Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumamosi, 31 Januari 2015

MPINZANI WA OBAMA 2012 AJIONDOA



Mitt Romney aliyeshindwa na Obama uchaguzi wa 2012
Mitt Romney, mgombea wa chama cha Republican aliyeshindwa na rais Obama katika uchaguzi wa mwaka 2012 ameamua kutowania tena wadhfa huo.
Bwana Romney mwenye umri wa miaka 67 amesema kuwa ameamua ni muhimu kuwapatia viongozi wengine katika chama hicho fursa ya kuchaguliwa kama wagombea.
Taarifa yake inajiri wiki kadhaa baada ya tangazo lake kwamba atawania kwa mara nyengine.
Hatua yake ya kutowania inawapa fursa wafadhili kuwaunga mkono wagombea wengine.
Aliyekuwa Gavana wa jimbo la Florida Jeb Bush ,gavana wa new Jerzy Chris Christie na seneta Rand Paul ni miongoni mwa wale wanaowania kuingia ikulu ya whitehouse.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni