Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Ijumaa, 16 Januari 2015

CAMEROON KUPAMBANA NA BOKO HARAM


Wapiganaji wa Boko Haram wamekuwa kero kubwa kwa wananchi wa Nigeria kwa miaka mingi sasa
Serikali ya Cameroon imesema Chad itatuma kikosi kikubwa cha wanajeshi wake kupambana na wapiganaji wa kiisilamu wa Boko Haram mpakani mwa Nigeria na nchi hio.
Tangazo hili limetolewa siku moja baada ya Chad kusema kwamba itaunga mkono jirani yake Nigeria katika harakati dhidi ya wapiganaji wa kiisilamu wa Boko Haram.
Hakuna taarifa zozote zimetolewa kuhusu idadi kamili ya wanajeshi watakaopelekwa huko au siku.
Mnamo siku ya Jumanne, Cameroon ilisema kwamba iliwaua wapiganaji 143 wa Boko Haram, ambao walishambulia kambi zake katika eneo la Kolofata karibu na mpaka na Nigeria.
Ilisema kuwa mwanajeshi mmoja alifariki wakati wa mashambulizi hayo ambayo yalisababisha ufyatulianaji risasi mkali kati ya wanajeshi na waasi hao kwa muda wa saa tano.
lilikuwa shambulizi la kwanza kubwa kufanywa na Boko Haram dhidi ya Cameroon tangu kundi hilo kutishia kiongozi wa nchi hio katika kanda ya video waliyoiweka kwenye mtandao mapema mwezi huu.
Wanamgambo hao wameteka miji na vijiji kadhaa ambavyo wanavidhibiti Kaskazini Mashariki mwa Nigeria katika harakati zao ambazo wameziendeleza kwa miaka sita sasa.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni