Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Ijumaa, 16 Januari 2015

WASHUKIWA KWA UGAIDI WAKAMATWA ULAYA




Msako barani ulaya kuwatafuta watu wenye itikadi kali za kidini 
Polisi katika nchi kadhaa barani Ulaya wamewakamata washukiwa kadhaa wenye iktikadi kali za kidini katika misako iliyofanywa usiku kucha.
Ripoti kutoka nchini Ufaransa zinasema kuwa washukiwa wanane wametiwa mbaroni, kuhusiana na mashambulio ya wiki iliyopita ambako watu kumi na saba waliuawa.
Afisa mmoja wa serikali ya nchi hiyo amesema kuwa washukiwa hao wanaendelea kuhojiwa kuhusiana na madai ya kuwasaidia washambuliaji kwa kuwabebea silaha au kuwapa usafiri .
Nchini Ujerumani, polisi wamewakamata washukiwa kadhaa wa ugaidi baada ya kufanya opereshenu kali mjini Berlin.
 
Mmoja wa waliokamatwa anashukiwa kuwa kiongozi wa kundi koja la kiislamu lenye itikadi kali ambalo lilikuwa likijiandaa kufanya mashambulio nchini Syria. Anadaiwa kuandaa mikutano ya kuchangisha pesa ili kuwasaidia wapiganaji wa Islamic State
Duru zinasema kwamba misako yote ilifanyika katika mtaa mmoja wa Kusini mwa Paris ambako mmoja wa washambuliaji alikulia.
Nchini Ujerumani, polisi wamewakamata washukiwa wa kundi la kigaidi baada ya kufanya misako mingine ndani na katika maeneo yanayozingira mji wa Berlin.
Hata hivyo polisi walisema hawakupata ushahidi kwamba walikuwa wanajiandaa kufanya mashambulizi nchini Ujerumani.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni