Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumanne, 20 Januari 2015

TIGER WOODS APOTEZA JINO UWANJANI


Tiger Woods baada ya ajali ya kamera. 

Tiger wood amepoteza jino lake la mbele juu baada ya kugongwa na kamera wakati akimtazama mpenzi wake Lindsey Vonn akinyakua kikombe cha ushindi
Nguli huyo wa zamani wa mchezo wa gofu, aliamua kwenda katika michuano ya kuteleza kwenye barafu ili kumshangaza Vonn mpenziwe ambaye alikuwa hamtarajii kumwona akichuana Cortina d’Ampezzo huko Italia.
Baada ya kuisha kwa michuano hiyo ya kuteleza barafuni, watu wakiwemo wandishi wa habari wakajisogeza karibu na mimbari ya kutolea tuzo ili kutaka kupata picha nzuri ya Woods.
Hata hivyo kulikuwa na msukumano mwandishi mmoja akisukumwa na mwenziwe kiasi cha kuteleza kutoka jukwaani na kamera kumtoka na kumgonga Tiger Woods mdomoni,na wakala ya nguli huyo wa zamani wa mchezo wa golfu alieleza hali hiyo kuwa aligongwa kwa bahati mbaya
chanzo bbc

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni