nchini Afrika ya kati, miaka kumi tangu ICC ilipotoa ilani ya kumkamata.
chanzo bbc

Jumapili, 25 Januari 2015

EQUATORIAL GUNIEA NA CONGO ZA SONGA MBELE


Equatoria Gunea siku ilipopambana na Senegal katika Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika
Wenyeji Equitoria Guinea na Congo Brazaville zimekuwa timu za kwanza kusonga mbele katika hatua ya robo fainali kutoka kundi A ya Michuano ya Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika baada timu hizo shindi mechi zao hapo jana usiku.
Equitoria Guinea iliwaadhibu wapinzani wao Gabon kwa jumla ya magoli 2 bila majibu, huku Congo Brazaville nayo ikiwashushia kipigo Burkina Faso cha magoli mawili kwa moja.
Wenyeji Equitorial Guinea waliandika bao la kwanza katika dakika ya 55 kipindi cha pili kwa mkwaju wa penalti baada ya Lloyd Palun kufanyiwa faulo katika eneo la hatari.
Kama hiyo hatoshi Wenyeji hao wakapigilia msumari wa moto kwenye kidonda pale waliondika bao la pili kupitia Salvador Iban ambaye aliukwamisha mpira wavuni uliotemwa na mlinda mlango wa Gabon.
Nayo Congo Brazavile ambayo ilihitaji sare ya aina yoyote ili isonge mbelehatua ya robo fainali ilipata goli lake la kwanza kupitia kwa mchezaji Thierry Bifouma huku goli la pili likifungwa na Fabrice Ondama.
Goli pekee la Burkina Faso lilitiwa wavuni na Aristide Bance.
Kwa matokeo hayo Congo Brazaville inaingia hatua ya robo fainali kwa mara ya kwanza ya michuano hiyo mikubwa barani Afrika kwa mara kwanza tangu mwaka 1992.
Leo kutakuwa na mechi mbili za kundi B ambapo timu mbili kutoka ukanda wa Afrika Mashariki na kati Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Zambia zitatupa karata zao za mwisho ambapo Jamuhuri Kidemokrasia ya Kongo itaumana vikali na Tunisia huku Zambia ikikutana uso kwa uso na Cape Verde.
Zambia na Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo lazima zishinde mechi zao leo ili ziweze kusonga mbele hatua robo fainali huku Zambia ikihitaji ushindi wa magoli zaidi ya matatu kwa bila.
CHANZO BBC

ANDY MURRAY AMBWAGA GRIGOR DIMITROV


Andy Murray
Mcheza Tennis maarufu Andy Murray amembwaga Grigor Dimitrov katika kusaka kibali cha kushiriki mashindano ya wazi ya mchezo wa Tennis ya Australia.
Mshindi huyo wa mchezo wa Tennis Uingereza Murry aliibuka mshindi baada ya kujipatia pointi 6-4 6-7 (5-7) 6-3 7-5 ndani ya saa tatu na dakika 32.
Katika seti ya tano ya mchezo huo dalili za ushindin wa Murray zilianza kuonekana na kisha ushindi huo kudhihirika wazi katika michezo mitano ya mwisho.
Kwa ushindi huo sasa Andy Murray anatarajiwa kukwaana na raia wa Austaralia Nick Kyrgios katika mzunguko wake wa nane.
Murray atakuwa akicheka robo fainal ya 16 katika mashindano Grand Slam ikiwa ndiyo hatua ambayo alimtoa Dimitrov katika michuano ya Wimbledon mwakajana.
CHANZO BBC

KAMANDA WA LRA KUPANDISHWA KIZIMBANI ICC




Dominic Ogwen 
Kamanda wa ngazi ya juu wa kundi la waasi la Lord resistance Army,Dominic Ong'wen atafikishwa katika mahakama ya kimataifa ya ICC mjini the hague nchini uholanzi. atakabiliwa na mashtaka ya uhalifu wa kivita.
Ong'wen ni kiongozi wa juu wakwanza kutoka katika kundi la waasi la Uganda, LRA kufikishwa mahakamani baada ya miongo miwili ya mapigano dhidi ya Serikali ya Uganda.
Mahakama ya ICC imesifu hatua hii ikisema kuwa ni hatua yenye kuelekea kumaliza visa vya kigaidi vinavyotekelezwa na LRA
CHANZO BBC

OBAMA ALAANI MAUJI YA MATEKA WA JAPAN


Japan Hostages
Rais wa Marekani Barack Obama amelaani kile alichokitaja kuwa mauaji ya kikatili ya mmoja wa raia wa Japan aliyekuwa akishikiliwa mateka na wanamgambo wa Islamic State Haruna Yukawa.
Rais Obama pia alitaka mateka mwingine anayeshikiliwa na wanamgambo hao mwandishi wa habari Kenji Goto kuachiliwa mara moja
Kwa njia ya video Goto alionekana kwenye mitandao akishika mkononi picha ya maiti ya bwan Yukawa.
Mapema wataalamu mjini Tokyo na Marekani walisema kuwa wanatathmini ukweli wa picha hiyo.
Waziri mkuu nchini Japan Shinzo Abe alisema kuwa ameghadhabishwa na video hiyo.
CHANZO BBC

18,WAUAWA MISRI.


Waandamanaji Misri
Serikali ya Misri imesema watu kumi na wanane akiwemo Polisi mmoja wameuawa wakati wa maandamano yaliyofanyika nchini humo wakati wakiadhimisha miaka minne tangu kuangushwa utawala wa Hosni Mubarak.
Vifo hivyo vimetokea mjini Alexandria na cairo,Serikali ilipiga marufuku kuadhimisha kumbukumbu hizo hali iliyosabbaisha vurugu kati ya Waandamanaji na Polisi.
Zaidi ya watu 400 pia wanashikiliwa kutokana vurugu hizo.Hata hivyo serikali ilipiga marufuku tukio hilo linalodaiwa kuwa ni la kumbukumbu ya maandamano 2011.
Maandamano hayo ya mwaka 2011 nchini Misri yalikuwa yakiratibiwa na makundi ya Waislam wenye msimamo mkali ambapo vikosi vya usalama vilishindwa kuwadhibiti waandamanaji hao
CHANZO BBC

EBOLA NI FUNZO KUBWA KWA WHO DUNIANI


Mkurugenzi mkuu wa WHO, Margaret Chan


Mkuu wa Shirika la Afya Duniani, WHO, ameeleza mpango wa kuliimarisha shirika hilo baada ya malalamiko mengi kuhusu namna WHO ilivyoshughulikia mripuko wa Ebola Afrika Magharibi, ambayo imeuwa watu zaidi ya 8,000.

Margaret Chan alielezea mripuko huo kuwa maafa ambayo ni funzo kubwa kwa ulimwengu na WHO.
Katika kikao cha viongozi wa WHO mjini Geneva, Bibi Chan alisema mbinu za kupambana na misukosuko kama hiyo zinafaa kuimarishwa na kuanzishwe mfuko wa kugharimia hali ya dharura.
Alisema maafa ya Ebola yameonesha piya kwamba mfumo mwema wa afya wa taifa ni kitu cha lazima, siyo anasa.
CHANZO BBC

DRC;KIPENGELE CHA UTATA CHATOKA

Maandamano ya KInshasa ya jula lilopita
Bunge la wawakilishi la Jamhuri ya Demokrasi ya Congo limepitisha mswada uliorekibishwa kuhusu uchaguzi, baada ya kuondoa kipengee kilicholeta utata, na ambacho upinzani unasema kingerefusha awamu ya uongozi wa Rais Kabila.
Mswada ulivyopitishwa awali juma lilopita ulizusha maandamano ya siku kadha.
Mashirika ya kutetea haki za kibinaadamu yanasema watu 40 walikufa katika maandamano hayo.
Mswada wa awali ulitaka kufanywe sensa kabla ya uchaguzi wa rais - upinzani uliona kuwa hiyo itachelewesha uchaguzi wa rais ambao umepangwa kufanywa mwaka ujao.
CHANZOBBC

SYRIZA YASHINDA UCHAGUZI,UBELGIJI


Alexis Tsipras,kiongozi wa chama cha Syriza
Chama cha mrengo wa kushoto cha Syriza ambacho kimekuwa kikipinga hatua ya kubana matumizi kimeshinda katika uchaguzi uliofanyika nchini humo,japo kuwa hakuna uhakika kama kina viti vya kutosha Bungeni kuweza kuongoza serikali. Kiongozi wa chama cha Alexis Tsipras amewaambia wafuasi wake kaytakia mji mkuu Anthens kuwa hatua ya kubana matumizi iliyotangazwa na serikali inayoondoka imefikia mwisho na watafanya kazi na wakopeshaji na kukubaliana namna ya kushughulikia madeni ya taifa. Waziri mkuu anayeondoka madarakani Antonis Samaras amemtaka kiongozi wa chama cha Syriza Alexis Tsipras kumpongeza. Samaras anadai kuwa sera zake zilisaidia kufufua uchumi wa Ugiriki na kwamba walichukua hatua kudumisha hali ya usalama wa raia. Amesema kuwa anakabidhi nchi ambayo ni mwanachama wa umoja wa Ulaya na sarafu ya euro.
chanzo bbc

Jumamosi, 24 Januari 2015

TUNADUMISHA MILA KWA KULETA KISASA.KAMA WAUTA SHISHA VILE


ALIKAIDI WAZAZILAKINI SASA ANAJUTA

 
Je unakumbuka kisa cha wapenzi wawili waliozua gumzo nchini Kenya?
Msichana mhindi Sarika Patel kutoka familia tajiri na Timothy Khamala mbukusu kutoka familia maskini kutoka Magharibi mwa Kenya kuoana? wakati yao mapenzi yao yalijulikana kama Bukusu Darling, sifa kwa wanakoishi wawili hao.
Taarifa sasa ni kwamba mapenzi yao yamefika kikomo. Familia ya msichana Sarika ililaani sana mapenzi hayo kwani Timothy alikuwa anafanya kazi kwao kama mfanyakazi wa nyumbani.
Na Sarika alipoamua kwenda kuishi na Timothy kama mume na mke familia yake ilimfukuza na kisha kumfuta kazi Timothy.
Wawili hao walioana kinyume na matakwa ya familia ya Sarika ambayo kwao ilikuwa ni kama aibu kubwa sana kwa mtoto wao kutoka familia tajiri kuolea na kijana asiyekuwa na mbele wala nyuma.
Wakati taarifa ya wawili hao ilipogonga vichwa vya habari nchini Kenya, Sarika na mume wake walipata kazi katika kiwanda cha kutengeza Sukari kutoka kwa wahisani.
Lakini sasa kuna madai kwamba ndoa yao imevunjika baada ya Sarika kulalamika kwamba Timothy amekuwa akimdhulumu na kumtusi kila mara hali iliyosababisha wawili hao kutalakiana.
Mtandao wa Standard Digital umemnukuu Sarika akisema: "nilipokuwa mgonjwa , hakuwa hata na muda wa kunipeleka hospitalini badala yake wazazi wake ndio walionipeleka kutafuta matibabu. Mbali na hayo amekuwa akinichapa, '' alisema Sarika huku akibubujikwa na machozi.
Kwa sasa inaarifiwa anajuta sana kwa nini alikaidi amri ya wazazi wake.
''Ninajuta sana kwa nini sikuwasikiliza wazazi wangu na kuolewa kinyume na mapenzi yao. Ninaomba radhi, natumai watanikubali kurejea nyumbani. ''
Sarika ambaye ni mtoto wa nne katika familia ya watoto watano, ameamua kurejea nyumbani na kusema kamwe hatawahi kuwa na uhusiano wa kimepenzi tena. Lakini wazazi wake wamempa masharti, mwanzo aishi na rafiki yake huku akifanya uamuzi wa mwisho kuhusu anakotaka kuishi.
Anasema anahofia kwamba jamii ya wahindi haitamkubali tena kwani hakuwasikiliza wakati walipomshauri kutoolewa na mwanamume mwafrika.
CHANZO BBC


THE EASAFERICAN LAPIGWA MARUFUKU





Serikali ya Tanzania imepiga marufuku kuchapishwa na kusambazwa kwa gazeti la kila wiki la The EastAfrican kwa madai ya kuwa halijasajiliwa nchini humo.
Hata hivyo Wilfred Kiboro, mwenyekiti wa kampuni ya Nation Media Group, wachapishaji wa gazeti hilo la lugha ya kiingereza, ameeleza kuwa adhabu hiyo haikutarajiwa na wala haistahili na kubainisha kuwa wamekuwa wakisambaza gazeti hilo Tanzania kwa miaka 20 bila matatizo.
Kampuni ya Nation imedai sababu kubwa huenda ni serikali ya Tanzania kutofurahishwa na msimamo wake wa kuandika habari dhidi ya maovu kama rushwa na kero nyingine nchini Tanzania.
Kampuni hiyo imesema serikali ya Tanzania imetaja kutofurahishwa na kibonzo kilichochapishwa katika toleo la wiki hii, ambapo imesema kimemdhalilisha Rais Jakaya Kikwete.
Hata hivyo BBC haikuweza kumpata afisa wa serikali ya nchi hiyo anayehusika na usajili wa magazeti kuweza kutoa maelezo zaidi.

GOODLUCK JONATHANAFIKA MAIDUGURI TENA


 Wakimbizi mjini MaiduguriRais wa Nigeria, Goodluck Jonathan, anafanya kampeni za uchaguzi katika mji wa kaskazini-mashariki mwa nchi wa Maiduguri.

Mji huo uko kati ya jimbo lilokumbwa na mashambulio mengi kabisa ya wapiganaji Waislamu, Boko Haram.
Ulinzi mkali umewekwa katika eneo la uwanja wa michezo ambako anahutubia wafuasi.
Kabla ya ziara ya rais, Boko Haram walishambulia kijiji nje ya Maiduguri na kuuwa watu kama 15.
Wadadisi wanamshutumu rais kuwa ameshindwa kuwalinda raia dhidi ya Boko Haram ambao wanadhibiti eneo kubwa la kaskazini-mashariki mwa Nigeria.
CHANZO BBC

WAZIRI WA MADINI AJIUZULU




Waziri wa nishati na madini nchini Tanzania Sospeter Muhongo amejiuzulu 
Waziri wa nishati na madini nchini Tanzania Profesa Sospeter Muhongo amejiuzulu,na kumfanya kuwa afisa wa tatu wa ngazi za juu serikalini kuathiriwa na ufisadi uliokumba sekta ya kawi katika taifa hilo la Afrika mashariki.
Professa Muhongo alitoa tanagazo hilo wakati wa mkutano na vyombo vya habari.
Kujiuzulu kwake kunajiri baada ya kufutwa kazi kwa waziri wa Ardhi na kujiuzulu kwa mwanasheria mkuu ,wote wakiwa wamehusishwa na kutolewa kwa zaidi ya dola milioni 120 kutoka kwa benki kuu ya taifa hilo kupitia mazingira ya kutatanisha.

RAIS KIKWETE ATEUA MAWAZIRI 8


Rais Jakaya Kikwete
Rais Jakaya kikwete wa Tanzania ametangaza mabadiliko katika baraza lake la mawaziri.
Rais amewateua mawaziri wanane wapya pamoja na manaibu watano.
Tangazo hilo lilifanywa na katibu katika ikulu ya rais balozi Ombeni Sefue.
Mabadiliko hayo yanajumuisha wadhfa wa waziri wa nishati na kawi wa Profesa Muhongo ambaye amejiuzulu mapema leo pamoja na wadhfa wa waziri wa ardhi ambao uliwachwa wazi baada ya kupigwa kalamu kwa Anna Tibaijuka.
Mawaziri hao wawili wanahusishwa na kashfa ya ufisadi ambayo ilimshinikiza mwanasheria mkuu pia kujiuzulu.Nafasi ya Profesa Muhongo imechukuliwa na aliyekuwa naibu wa waziri wa ardhi, George Simbachawene
Rais Kikwete amewaapisha mawaziri hao wapya hii leo katika tangazo lililorushwa hewani na runinga ya taifa moja kwa moja.
Hii ndio orodha ya mawaziri walioteuliwa
MAWAZIRI
George Simachawene waziri wa nishati na madini
Mary Nagu- waziri wa nchi [afisi ya rais] mahusiano na uratibu
Christopher chiza -waziri uwezeshaji na uwekezaji
Harisson Mwakyembe[waziri wa ushirikiano wa afrika mashariki]
William Lukuvi -waziri wa ardhi nyumba na makaazi
Steven Wasira -waziri wa kilimo chakula na ushirika
Samwel Sita -waziri wa uchukuzi
Jenista Muhagama -waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera uratibu na bunge
MANAIBU WAZIRI
Stephen Masele -naibu waziri afisi ya makamu wa rais muungano
Angela Kariuki -naibu waziri wa ardhi nyumba na makaazi
Ummi Mwalimu- naibu waziri wa katiba na sheria
Anna Kilango naibu waziri wa elimu na mafunzo ya kiufundi
Charles Mwijage-naibu waziri wa nishati na madini

Ijumaa, 23 Januari 2015

NI SHANGWE BAADA YA VURUGU DRC.


Mashirika ya kutetea haki za binadamu yanasema kwamba watu 40 wamefariki katika vurugu ingawa serikali imekanusha hilo
Wanaharakati wa upinzani nchini DRC, wanasherehekea kwa kile wanachosema ni ushindi baada ya baraza la Senate kupiga kura kurekebisha mswada uliosababisha vurugu na maandamano kwa siku nne.
Baraza hilo la Senate lilipiga kura kurekebisha mswada huo tatanishi uliopendekeza sheria za uchaguzi kufanyiwa mabadiliko. Limefuta kipengee kinachohitaji kufanyika kwa sensa kote nchini kabla ya uchaguzi kufanyika mwaka ujao.
Mswada huo ndio uliozua vurugu na ghasia katika Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo kwa wiki moja.
Mabadiliko hayo sasa yanafuta kipengee ambacho kingechelewesha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi ujao.
Wapinzani wa Rais Joseph Kabaila wanasema hii ni njama ya Rais kufanya mageuzi ya kikatiba hali ambayo itampa fursa Kabila kusaialia madarakani kwa muhula mwingine.
Kura ya mwisho kuhusu mswada huo itafanyika wiki ijayo katika bunge la waakilishi na baraza hilo la Senate.
Huduma ya internet sasa imerejeshwa nchini humo, katika juhudi za serikali kusitisha vurugu ingawa mitandao ya kijamii bado imevurugwa ili kutatiza mawasiliano.
Mashirika ya kutetea haki za binadamu yanasema zaidi ya watu 40 waliuawa katika vurugu hizo ingawa serikali imepinga madai hayo.
Mkuu wa baraza hilo alitaja uamuzi huo kama wa kihistoria na kusema kuwa masenta walisikiliza kilio cha wengi.
chanzo bbc

Alhamisi, 22 Januari 2015

ISIWE SHIDA NAENDA LALA HIVIHIVI....KARIBU KWETU DODOMA


EBOLA;MASHABIKI WATAKIWA UWA NA SUBRA






Kolo Toure
Mlinzi wa Ivory Coast Kolo Toure amewataka mashabiki katika michuano ya mataifa ya Afrika nchini Equitorial Guinea kuwa na Subra wanapokaguliwa ugonjwa wa Ebola.
Mashabiki na maafisa wa polisi wamekuwa wakikabiliana kabla ya mechi kadhaa baada ya kucheleweshwa kutokana na upimaji wa Ebola nje ya viwanja vya soka.
''Nadhani mashabiki wanafaa kujua kwamba ni lazima wakaguliwa'' alisema mchezaji huyo wa liverpool.
 Maafisa wa afya wakiwakagua mashabiki katika michuano ya Afcon
''Ebola ipo na watu wengi huwa hawaamini wanapofika katika maeneo ambayo hayana watu walioambukiwa''.aliongezea.
Wafanyikazi wa Shirika la afya duniani WHO,ambao wanafanya ukaguzi huo wa Ebola wanakutana alhamisi ili kujadiliana kuhusu wasiwasi wa usalama wao baada ya kukabiliana na mashabiki wengine nchini humo.
CHANZO BBC

CAPE VERDE KUMENYANA NA CONGO DRC



Afcon
Mkufunzi wa timu ya Cape Verde Rui Aguas amebaini kwamba atafanya mabadiliko katika mechi dhidi ya Congo DRC lakini akongezea kwamba ameamua kuweka siri mbinu atakayotumia.
Huku akikiri kwamba baadhi ya wachezaji wake wana majeraha amesema hatasema ni wachezaji gani.
Naye mshambuliaji wa DRC Congo Yannick Bolassie ambaye ndiye mfungaji wa bao lililosabbisha sare ya 1-1 dhidi ya Zambia anasema wataibuka washindi.
CHANZO BBC
Amesema: Cape Verde ina wachezaji wazuri lakini tunataka kusonga mbele katika kundi hili halafu chochote chaweza kutokea''

ARSENAL YAFANYA MAZUNGUMZO NA PAULISTA.


Paulista kushoto 
Mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger amesema kuwa kilabu yake imeanza mazungumzo na mlinzi wa wa Villareal Gabriel Paulista.
''Mazungumzo yanaendelea vyema''alisema.
''Hatahivyo sijuia kama tutaafikia makubaliano,lakini tuna fursa ya mafanikio''.
The Gunners italazimika kumtafutia cheti za kufanyia kazi mchezaji huyo wa Brazil mwenye umri wa miaka 24.
Arsenal imemsajili Krystian Bielik kutoka kilabu ya Legia warsaw kwa kitita cha pauni 2.4 wiki hii.
Wenger alisema kuwa Bielik ambaye anaweza kucheza katika safu ya kati atatumiwa kama kiungo wa kati wa ulinzi.
CHANZO BBC

TANZANIA NA MABADILIKO YA TABIA YA NCHI


Mazao ya samaki
Mabadiliko ya hali ya hewa yamekuwa yakileta madhara duniani ,nchini Tanzanian mamlaka ya hali ya hewa imelazimika kutoa taarifa maalumu kwa umma kuhusiana na tahadhali ya mabadiliko ya hali hewa katika ukanda wa Pwani kutokana na kuimarika kwa mgandamizo mdogo wa hewa katika eneo la Bahari ya hindi mashariki mwa kisiwa cha Madagascar hali inayoleta mawimbi makali.
Shughuli ya uvuvi katika bahari ya Hindi ni tegemeo kwa uchumi na huduma ya samaki,lakini kwa sasa mambo yamebadilika samaki wanapatikana kwa tabu kufuatia wavuvi kuogopa kuingia Baharini kuvua,huku hali ya usafiri kwa vyombo vya majini ndani ya Bahari hiyo vikikumbwa na hali mbaya kutokana na mawimbi makali.
Hali hiyo ya kuchafuka kwa bahari na hali ya hewa, pamoja na mawimbi makali bahari ya Hindi, ni kilio kikubwa kwa wavuvi wa mwambao huo wanaoendesha maisha yao kwa kutegemea uvuvi, kwani kwa sasa samaki hawapatikani tena kama hapo awali.
 Hali ya mabadiliko ya tabia nchi, kwa mwaka huu wa 2015 limekuwa si jambo la kawaida, kwani kwa kawaida nchini Tanzaia majira kama haya ya mwezi wa kwanza mpaka wa pili katikati upepo hukata na kuwapa fursa wavuvi kutafuta riziki zao.
Kutokana na mabadiliko hayo ya hali ya hewa,imeathiri upatikanaji wa mazao ya samaki na sasa bidhaa ya samaki imepanda bei kutoka elfu kumi ama ishirini kwa ndoo ya lita kumi hapo awali sasa inauzwa kwa elfu sabini kwa dagaa mchele, na hivyo kumfanya mjasiriamali mwenye kipato cha chini kutomudu kununua bidhaa hiyo.
CHANZO BBC

WHATSAPP YAWABANA WATUMIAJI


Mtandao wa WjhatsApp
Mtandao wa kijamii wa WhatsApp unawabana watu wanaotumia huduma hio kupitia programu bandia na ambayo haijaidhinishwa ya Android kwa muda wa saa 24.
WhatsApp ambayo inamilikiwa na Facebook, ilisema kuwa imechukua hatua dhidi ya watumiaji wa huduma ya WhatsApp Plus kwa sababu ya wasiwasi kwamba programu hiiyo huenda iksababisha kuvuja kwa taarifa za siri za watumiaji wa WhatsApp.
Programu hio bandia na isio rasmi ya Android inawezesha watumiaji wa WhatsApp Plus kupamba mawasiliano yao wanavyotaka.
Wataalamu wanasema kwamba watumiaji wa Android wanapaswa kuwa makini na kutahadhari kuhusu wanavyodownload programu flani au 'Apps'.
Mtandao wa WhatsApp ulisema hivi karibuni kwamba ina watumiaji milioni 700 wanaotuma ujumbe bilioni 30 kila siku. Kwa sasa inatoza dola 0.99 kwa watumiaji wake wanaotumia huduma ya WhatsApp Plus kila mwaka.
''Lengo letu ni kuhakikisha kwamba huduma ya WhatsApp ni ya kasi kwa wanaoitumia, hilo ndio jambo muhimu sana kwetu,'' alisema msemaji wa kampuni hio.
''Watu wengine wamebuni progarmu ambazo bado hazijaidhinishwa na sasa wanazitumia na WhatsApp , kitu ambacho kinaweza kusababisha kupotea kwa ujumbe au baadhi ya taarifa kuvujishwa. ''
''Bila shaka jambo hili linakwenda kinyume na malengo yetu ya kutoa huduma kwa wateja wetu. Kuanzia leo tutaanza kuchukua hatua kali dhidi ya wanaotumia programu ambazo hazijaithinishwa ili kuweza kutumia programu zetu na pia kuwatahadharisha wanaozitumia programu hizo''.
Kulingana na moja ya maduka ya kuuza programu za kwenye mitandao, programu ya WhatsApp Plus yenyewe ilikuwa imekuwa dowloaded mara milioni 35
CHANZO BBC

WATOTO WA HOSNI MUBARAK KUACHILIWA


aliyekuwa rais wa Misri Hosni Mubarak na wanawe Alaa na Gamal wakiwa kizimbani
Mahakama nchini Misri imeamrisha kuachiliwa kwa watoto wa kiume wa rais wa zamani Hosni mubarak wakati wanaposubiri kesi yao pamoja na baba yao inayohusu ufisadi.
Wakili wa Alaa na Gamal Mubarak anasema kwa anatarajia wawili hao kuachiliwa leo.
Hasira kutokana na kile kilichoonekana kama jitihada za kumuandaa Gamal Mubarak kuweza kumrithi babake kama rais ni moja ya sababu zilizosababisha maandamano makubwa yaliyomundoa madarakani rais Hosni Mubarak.
CHANZO BBC