Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumamosi, 17 Januari 2015

MECHI ZA KOMBE LA AFRIKA KUANZA LEO


Kinyanganyiroi cha kombe la Afrika kuanza leo nchini Equitorial Guinea
Timu kutoka kote Afrika zimewasili nchini Equatorial Guinea wakati ambapo mechi za taifa bingwa barani zitarajiwa kung'oa nanga hii leo ikiwa ni miezi miwili tangu taifa hilo la afrika ya kati likubali kuandaa mechi hizo.
Morocco ndiyo iliokuwa iandae kombe hilo lakini badala yake ikaomba kuahirishwa kwake kutokana na hofu ya kusambaa kwa ugonjwa wa ebola.
Shirikisho la kandanda barani Afrika CAF hata hivyo lilikataa ombi hilo la Morocco
Mkuu wa CAF (Hicham El Amrani) anasema kuwa kila tahadhari imechukuliwa nchini Equatorial Guinea kuwalinda watu kutokana na ugonjwa wa ebola.
Mechi ya kwanza itakuwa kati ya wenyeji Equatorial Guinea na Congo.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni